< Ayubu 18 >

1 Ndipo Bildadi Mshuhi alijibu na kusema, “
Then Bildad the Shuhite answered,
2 Je, lini utaacha kusema kwako? Fikiri, na baadaye tutazungumza.
"How long will you hunt for words? Consider, and afterwards we will speak.
3 Kwa nini sisi tumehesabiwa kama wanyama mwitu; kwa nini tumekuwa wapumbavu machoni pako?
Why are we counted as animals, which have become unclean in your sight?
4 Wewe ambaye wajirarua mwenyewe katika hasira yako, nchi haipaswi kuachwa kwa ajili yako au miamba inapaswa kuondolewa kutoka mahali pake?
You who tear yourself in your anger, shall the earth be forsaken for you? Or shall the rock be removed out of its place?
5 Ni dhahiri, nuru ya watu waovu itawekwa nje; cheche ya moto wake haitanga'ra.
"Yes, the light of the wicked shall be put out, The spark of his fire shall not shine.
6 Nuru itakuwa giza katika hema yake; taa yake juu yake yeye itawekwa nje.
The light shall be dark in his tent. His lamp above him shall be put out.
7 Hatua za nguvu zake yeye zitafanywa kuwa fupi; mipango yake yeye mwenyewe itamwangusha yeye chini.
The steps of his strength shall be shortened. His own counsel shall cast him down.
8 Kwa maana yeye atatupwa katika mtego kwa miguu yake mwenyewe; yeye atatembea katika mahangaiko.
For he is cast into a net by his own feet, and he wanders into its mesh.
9 Tanzi litamchukua yeye kwa kisigino; mtego utabaki kushikilia juu yake.
A snare will take him by the heel. A trap will catch him.
10 Tanzi limefichwa kwa ajili yake chini ya ardhi; na mtego kwa ajili yake katika njia.
A noose is hidden for him in the ground, a trap for him in the way.
11 Watishao watamfanya yeye aogope juu ya sehemu zote; wao watamkimbiza yeye kwenye visigino vyake.
Terrors shall make him afraid on every side, and shall chase him at his heels.
12 Utajiri wake utageuka kuwa njaa, na majanga yatakuwa tayari upande wake.
His strength shall be famished. Calamity shall be ready at his side.
13 Sehemu za mwili wake zitakuwa zimemezwa; Hakika, mzaliwa wa kwanza wa kifo atazila sehemu zake yeye.
The members of his body shall be devoured. The firstborn of death shall devour his members.
14 Yeye ameraruliwa kutoka kwenye usalama wa hema yake na hakuweza kutembea kwenda kwa mfalme mwenye utisho.
He shall be rooted out of his tent where he trusts. He shall be brought to the king of terrors.
15 Watu ambao siyo wa kwake wataishi kwenye hema yake baada ya kuona ule moto mesambaa ndani ya nyumba yake yeye.
There shall dwell in his tent that which is none of his. Sulfur shall be scattered on his habitation.
16 Mizizi yake itanyauka chini yake; juu tawi lake yeye litakatwa.
His roots shall be dried up beneath. Above shall his branch be cut off.
17 Kumbukumbu lake yeye litapotea kutoka katika nchi; yeye hatakuwa na jina katika mtaa.
His memory shall perish from the earth. He shall have no name in the street.
18 Yeye atafukuzwa kutoka katika nuru mpaka kwenye giza na kuwa amefukuzwa nje na ulimwengu huu.
He shall be driven from light into darkness, and chased out of the world.
19 Hatakuwa na mtoto wa kiume wala mjukuu miongonni mwa watu wake, wala kizazi chochote kitakachobakia mahali alipokuwa amekaa.
He shall have neither son nor grandson among his people, nor any remaining where he sojourned.
20 Wale wanaoishi upande wa magharibi watakuwa wametiwa hofu kwa kile kitakachotokea kwake siku moja; wale wanaoishi upande wa mashariki watakuwa wameogopeshwa kwa hicho.
Those who come after shall be astonished at his day, as those who went before were frightened.
21 Hakika hizo ni nyumba za watu wasio haki, ni sehemu ya wale wasiomjua Mungu.”
Surely such are the dwellings of the unrighteous. This is the place of him who doesn't know God."

< Ayubu 18 >