< Ayubu 3 >

1 Baada ya hayo, Ayubu akafunua kinywa chake na kuilani siku aliyozaliwa.
After this Job opened his mouth, and cursed his day.
2 Akasema,
Job answered:
3 “Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'
"Let the day perish in which I was born, the night which said, 'A man is conceived.'
4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu toka juu asiifikilie, wala mwanga usiiangazie.
Let that day be darkness. May God above not care about it, neither let the light shine on it.
5 Ishikwe na giza na giza la mauti liwe lake. Wingu na likae juu yake; kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza kweli na kiitishe.
Let darkness and the shadow of death claim it for their own. Let a cloud dwell on it. Let the blackness of the day terrify it.
6 Usiku huo, na ukamatwe na giza tororo. Usihesabiwe miongoni mwa siku za mwaka; na usiwekwe katika hesabu ya miezi.
As for that night, let thick darkness seize on it. Let it not rejoice among the days of the year. Let it not come into the number of the months.
7 Tazama, usiku huo na uwe tasa; na sauti ya shangwe isiwe ndani yake.
Look, let that night be barren. Let no joyful voice come in it.
8 Na wailani siku hiyo, hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathani.
Let them curse it who curse the day, who are ready to rouse up leviathan.
9 Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza. Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate; wala makope ya mapambazuko isiyaone,
Let the stars of its twilight be dark. Let it look for light, but have none, neither let it see the eyelids of the morning,
10 kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu, na kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.
because it did not shut up the doors of my mother's womb, nor did it hide trouble from my eyes.
11 Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi? Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?
"Why did I not die from the womb? Why did I not give up the spirit when my mother bore me?
12 kwanini magoti yake yalinipokea? Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?
Why did the knees receive me? Or why the breast, that I should suck?
13 Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimya kimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko
For now should I have lain down and been quiet. I should have slept, then I would have been at rest,
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, ambao walijijengea makaburi ambayo sasa ni magofu.
with kings and counselors of the earth, who built up waste places for themselves;
15 Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha.
or with princes who had gold, who filled their houses with silver:
16 Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.
or as a hidden untimely birth I had not been, as infants who never saw light.
17 Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.
There the wicked cease from troubling. There the weary are at rest.
18 Huko wafungwa kwa pamoja hupata amani; hawaisikii sauti ya msimamizi wa watumwa.
There the prisoners are at ease together. They do not hear the voice of the taskmaster.
19 Wote wadogo na watu maarufu wako huko; mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.
The small and the great are there. The servant is free from his master.
20 Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai,
"Why is light given to him who is in misery, life to the bitter in soul,
21 ambao hutamani mauti lakini hawapati; ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika?
Who long for death, but it doesn't come; and dig for it more than for hidden treasures,
22 Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi?
who rejoice exceedingly, and are glad, when they can find the grave?
23 Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?
Why is light given to a man whose way is hid, whom God has hedged in?
24 Kwa kuwa kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji.
For my sighing comes before I eat. My groanings are poured out like water.
25 Maana jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia.
For the thing which I fear comes on me, That which I am afraid of comes to me.
26 Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko; badala yake huja taabu.”
I am not at ease, neither am I quiet, neither have I rest; but trouble comes."

< Ayubu 3 >