< Ayubu 23 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Then Job answered and said:
2 “Hata leo malalamiko yangu ni machungu; maumivu yangu ni mazito kuliko manung'uniko yangu.
Even to-day is my complaint bitter; my hand is become heavy because of my groaning.
3 Ee, ningejua niwezapokumwona! Ee, kwamba ningeweza kwenda alipo!
Oh that I knew where I might find Him, that I might come even to His seat!
4 Ningeweka shitaka langu mbele yake na kukijaza kinywa changu hoja.
I would order my cause before Him, and fill my mouth with arguments.
5 Ningejua ambavyo angenijibu na kufahamu ambavyo angesema juu yangu.
I would know the words which He would answer me, and understand what He would say unto me.
6 Je angehojiana nami katika ukuu wa nguvu zake? Hapana, angenisikiliza.
Would He contend with me in His great power? Nay; but He would give heed unto me.
7 Pale mwenye haki angehojiana nami. Kwa njia hii ningeonekana bila hatia kwa mwamzi wangu.
There the upright might reason with Him; so should I be delivered for ever from my Judge.
8 Tazama, naelekea mashariki, lakini hayupo pale, na upande wa magharibi, lakini siwezi kumwona.
Behold, I go forward, but He is not there, and backward, but I cannot perceive Him;
9 Kaskazini, anapofanya kazi, lakini siwezi kumwona, na kusini, anapojificha hata nisimwone.
On the left hand, when He doth work, but I cannot behold Him, He turneth Himself to the right hand, but I cannot see Him.
10 Lakini anaijua njia ninayoichukua; atakapokuwa amenipima, nitatoka kama dhahabu.
For He knoweth the way that I take; when He hath tried me, I shall come forth as gold.
11 Mguu wangu umeunganishwa na hatua zake; nimezitunza njia zake na sijageuka.
My foot hath held fast to His steps, His way have I kept, and turned not aside.
12 Sijaiacha amri ya midomo yake; nimeyatii maneno ya kinywa chake.
I have not gone back from the commandment of His lips; I have treasured up the words of His mouth more than my necessary food.
13 Lakini yeye ni wa pekee, naniawezaye kumgeuza? Analolitaka, hulitenda.
But He is at one with Himself, and who can turn Him? And what His soul desireth, even that He doeth.
14 Kwa maana hulitimiza agizo lake kinyume changu; anamipango mingi kwa ajili yangu; ipo mingi kama hiyo.
For He will perform that which is appointed for me; and many such things are with Him.
15 Kwa hiyo, nimetishwa mbele zake; ninapofikiri kumhusu, ninamwogopa.
Therefore am I affrighted at His presence; when I consider, I am afraid of Him.
16 Kwani Mungu ameudhoofisha moyo wangu; Mwenyezi amenitisha.
Yea, God hath made my heart faint, and the Almighty hath affrighted me;
17 Si kwa sababu nimeondolewa na giza, wala siyo kwamba giza nene limeufunika uso wangu.
Because I was not cut off before the darkness, neither did He cover the thick darkness from my face.

< Ayubu 23 >