< Ayubu 3 >

1 Baada ya hayo, Ayubu akafunua kinywa chake na kuilani siku aliyozaliwa.
Depois disto abriu Job a sua boca, e amaldiçoou o seu dia.
2 Akasema,
E Job respondeu, e disse:
3 “Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'
Pereça o dia em que nasci, e a noite em que se disse: Foi concebido um homem!
4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu toka juu asiifikilie, wala mwanga usiiangazie.
Converta-se aquele dia em trevas; e Deus de cima não tenha cuidado dele, nem resplandeça sobre ele a luz.
5 Ishikwe na giza na giza la mauti liwe lake. Wingu na likae juu yake; kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza kweli na kiitishe.
Contaminem-no as trevas e a sombra de morte; habitem sobre ele nuvens: a escuridão do dia o espante!
6 Usiku huo, na ukamatwe na giza tororo. Usihesabiwe miongoni mwa siku za mwaka; na usiwekwe katika hesabu ya miezi.
A escuridão tome aquela noite, e não se goze entre os dias do ano, e não entre no número dos meses!
7 Tazama, usiku huo na uwe tasa; na sauti ya shangwe isiwe ndani yake.
Ah que solitária seja aquela noite, e suave música não entre nela!
8 Na wailani siku hiyo, hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathani.
Amaldiçoem-na aqueles que amaldiçoam o dia, que estão prontos para levantar o seu pranto.
9 Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza. Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate; wala makope ya mapambazuko isiyaone,
Escureçam-se as estrelas do seu crepúsculo; que espere a luz, e não venha: e não veja as pestanas dos olhos da alva!
10 kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu, na kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.
Porque não fechou as portas do ventre; nem escondeu dos meus olhos a canceira?
11 Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi? Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?
Porque não morri eu desde a madre? e em saindo do ventre, não expirei?
12 kwanini magoti yake yalinipokea? Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?
Porque me receberam os joelhos? e porque os peitos, para que mamasse?
13 Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimya kimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko
Porque já agora jazera e repousara; dormiria, e então haveria repouso para mim.
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, ambao walijijengea makaburi ambayo sasa ni magofu.
Com os reis e conselheiros da terra, que se edificavam casas nos lugares assolados,
15 Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha.
Ou com os príncipes que tinham ouro, que enchiam as suas casas de prata,
16 Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.
Ou como aborto oculto, não existiria: como as crianças que não viram a luz.
17 Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.
Ali os maus cessam de perturbar: e ali repousam os cançados.
18 Huko wafungwa kwa pamoja hupata amani; hawaisikii sauti ya msimamizi wa watumwa.
Ali os presos juntamente repousam, e não ouvem a voz do exator:
19 Wote wadogo na watu maarufu wako huko; mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.
Ali está o pequeno e o grande, e o servo fica livre de seu senhor.
20 Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai,
Porque se dá luz ao miserável, e vida aos amargosos de ânimo?
21 ambao hutamani mauti lakini hawapati; ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika?
Que esperam a morte, e não se acha: e cavam em busca dela mais do que de tesouros ocultos:
22 Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi?
Que de alegria saltam, e exultam, achando a sepultura:
23 Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?
Ao homem, cujo caminho é oculto, e a quem Deus o encobriu?
24 Kwa kuwa kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji.
Porque antes do meu pão vem o meu suspiro: e os meus gemidos se derramam como água.
25 Maana jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia.
Porque o temor que temo me veio: e o que receiava me aconteceu.
26 Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko; badala yake huja taabu.”
Nunca estive descançado, nem sosseguei, nem repousei, mas veio sobre mim a perturbação.

< Ayubu 3 >