< Ayubu 13 >

1 Tazama, jicho langu limeyaona haya yote; sikio langu limeyasikia na kuyaelewa hayo.
See, my eye has seen all this; my ear has heard and understood it.
2 Kile mnachokifahamu, ndicho hicho mimi pia ninachokifahamu; Mimi siyo duni kwenu ninyi.
What you know, the same I also know; I am not inferior to you.
3 Hata hivyo, Mimi ningeweza kuzungumza na mwenye nguvu; Mimi natamani kusemezana na Mungu.
However, I would rather speak with the Almighty; I wish to reason with God.
4 Lakini ninyi mnauficha ukweli kwa uongo; ninyi nyote ni tabibu msiokuwa na thamani.
But you whitewash the truth with lies; you are all physicians of no value.
5 Laiti, kwamba kwa pamoja mngeshikilia amani yenu! Hilo lingekuwa hekima yenu ninyi.
Oh, that you would altogether hold your peace! That would be your wisdom.
6 Sikia sasa kuhoji kwangu; Sikiliza kusihi kwa midomo yangu mwenyewe.
Hear now my own reasoning; listen to the pleading of my own lips.
7 Ninyi mtazungumza visivyo haki kwa ajili ya Mungu, na ninyi mtazungumza udanganyifu kwa yeye? Ni kweli ninyi mngeonyesha ukarimu kwa yeye?
Will you speak unrighteously for God, and will you talk deceitfully for him?
8 Ni kweli ninyi mngetetea katika mahakama kama mawakili wa Mungu?
Will you show him partiality? Will you argue the case for God?
9 Je, kweli ingekuwa vizuri kwenu wakati yeye akiwatafuta ninyi? Mngeweza ninyi kumdanganya yeye kama mlivyoweza kuwadanganya watu?
Will it be good for you when he searches you out? Could you deceive him as you might deceive men?
10 Yeye kwa hakika angewathibitisha upya ninyi ikiwa katika siri ninyi mmeonyesha kutokukamilika.
He would surely reprove you if in secret you showed partiality.
11 Je, ukuu wake usingewafanya ninyi muogope? Je, utisho wake usingeshuka juu yenu?
Will not his majesty terrify you, and the dread of him fall upon you?
12 Hadithi zenu za misemo ya kukariri, ni mithali zimetengenezwa kwa majivu; utetezi wenu ni utetezi uliotengenezwa kwa udongo wa mfinyanzi.
Your memorable sayings are proverbs made of ashes; your defenses are defenses made of clay.
13 Shikilieni amani yenu, mniache peke yangu, ili ya kwamba nipate kusema, acheni yaje yale yanayoweza kuja kwangu.
Hold your peace, let me alone, so that I may speak, let come what may on me.
14 Nitaichukua nyama yangu mwenywewe katika meno yangu; Nitayachukua maisha yangu katika mikono yangu.
I will take my own flesh in my teeth; I will take my life in my hands.
15 Tazama, ikiwa ataniua mimi, sitakuwa na tumaini lililobakia; hata hivyo, nitazitetea njia zangu mbele zake yeye.
See, if he kills me, I will have no hope left; nevertheless, I will defend my ways before him.
16 Hiki kitakuwa sababu ya kutohesabiwa hatia, kwamba mimi sikuja mbele zake kama mtu asiyemcha Mungu.
This will be the reason for my deliverance, for no godless person would come before him.
17 Mungu, sikiliza kwa makini kuzungumza kwangu; ruhusu kutangaza kwangu kuje kwenye masikio yako.
God, listen carefully to my speech; let my declaration come to your ears.
18 Tazama sasa, Nimeuweka utetezi wangu katika mpangilio, Mimi ninafahamu kwamba mimi sina hatia.
See now, I have set my defense in order; I know that I am innocent.
19 Ni nani anayeweza kushindana na mimi katika mahakama? Ikiwa mlikuja kufanya hivyo, na kama mimi nilithibitishwa kukosea, ndipo ningekuwa kimya na kuyatoa maisha yangu.
Who is the one who would argue against me in court? If you came to do so, and if I were proved wrong, then I would be silent and give up my life.
20 Mungu, fanya mambo mawili kwa ajili yangu, na tena Mimi sitajificha kutoka katika uso wako.
God, do only two things for me, and then I will not hide myself from your face:
21 Ondoa kutoka kwangu mkono wako unaotesa, na usiache utisho wako unifanye mimi kuogopa.
withdraw your oppressive hand from me, and do not let your terrors make me afraid.
22 Ndipo niite mimi, na mimi nitakujibu; au uniache mimi niseme na wewe na wewe unijibu mimi.
Then call me, and I will answer; or let me speak to you, and you answer me.
23 Je, maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi? Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.
How many are my iniquities and sins? Let me know my transgression and my sin.
24 Kwa nini unaficha uso wako kutoka kwangu mimi na kunitendea mimi kama adui yako?
Why do you hide your face from me and treat me like your enemy?
25 Je, wewe utalitesa jani linalopeperushwa? Je, utaendelea kulifuatilia bua kavu?
Will you persecute a driven leaf? Will you pursue dry stubble?
26 Kwa maana wew unaandika chini vitu vichungu dhidi yangu mimi; wewe unanifanya mimi kurithi uovu wa ujana wangu.
For you write down bitter things against me; you make me inherit the iniquities of my youth.
27 Wewe pia unaiweka miguu yangu katika nguo nyembamba; wewe waangalia njia zangu zote; wewe wachunguza chini mahali ambapo nyayo za miguu yangu zimekanyaga.
You also put my feet in the stocks; you closely watch all my paths; you examine the ground where the soles of my feet have walked
28 japokuwa mimi ni kama kitu kilichooza ambacho hutupwa mbali, kama vazi lile ambalo nondo wamelila.
although I am like a rotten thing that wastes away, like a garment that moths have eaten.

< Ayubu 13 >