< Ayubu 16 >

1 Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
And he answered Job and he said.
2 “Mimi nimevisikia vitu hivyo vingi; ninyi nyote ni wafariji wenye kuhuzunisha.
I have heard like these [things] many [are] comforters of trouble all of you.
3 Maneno yenye upuuzi daima yanaweza kuwa na mwisho? Nini kimeharibika kwenu kwamba mnajibu kama hivi?
¿ [does] an end [belong] to Words of wind or what? is it making sick you that you will answer.
4 Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi mnavyofanya, kama ninyi mngekuwa katika nafasi yangu; Mimi ningekusanya na kuunganisha maneno pamoja dhidi yenu na kutikisa kichwa changu kwenu ninyi katika dhihaka.
Also - I like you I will speak if there [were] self your in place of self my I will make join on you words and I will shake on you with head my.
5 Laiti, jinsi gani Mimi ningewatia moyo na midomo yangu! Jinsi gani faraja kutoka midomo yangu ingenga'risha huzuni yenu!
I will strengthen you with mouth my and [the] condolence of lips my it will restrain.
6 Ikiwa Mimi ninazungumza, kuomboleza kwangu hakujasikilizwa; Ikiwa nikiendelea katika kuzungumza, jinsi gani mimi ninaidiwa?
If I will speak not it will be restrained pain my and I will cease what? from me will it go.
7 Lakini sasa, Mungu,
Nevertheless now he has made weary me you have devastated all company my.
8 wewe umenifanya mimi kuchoka; wewe umeifanya familia yangu yote kuwa ukiwa. Wewe umenifanya mimi kukauka, ambayo yenyewe ni ushuhuda dhidi yangu mimi; kukonda kwa mwili wangu huinuka dhidi yangu, na kunashuhudia dhidi ya macho yangu.
And you have seized me a witness it has become and it has risen up on me leanness my in face my it testifies.
9 Mungu amenirarua mimi katika ghadhabu yake na amenitesa mimi; Yeye amenisaga mimi kwa meno yake; Adui yangu amenikazia macho yake juu yangu kama yeye anavyonirarua mimi vipande.
Anger his it has torn [me] - and it has assailed me he has gnashed towards me with teeth his opponent my - he sharpens eyes his to me.
10 Watu wameachama na midomo iliyowazi juu yangu; wamenipiga mimi katika shavu kwa kunitukana; wamekusanyika pamoja kinyume changu mimi.
People have opened wide on me - mouth their in scorn they have struck cheeks my together on me they mass themselves!
11 Mungu amenikabidhi mimi juu ya watu wasio mcha Mungu, na kunitupa mimi ndani ya mikono ya watu waovu.
He delivers up me God to an unjust one and on [the] hands of wicked [people] he casts me.
12 Mimi nilikuwa katika wepesi, na yeye amenivunjavunja mimi vipande. Hakika, amenichukua mimi kwa shingo na ameniponda mimi vipande vipande; yeye pia ameniweka mimi juu kama shabaha yake.
At ease I was - and he smashed me and he took hold on neck my and he shattered me and he set up me of him to a target.
13 Wapiga upinde wake wote wamenizunguka mimi; Mungu huzikata vipande vipande figo zangu, na haniokoi mimi; yeye humwaga nje nyongo yangu juu ya ardhi.
They surround me - archers his he splits open kidneys my and not he has compassion he pours out to the ground gall my.
14 yeye hukanyaga kanyaga kupitia ukuta wangu tena na tena; yeye hukimbia juu yangu mimi kama shujaa.
He breaks through me a breach on [the] face of a breach he runs on me like a warrior.
15 nguo ya magunia juu ya ngozi yangu; Mimi nimeisukuma kwa nguvu pembe yangu ndani ya ardhi.
Sackcloth I have sewed over skin my and I have inserted in the dust horn my.
16 Uso wangu ni mwekundu na kuomboleza; juu ya ngozi inayofunika macho kuna kivuli cha mauti
Face my (they are reddened *QK) from weeping and [is] on eyelids my deep darkness.
17 ingawa hakuna dhuluma katika mikono yangu, na kuomba kwangu ni safi.
On not violence [is] in hands my and prayer my [is] pure.
18 Nchi, haifuniki juu damu yangu mimi; acha kulia kwangu kuwe hakuna mahali pa kupumzika.
O earth may not you cover blood my and may not it belong a place to outcry my.
19 Hata sasa, tazama, ushuhuda wangu uko mbinguni; yeye ambaye ashuhudiaye kwa ajili yangu mimi yuko juu.
Also now there! [is] in the heavens witness my and witness my [is] in high places.
20 Rafiki zangu wananicheka kwa dharau, lakini jicho langu linamwaga machozi kwa Mungu.
[are] scoffing at Me companions my to God it has wept eye my.
21 Mimi ninaomba ule ushuhuda ulioko mbinguni kumtetea mtu huyu na Mungu kama mwanadamu afanyavyo na jirani yake.
And he may argue for a man with God and a child of humankind for companion his.
22 Kwa maana wakati miaka michache itakapokuwa imepita, Mimi nitakwenda mahali ambapo mimi sitaweza kurudi.
For years of number they will come and a way [which] not I will return I will go.

< Ayubu 16 >