< Ayubu 20 >

1 Ndipo Sofari, Mnaamathi alijibu na kusema,
Then answered Zophar the Naamathite, and said,
2 “Mawazo yangu yananifanya mimi nijibu kwa haraka kwa sababu ya mashaka yaliyomo ndani yangu mimi.
Therefore do my thoughts give answer to me, even by reason of my haste that is in me.
3 Mimi ninasikia kukemewa ambako kunaniondolea heshima mimi, lakini roho kutoka katika ufahamu wangu hunijibu mimi.
I have heard the reproof which putteth me to shame, and the spirit of my understanding answereth me.
4 Je, unafahamu kwamba ukweli huu kutoka enzi za kale, wakati Mungu alipomweka mwanadamu juu ya nchi:
Knowest thou [not] this of old time, since man was placed upon earth,
5 ushindi wa mtu mwovu ni mfupi, na furaha ya mtu asiyemcha Mungu hudumu kwa kitambo tu?
That the triumphing of the wicked is short, and the joy of the godless but for a moment?
6 Ingawa urefu wake yeye hufikia juu kwenye mbingu, na kichwa chake yeye kufikia kwenye mawingu,
Though his excellency mount up to the heavens, and his head reach unto the clouds;
7 bado mtu huyo atapotea siku zote kama mavi yake yeye mwenyewe; wale waliokuwa wamemuona yeye watasema, 'Yuko wapi yeye'?
Yet he shall perish for ever like his own dung: they which have seen him shall say, Where is he?
8 Yeye atapaa mbali kama ndoto na hataonekana; ndivyo ilivyo, yeye atakuwa amefukuzwa mbali kama ono la
He shall fly away as a dream, and shall not be found: yea, he shall be chased away as a vision of the night.
9 usiku. Jicho ambalo lilimuona yeye halitamuona yeye tena; mahali pake hapatamuona yeye tena.
The eye which saw him shall see him no more; neither shall his place any more behold him.
10 Watoto wake wataomba msamaha kwa watu maskini, mikono yake itaweza kurudisha utajiri wake.
His children shall seek the favour of the poor, and his hands shall give back his wealth.
11 Mifupa yake imejaa nguvu za ujanani, lakini zitalala naye chini katika mavumbi.
His bones are full of his youth, but it shall lie down with him in the dust.
12 Japokuwa uovu ni mtamu katika mdomo wake yeye, japokuwa yeye anauficha chini ya ulimi wake yeye,
Though wickedness be sweet in his mouth, though he hide it under his tongue;
13 japokuwa anaushikilia pale na hauruhusu kwenda lakini bado huushikilia katika mdomo wake yeye -
Though he spare it, and will not let it go, but keep it still within his mouth;
14 chakula katika koromeo lake yeye hugeuka kuwa uchungu; hugeuka kuwa sumu ya majoka ndani yake yeye.
Yet his meat in his bowels is turned, it is the gall of asps within him.
15 Yeye humeza chini utajiri, lakini yeye atautapika tena; Mungu atautoa nje kutoka katika tumbo lake yeye.
He hath swallowed down riches, and he shall vomit them up again: God shall cast them out of his belly.
16 Yeye atamumunya sumu ya majoka; ulimi wa nyoka mwenye sumu utamwua yeye.
He shall suck the poison of asps: the viper’s tongue shall slay him.
17 Yeye hatafurahia vijito vya maji, wingi wa asali na siagi.
He shall not look upon the rivers, the flowing streams of honey and butter.
18 Yeye atayarudisha matunda ya kazi yake na hataweza kuyala; yeye hatafurahia utajiri alioupata kwa biashara zake yeye.
That which he laboured for shall he restore, and shall not swallow it down; according to the substance that he hath gotten, he shall not rejoice.
19 Kwa kuwa yeye amewakandamiza na kuwasahau watu maskini; yeye kwa uonevu, amezichukua mbali nyumba ambazo hakuzijenga yeye.
For he hath oppressed and forsaken the poor; he hath violently taken away an house, and he shall not build it up.
20 Kwa sababu yeye mwenyewe hakujua utoshelevu wowote, yeye hataweza kuokoa kitu chochote katika kile ambacho alijifurahisha.
Because he knew no quietness within him, he shall not save aught of that wherein he delighteth.
21 Hakuna chochote kilichoachwa ambacho yeye hakukimeza; kwa hiyo mafanikio yake yeye hayatakuwa ya kudumu.
There was nothing left that he devoured not; therefore his prosperity shall not endure.
22 katika wingi wa utajiri wake yeye ataanguka katika mahangaiko; mkono wa kila mmoja ambaye yuko katika umaskini utakuja kinyume chake yeye.
In the fulness of his sufficiency he shall be in straits: the hand of every one that is in misery shall come upon him.
23 Wakati akiwa katika kulijaza tumbo lake, Mungu atatupa hasira ya ghadhabu yake juu yake yeye; Mungu ataunyeshea chini juu yake yeye wakati yeye anakula.
When he is about to fill his belly, [God] shall cast the fierceness of his wrath upon him, and shall rain it upon him while he is eating.
24 Ingawa mtu huyo atakimbia kutoka katika silaha ya chuma, upinde wa shaba utampiga yeye.
He shall flee from the iron weapon, and the bow of brass shall strike him through.
25 Mshale utatoboa kupitia mgongoni mwake na utatokezea; ni dhahiri, ncha inayong'ra itatokezea nje kupitia ini lake yeye; watesi huja tena juu yake.
He draweth it forth, and it cometh out of his body: yea, the glittering point cometh out of his gall; terrors are upon him.
26 Giza lliilo kamilika limetunzwa kwa akiba zake; moto usiopulizwa utamla yeye kwa haraka; utameza kile kilichoachwa katika hema yake.
All darkness is laid up for his treasures: a fire not blown [by man] shall devour him; it shall consume that which is left in his tent.
27 Mbingu zitauweka wazi uovu wake, na nchi itainuka juu dhidi yake yeye kama shahidi.
The heavens shall reveal his iniquity, and the earth shall rise up against him.
28 Utajiri wa nyumba yake utatoweka; bidhaa zake zitamwagika mbali siku ya ghadhabu ya Mungu.
The increase of his house shall depart, [his goods] shall flow away in the day of his wrath.
29 Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu kutoka kwa Mungu, urithi uliotunzwa akiba na Mungu kwa ajili yake yeye.”
This is the portion of a wicked man from God, and the heritage appointed unto him by God.

< Ayubu 20 >