< Ayubu 14 >

1 Mwanadamu, ambaye amezaliwa na mwanamke, huishi siku chache tu na amejaa mahangaiko.
For a mortal born of a woman [is] short lived, and full of wrath.
2 Yeye huchanua kutoka katika ardhi kama ua na kukatwa chini; yeye hukimbia kama kivuli na hawezi kudumu.
Or he falls like a flower that has bloomed; and he departs like a shadow, and can’t continue.
3 Je, wewe unatazama chochote katika hivi? Mnanileta mimi hukumuni pamoja nanyi?
Hast you not taken account even of him, and caused him to enter into judgment before you?
4 Ni nani anayeweza kukileta kitu safi kutoka katika kitu kichafu? Hakuna awaye yote.
For who shall be pure from uncleanness? not even one;
5 Siku za mwanadamu zimeamriwa. Idadi ya miezi yake unayo wewe; umekiweka kikomo chake ambacho hawezi kukivuka.
if even his life should be [but] one day upon the earth: and his months are numbered by him: you have appointed [him] for a time, and he shall by no means exceed [it].
6 Tazama mbali kutoka kwake kwamba yeye aweze kupumzika, ili kwamba aweze kufurahia siku yake kama mtu aliyekodishwa kama yeye anaweza kufanya hivyo.
Depart from him, that he may be quiet, and take pleasure in his life, [though] as a hireling.
7 Kunaweza kuwa na tumaini kwa mti; kama ukikatwa chini, unaweza kuchipua tena, hivyo chipukizi lake halitapotea.
For there is hope for a tree, even if it should be cut down, [that] it shall blossom again, and its branch shall not fail.
8 Japokuwa mizizi yake inakua na kuzeeka katika ardhi, na shina lake kufa katika udongo,
For though its root should grow old in the earth, and its stem die in the rock;
9 hata kama bado lina harufu ya maji pekee, litachipua tena na kutoa nje matawi kama mche.
it will blossom from the scent of water, and will produce a crop, as one newly planted.
10 Lakini mwanadamu hufa; yeye huwa dhaifu; haswaa, mwanadamu hukoma kupumua, na tena yuko wapi yeye?
But a man that has died is utterly gone; and when a mortal has fallen, he is no more.
11 Kama maji yanavyopotea kutoka ziwani, na kama vile mto upotezavyo maji na kukauka,
For the sea wastes in [length of] time, and a river fails and is dried up.
12 vivyo hivyo watu hulala chini na hawaamki tena. Mpaka pale mbingu zitakapokuwa hazipo tena, hawataamka wala kuamshwa kutoka katika kulala kwao.
And man that has lain down [in death] shall certainly not rise again till the heaven be dissolved, and they shall not awake from their sleep.
13 Laiti, kwamba ungenificha mimi mbali katika kuzimu mbali kutoka katika mahangaiko, na kwamba ungenitunza mimi katika siri hadi hasira yake imalizike, kwamba ungeniwekea mimi muda maalumu wa kukaa huko na kisha kuniita mimi katika fahamu! (Sheol h7585)
For oh that you had kept me in the grave, and had hidden me until your wrath should cease, and you should set me a time in which you would remember me! (Sheol h7585)
14 Ikiwa mwanadamu akifa, yeye ataishi tena? Ikiwa hivyo, ningependa kusubiri kule muda wangu wote wa kuharibika mpaka kufunguliwa kwangu kutakapokuja.
For if a man should die, shall he live [again], having accomplished the days of his life? I will wait till I exist again?
15 Wewe ungeita, na mimi ningekujibu wewe. Wewe ungekuwa na shauku ya kazi ya mikono yako.
Then shall you call, and I will listen to you: but do not you reject the work of your hands.
16 Wewe ungehesabu na kutunza nyayo zangu; Wewe usingejali kumbukumbu ya dhambi yangu.
But you have numbered my devices: and not one of my sins shall escape you?
17 Uovu wangu ungetiwa muhuri katika mkoba; wewe ungeufunga uovu wangu.
An you have sealed up my transgressions in a bag, and marked if I have been guilty of any transgression unawares.
18 Lakini hata milima huanguka na kuwa si chochote; hata miamba huhamishwa kutoka mahali pake;
And verily a mountain falling will utterly be destroyed, and a rock shall be worn out of its place.
19 maji yaliyokuwa chini ya mawe; kufurika kwake huondoa mbali mavumbi ya nchi. Kama hivi, ninyi mnavyoharibu matumaini ya mwanadamu.
The waters wear the stones, and waters falling headlong [overflow] a heap of the earth: and you destroy the hope of man.
20 Ninyi daima humshinda yeye, na yeye hupita mbali; Ninyi mnabadilisha uso wake na kumtuma yeye mbali kufa.
You drive him to an end, and he is gone: you set your face against him, and send him away;
21 Kama watoto wake wa kiume ni wa kuheshimiwa, yeye, hatambui hicho; na kama wakishushwa chini, yeye haoni hicho.
and though his children be multiplied, he knows [it] not; and if they be few, he is not aware.
22 Yeye hujisikia tu maumivu ya mwili wake mwenyewe, na hujiombolezea yeye mwenyewe.
But his flesh is in pain, and his soul mourns.

< Ayubu 14 >