< Ayubu 19 >

1 Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
Then Job answered and said:
2 lini mtanifanya mimi kuteseka na kunivunja vunja mimi vipande vipnde kwa maneno?
How long will ye vex my soul, and crush me with words?
3 Mara kumi hivi mmenishutumu mimi; ninyi hamuoni aibu kwamba mmenitendea mimi kwa ukatili.
These ten times have ye reproached me; ye are not ashamed that ye deal harshly with me.
4 Kama ni dhahiri kweli mimi nimekosa, makosa yangu hubaki kuwa wajibu wangu.
And be it indeed that I have erred, mine error remaineth with myself.
5 Kama ni dhahiri ninyi mtajiinua juu yangu mimi na kuutumia uvumilivu wangu kunipinga mimi,
If indeed ye will magnify yourselves against me, and plead against me my reproach;
6 kisha ninyi mnapaswa kutambua kwamba Mungu amefanya mabaya kwangu mimi na amenikamata mimi katika mtego wake yeye.
Know now that God hath subverted my cause, and hath compassed me with His net.
7 Tazama, Mimi ninalia kwa sauti, “dhuluma!” lakini sipati jibu. Mimi ninaita kwa ajili ya msaada, lakini hakuna haki.
Behold, I cry out: 'Violence!' but I am not heard; I cry aloud, but there is no justice.
8 Yeye ameiwekea ukuta njia yangu, ili kwamba mimi nisiweze kupita, na yeye ameweka giza katika njia yangu.
He hath fenced up my way that I cannot pass, and hath set darkness in my paths.
9 Yeye ameniondoa Mimi kutoka katika utukufu wangu, na ameichukua taji kutoka kwenye kichwa changu mimi.
He hath stripped me of my glory, and taken the crown from my head.
10 Yeye amenivunjavunja mimi chini kwa kila upande, na Mimi nimetoweka; yeye amelikokota juu tumaini langu kama mti.
He hath broken me down on every side, and I am gone; and my hope hath He plucked up like a tree.
11 Yeye pia ameiongeza ghadhabu yake dhidi yangu mimi; yeye ananihesabu mimi kama mmoja wa adui zake.
He hath also kindled His wrath against me, and He counteth me unto Him as one of His adversaries.
12 Majeshi yake huja juu pamoja; wao wananikosesha tumaini kwa kuniteka nyara kwa kundi kubwa kupigana na mimi wakizunguka hema yangu.
His troops come on together, and cast up their way against me, and encamp round about my tent.
13 Yeye amewaweka ndugu zangu mbali kutoka kwangu mimi; watu wangu wa karibu wote wamejitenga kutoka kwangu mimi.
He hath put my brethren far from me, and mine acquaintance are wholly estranged from me.
14 Vizazi vyangu vimeniangusha mimi; rafiki zangu wa karibu wamenisahamu mimi.
My kinsfolk have failed, and my familiar friends have forgotten me.
15 Wale ambao mwanzoni walikaa kama wageni ndani ya nyumba yangu na watumishi wangu wa kike, hunihesabu mimi kama mgeni. Mimi nimekuwa mgeni katika macho yao.
They that dwell in my house, and my maids, count me for a stranger; I am become an alien in their sight.
16 Mimi ninamwita mtumishi wangu, lakini yeye hanipi jibu japokuwa Mimi nimemsihi yeye kwa midomo yangu.
I call unto my servant, and he giveth me no answer, though I entreat him with my mouth.
17 Pumzi yangu mimi ni chukizo kwa mke wangu; Hata mimi ninachukiwa na wale ambao walizaliwa kutoka katika tumbo la mama yangu mimi.
My breath is abhorred of my wife, and I am loathsome to the children of my tribe.
18 Hata watoto wachanga wananichukia mimi; ikiwa Mimi nitainuka kuzungumza, wao huzungumza dhidi yangu mimi.
Even urchins despised me; if I arise, they speak against me.
19 Rafiki zangu wote ninaowazoea wananichukia sana mimi; wale ambao Mimi ninawapenda wamegeuka kinyume na mimi.
All my intimate friends abhor me; and they whom I loved are turned against me.
20 Mifupa yangu inashikamana kwenye ngozi yangu na kwenye mwili wangu; Mimi ninaishi tu kwa ngozi ya meno yangu.
My bone cleaveth to my skin and to my flesh, and I am escaped with the skin of my teeth.
21 Iweni na huruma juu yangu mimi, muwe na huruma juu yangu mimi, rafiki zangu, kwa maana mkono wa Mungu umenigusa mimi.
Have pity upon me, have pity upon me, O ye my friends; for the hand of God hath touched me.
22 Kwa nini mnanitesa mimi kama ninyi mlikuwa Mungu? kwa nini hamjatosheka bado kwa kula mwili wangu?
Why do ye persecute me as God, and are not satisfied with my flesh?
23 Laiti, hayo maneno yangu yangekuwa yameandikwa chini! Laiti, hayo yangekuwa yameandikwa katika kitabu!
Oh that my words were now written! Oh that they were inscribed in a book!
24 Laiti, kwa kalamu ya chuma na risasi hayo yangekuwa yamechorwa katika mwamba siku zote!
That with an iron pen and lead they were graven in the rock for ever!
25 Lakini kama ilivyo kwangu mimi, Mimi ninafahamu kwamba mkombozi wangu anaishi, na kwamba hata mwisho atasimama katika nchi;
But as for me, I know that my Redeemer liveth, and that He will witness at the last upon the dust;
26 baada ya ngozi yangu, hivyo ndivyo, mwili huu, unaharibiwa, ndipo katika mwili wangu mimi Nitamwona Mungu.
And when after my skin this is destroyed, then without my flesh shall I see God;
27 Mimi nitamwona yeye kwa macho yangu mwenyewe-Mimi, na siyo mtu mwingine. Moyo wangu hushindwa ndani yangu mimi.
Whom I, even I, shall see for myself, and mine eyes shall behold, and not another's. My reins are consumed within me.
28 Kama mnatasema, 'Kwa jinsi gani tutamtesa yeye? Mzizi wa mahangaiko yake unakaa katika yeye;
If ye say: 'How we will persecute him!' seeing that the root of the matter is found in me;
29 ndipo uwe umeogopeshwa kwa ule upanga, kwa sababu ghadhabu huleta hukumu ya upanga, hivyo kwamba wewe uweze kutambua kuna hukumu.”
Be ye afraid of the sword; for wrath bringeth the punishments of the sword, that ye may know there is a judgment.

< Ayubu 19 >