< Ayubu 21 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Then Job answered and said:
2 “Sikilizeni hotuba yangu kwa makini, hii na iwe faraja yenu.
Hear diligently my speech; and let this be your consolations.
3 Nimeteswa, lakini pia nitasema; nikisha kusema, endeleeni kudhihaki.
Suffer me, that I may speak; and after that I have spoken, mock on.
4 Lakini kwangu mimi, malalamikio yangu ni kwa mtu? Kwa nini nisiwe mwenye subira?
As for me, is my complaint to man? Or why should I not be impatient?
5 Nitazameni na mshangae, nanyi wekeni mkono wenu midomoni mwenu.
Turn unto me, and be astonished, and lay your hand upon your mouth.
6 Ninapoyafikiria mateso yangu, ninaumizwa, mwili wangu unaogopa.
Even when I remember I am affrighted, and horror hath taketh hold on my flesh.
7 Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wanazeeka, na kuwa na uwezo katika madaraka?
Wherefore do the wicked live, become old, yea, wax mighty in power?
8 Wazao wao wanathibitishwa mbele zao, na uzao wao unaimarika machoni pao.
Their seed is established in their sight with them, and their offspring before their eyes.
9 Nyumba zao ziko salama mbali na hofu; wala fimbo ya Mungu haiko juu yao.
Their houses are safe, without fear, neither is the rod of God upon them.
10 Dume lao la ng'ombe linazalisha; halishindwi kufanya hivyo; ng'ombe wao anazaa na hafishi ndama wake akiwa mchanga.
Their bull gendereth, and faileth not; their cow calveth, and casteth not her calf.
11 Wanawapeleka wadogo wao kama kundi la kondoo, na watoto wao hucheza.
They send forth their little ones like a flock, and their children dance.
12 Wanaimba kwa tari na vinubi na hufurahi kwa muziki na zomari.
They sing to the timbrel and harp, and rejoice at the sound of the pipe.
13 Wanatumia siku zao katika mafanikio, na wanashuka kuzimu kwa utulivu. (Sheol h7585)
They spend their days in prosperity, and peacefully they go down to the grave. (Sheol h7585)
14 Wanamwambia Mungu, 'Ondoka kwetu kwani hatutaki ufahamu wowote juu ya njia zako.
Yet they said unto God: 'Depart from us; for we desire not the knowledge of Thy ways.
15 Mwenye enzi ni nani, hata tumwabudu? Tutafaidika na nini tukimwabudu? Tutapata faida gani ikiwa tutamwomba?
What is the Almighty, that we should serve Him? And what profit should we have, if we pray unto Him?' —
16 Tazama, je mafanikio yao hayamo katika mikono yao wenyewe? Sina cha kufanya na ushauri wa waovu.
Lo, their prosperity is not in their hand; the counsel of the wicked is far from me.
17 Mara ngapi taa za waovu huzimwa, au kwamba majanga huja juu yao? Mara ngapi inatokea kwamba Mungu husambaza huzuni kwao kwa hasira?
How oft is it that the lamp of the wicked is put out? that their calamity cometh upon them? that He distributeth pains in His anger?
18 Ni mara ngapi inatokea kwamba wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba?
That they are as stubble before the wind, and as chaff that the storm stealeth away?
19 Mnasema, 'Mungu huweka hatia ya mtu kwa watoto wake kuilipa.' Na alipe yeye mwenyewe, ili kwamba aweze kujua hatia yake mwenyewe.
'God layeth up his iniquity for his children!' — let Him recompense it unto himself, that he may know it.
20 Acha macho yake yaone uangamivu wake mwenyewe, na acha anywe gadhabu ya Mwenyezi.
Let his own eyes see his destruction, and let him drink of the wrath of the Almighty.
21 Kwani anaangaliaje familia yake mbele yake idadi ya miezi yake inapokwisha.
For what pleasure hath he in his house after him? seeing the number of his months is determined.
22 Je kuna mtu anaweza kumfundisha Mungu maarifa kwa kuwa yeye huwaukumu hata walio juu?
Shall any teach God knowledge? seeing it is He that judgeth those that are high.
23 Mtu mmoja ufa katika nguvu zake kamili, akiwa na utulivu kabisa na kwa amani.
One dieth in his full strength, being wholly at ease and quiet;
24 Mwili wake hauna uhitaji, na kiini cha mifupa yake ina unyevu na afya njema.
His pails are full of milk, and the marrow of his bones is moistened.
25 Mtu mwingine ufa kwa uchungu wa nafsi, bila kujifurahisha kwa jambo lolote jema.
And another dieth in bitterness of soul, and hath never tasted of good.
26 Wanazikwa kaburini wote kwa pamoja, funza wanawafunika wote.
They lie down alike in the dust, and the worm covereth them.
27 Tazama, nayajua mawazo yenu, na jinsi mnavyotaka kunikosesha.
Behold, I know your thoughts, and the devices which ye wrongfully imagine against me.
28 Kwa kuwa mwasema, 'Iko wapi sasa nyumba ya mwana wa mfalme? Liko wapi kao alipokaa mwovu?'
For ye say: 'Where is the house of the prince? And where is the tent wherein the wicked dwelt?'
29 Je hamjawauliza wasafiri? Hamfahamu wanavyoweza kusema,
Have ye not asked them that go by the way; and will ye misdeem their tokens,
30 kwamba mwovu anaepushwa na siku ya shida, na kwamba anawekwa mbali na siku ya gadhabu?
That the evil man is reserved to the day of calamity, that they are led forth to the day of wrath?
31 Ni nani atakaye ituhumu siku ya mwovu mbele yake? Ni nani atakayemwadhibu kwa alichokifanya?
But who shall declare his way to his face? And who shall repay him what he hath done?
32 Hata hivyo atapelekwa kaburini; watu wataliona kaburi lake.
For he is borne to the grave, and watch is kept over his tomb.
33 Udongo wa bondeni utakuwa mtamu kwake; watu wote watamfuata, hata kuwe na watu wengi mbele yake.
The clods of the valley are sweet unto him, and all men draw after him, as there were innumerable before him.
34 Ni jinsi gani basi mtanifariji bila kufikiri, kwa kuwa majibu yenu hayana lolote ila uongo?”
How then comfort ye me in vain? And as for your answers, there remaineth only faithlessness?

< Ayubu 21 >