< Ayubu 25 >

1 Kisha Bilidadi Mshuhi akajibu na kusema, 2 “Utawala na hofu vipo naye; anaagiza mahali pa juu pake mbinguni. 3 Je kuna idadi ya majeshi yake? Ni wapi pasipo na nuru yake? 4 Jinsi gani basi mtu awe mwenye haki kama Mungu? Jinsi gani aliyezaliwa na mwanamke awe safi, amekubaliwa naye? 5 Tazama, hata mwezi kwake haungazii; nyota hazikosafi mbele zake. 6 Ni vipi mtu, aliyemdudu - mwana wa mtu, aliye mdudu!”

< Ayubu 25 >