< Ayubu 28 >

1 Hakika kuna machimbo ya fedha, wanaposafisha dhahabu.
Habet argentum, venarum suarum principia: et auro locus est, in quo conflatur.
2 Chuma uchimbwa; shaba uyeyushwa kutoka katika jiwe.
Ferrum de terra tollitur: et lapis solutus calore, in æs vertitur.
3 Mtu anaondoa giza na kutafuta, katika mpaka wa mbali, mawe hayaonekani na giza totoro.
Tempus posuit tenebris, et universorum finem ipse considerat, lapidem quoque caliginis, et umbram mortis.
4 Huchimba shimo mbali na makazi ya watu, mahali pasipopitwa na mtu. Huning'inia mbali na watu; uharakisha kwenda na kurudi.
Dividit torrens a populo peregrinante, eos, quos oblitus est pes egentis hominis, et invios.
5 Kwa nchi, kizalishwapo chakula, inapinduliwa kama kwa moto.
Terra, de qua oriebatur panis in loco suo, igni subversa est.
6 Mawe yake yana johari, na vumbi lake lina dhahabu.
Locus sapphiri lapides eius, et glebæ illius aurum.
7 Hata ndege mwindaji hapajui, wala jicho la kipanga halijapaona.
Semitam ignoravit avis, nec intuitus est eam oculus vulturis.
8 Ndege mwenye majivuna hajawai kuiona njia hiyo, wala simba mkali kupita pale.
Non calcaverunt eam filii institorum, nec pertransivit per eam leæna.
9 Mtu huchimba mwamba mgumu; hupindua milima katika vyanzo vyake.
Ad silicem extendit manum suam, subvertit a radicibus montes.
10 Huweka njia katika miamba; macho yake pale kila kilicho cha thamani.
In petris rivos excidit, et omne pretiosum vidit oculus eius.
11 Hufunga vyanzo hata wasiondoke; kilichofichika pale hukifunua.
Profunda quoque fluviorum scrutatus est, et abscondita in lucem produxit.
12 Hekima itakuwa wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
Sapientia vero ubi invenitur? et quis est locus intelligentiæ?
13 Mtu hafahamu thamani yake; wala haipatikani katika nchi ya walio hai.
Nescit homo pretium eius, nec invenitur in terra suaviter viventium.
14 Vilindi vya maji chini ya nchi husema, 'Haiko kwangu'; bahari husema, 'Haipo pamoja nami.'
Abyssus dicit: Non est in me: et mare loquitur: Non est mecum.
15 Hainunuliwi kwa dhahabu; wala hailinganishwi na fedha.
Non dabitur aurum obrizum pro ea, nec appendetur argentum in commutatione eius.
16 Haiwezi kuthamanishwa na dhahabu ya Ofiri, kwa jiwe jeusi la thamani au johari.
Non conferetur tinctis Indiæ coloribus, nec lapidi sardonycho pretiosissimo, vel sapphiro.
17 Dhahabu na fuwele hailingani nayo kwa thamani; wala haiwezi kubadilishwa kwa vito vya dhahabu safi.
Non adæquabitur ei aurum vel vitrum, nec commutabuntur pro ea vasa auri:
18 Hailinganishwi na marijani wala yaspi; hakika, thamani ya hekima inapita madini ya rubi.
Excelsa et eminentia non memorabuntur comparatione eius: trahitur autem sapientia de occultis.
19 Topazi ya Ethiopia hailinganishwi nayo; wala kuthamanishwa kwa dhahabu safi.
Non adæquabitur ei topazius de Æthiopia, nec tincturæ mundissimæ componetur.
20 Je hekima inatoka wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
Unde ergo sapientia venit? et quis est locus intelligentiæ?
21 Hekima imejificha mbali na macho ya viumbe wote na ndege wa angani.
Abscondita est ab oculis omnium viventium, volucres quoque cæli latet.
22 Mauti na uharibifu husema, 'Tumesikia tu tetesi kwa masikio yetu.'
Perditio et mors dixerunt: Auribus nostris audivimus famam eius.
23 Mungu hufahamu njia ya kuipata; anapafahamu ilipo.
Deus intelligit viam eius, et ipse novit locum illius.
24 Kwani uona miisho yote ya dunia na huona chini ya mbingu zote.
Ipse enim fines mundi intuetur: et omnia, quæ sub cælo sunt, respicit.
25 Hapo kale, alifanya nguvu za upepo na kuyagawanya maji kwa kipimo.
Qui fecit ventis pondus, et aquas appendit in mensura.
26 Aliiwekea mvua tamko na njia ya radi na munguromo.
Quando ponebat pluviis legem, et viam procellis sonantibus:
27 Kisha akaiona hekima na kuitangaza; aliianzisha, bila shaka, na kuipima.
Tunc vidit illam, et enarravit, et præparavit, et investigavit.
28 Aliwambia watu, 'Tazameni, kumcha Bwana - ni hekima; kuacha uovu ni ufahamu.”
Et dixit homini: Ecce timor Domini, ipsa est sapientia: et recedere a malo, intelligentia.

< Ayubu 28 >