< Ayubu 21 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Entonces Job respondió:
2 “Sikilizeni hotuba yangu kwa makini, hii na iwe faraja yenu.
Escuchen con atención mis palabras, y que sea esto el consuelo que me den.
3 Nimeteswa, lakini pia nitasema; nikisha kusema, endeleeni kudhihaki.
Tolérenme mientras hablo, y después que hable, búrlense.
4 Lakini kwangu mimi, malalamikio yangu ni kwa mtu? Kwa nini nisiwe mwenye subira?
¿Me quejo ante un hombre? ¿Por qué no se debe impacientar mi espíritu?
5 Nitazameni na mshangae, nanyi wekeni mkono wenu midomoni mwenu.
Mírenme, asómbrense y coloquen la mano sobre su boca.
6 Ninapoyafikiria mateso yangu, ninaumizwa, mwili wangu unaogopa.
Cuando lo recuerdo me asombro, y el horror estremece mi carne.
7 Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wanazeeka, na kuwa na uwezo katika madaraka?
¿Por qué viven los perversos, envejecen y son poderosos?
8 Wazao wao wanathibitishwa mbele zao, na uzao wao unaimarika machoni pao.
Sus descendientes se establecen con ellos y ante ellos. Sus hijos están ante ellos.
9 Nyumba zao ziko salama mbali na hofu; wala fimbo ya Mungu haiko juu yao.
Sus casas están libres de temor. No tienen azote de ʼElohim sobre ellos.
10 Dume lao la ng'ombe linazalisha; halishindwi kufanya hivyo; ng'ombe wao anazaa na hafishi ndama wake akiwa mchanga.
Su toro fecunda sin fallar, sus vacas paren y no pierden crías.
11 Wanawapeleka wadogo wao kama kundi la kondoo, na watoto wao hucheza.
Sueltan a sus pequeños como manada y sus hijos andan saltando.
12 Wanaimba kwa tari na vinubi na hufurahi kwa muziki na zomari.
Cantan al son del tamboril y el arpa. Se regocijan con el sonido de la flauta.
13 Wanatumia siku zao katika mafanikio, na wanashuka kuzimu kwa utulivu. (Sheol h7585)
Sus días transcurren en prosperidad. Con tranquilidad bajan al Seol. (Sheol h7585)
14 Wanamwambia Mungu, 'Ondoka kwetu kwani hatutaki ufahamu wowote juu ya njia zako.
Ellos dicen a ʼElohim: Apártate de nosotros. Ni siquiera deseamos el conocimiento de tus caminos.
15 Mwenye enzi ni nani, hata tumwabudu? Tutafaidika na nini tukimwabudu? Tutapata faida gani ikiwa tutamwomba?
¿Quién es ʼEL-Shadday para que le sirvamos, y de qué nos aprovecha que le supliquemos?
16 Tazama, je mafanikio yao hayamo katika mikono yao wenyewe? Sina cha kufanya na ushauri wa waovu.
Ciertamente, la prosperidad de ellos no está en sus propias manos. El consejo de los perversos esté lejos de mí.
17 Mara ngapi taa za waovu huzimwa, au kwamba majanga huja juu yao? Mara ngapi inatokea kwamba Mungu husambaza huzuni kwao kwa hasira?
¿Cuántas veces es apagada la lámpara de los perversos, o su calamidad cae sobre ellos, o ʼElohim les reparte destrucción en su ira?
18 Ni mara ngapi inatokea kwamba wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba?
¿Son como concha de grano trillado llevada por el viento, y como pasto que arrebata la tormenta?
19 Mnasema, 'Mungu huweka hatia ya mtu kwa watoto wake kuilipa.' Na alipe yeye mwenyewe, ili kwamba aweze kujua hatia yake mwenyewe.
Ustedes dicen: ʼElohim guarda la perversidad del hombre para sus hijos. ¡Que ʼElohim le retribuya para que aprenda!
20 Acha macho yake yaone uangamivu wake mwenyewe, na acha anywe gadhabu ya Mwenyezi.
¡Vean sus ojos su ruina, y beba él mismo de la ira de ʼEL-Shadday!
21 Kwani anaangaliaje familia yake mbele yake idadi ya miezi yake inapokwisha.
Pues después que muera y acabe la cuenta de sus meses, ¿qué le importa su familia?
22 Je kuna mtu anaweza kumfundisha Mungu maarifa kwa kuwa yeye huwaukumu hata walio juu?
¿Puede alguno enseñar conocimientos a ʼElohim, puesto que Él juzga a los que están en las alturas?
23 Mtu mmoja ufa katika nguvu zake kamili, akiwa na utulivu kabisa na kwa amani.
Un hombre muere en la plenitud de su vigor, completamente tranquilo y en paz,
24 Mwili wake hauna uhitaji, na kiini cha mifupa yake ina unyevu na afya njema.
con las cavidades internas llenas de grasa y la médula de sus huesos bien nutrida.
25 Mtu mwingine ufa kwa uchungu wa nafsi, bila kujifurahisha kwa jambo lolote jema.
Otro muere con el alma amargada, sin comer jamás con gusto.
26 Wanazikwa kaburini wote kwa pamoja, funza wanawafunika wote.
Juntamente están tendidos en el polvo, y los gusanos los cubren.
27 Tazama, nayajua mawazo yenu, na jinsi mnavyotaka kunikosesha.
Ciertamente conozco los pensamientos de ustedes, y sus estratagemas contra mí.
28 Kwa kuwa mwasema, 'Iko wapi sasa nyumba ya mwana wa mfalme? Liko wapi kao alipokaa mwovu?'
Sé que dicen: ¿Dónde está la casa del que era poderoso, y la vivienda en la cual vivían los perversos?
29 Je hamjawauliza wasafiri? Hamfahamu wanavyoweza kusema,
¿Por qué no lo preguntan a los viajeros, ni han consultado su respuesta?
30 kwamba mwovu anaepushwa na siku ya shida, na kwamba anawekwa mbali na siku ya gadhabu?
Porque el perverso es preservado en el día de la calamidad, y se lo excluye del día de la ira.
31 Ni nani atakaye ituhumu siku ya mwovu mbele yake? Ni nani atakayemwadhibu kwa alichokifanya?
¿Quién le denuncia en la cara su camino? Y lo que hizo, ¿quién se lo retribuye?
32 Hata hivyo atapelekwa kaburini; watu wataliona kaburi lake.
Porque es conducido al sepulcro, y sobre su tumba se hará vigilancia,
33 Udongo wa bondeni utakuwa mtamu kwake; watu wote watamfuata, hata kuwe na watu wengi mbele yake.
y junto a la tumba magnífica se monta guardia. Así, tras él, todo el mundo desfila, y adelante de él, otros sinnúmero.
34 Ni jinsi gani basi mtanifariji bila kufikiri, kwa kuwa majibu yenu hayana lolote ila uongo?”
¿Cómo pueden ustedes consolarme con palabras vacías y fútiles, puesto que en sus respuestas solo hay falsedad?

< Ayubu 21 >