< Ayubu 12 >

1 Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
Job respondió:
2 “Hakuna shaka ninyi wanadamu; Hekima mtakufa nayo.
Entonces ciertamente ustedes son el pueblo, y con ustedes se acaba la sabiduría.
3 Lakini nina ufahamu kama vile ninyi; Mimi siyo duni kwenu. Ni dhhiri, ni nani asiyefahamu vitu hivyo kama hivi?
Pero yo tengo entendimiento como ustedes. No soy menos que ustedes. ¿Quién no sabe tales cosas?
4 Mimi ni kitu cha kuchekwa na jirani-Mimi, ni mmoja aliyemwita Mungu na ambaye alijibiwa na yeye! Mimi, ni mwenye haki na mtu asiyekuwa na hatia-Mimi sasa nimekuwa kitu cha kuchekwa.
Yo soy alguien que para su amigo es motivo de risa, uno que clamó a ʼElohim y le respondió. ¡El justo e intachable es un payaso!
5 Katika mawazo yake mtu fulani aliye katika kufurahi, kuna kudharau kwa mashaka; hufikiri katika njia ambayo huleta mambo mabaya zaidi kwa wale ambao miguu yao inateleza.
El que tiene bienestar desprecia la calamidad como algo preparado para aquellos que resbalan.
6 Hema za wezi hufanikiwa, na wale ambao humkasirisha Mungu huhisi salama; mikono yao wenyewe ni miungu wao.
Prosperan las tiendas de los ladrones y los que provocan a ʼEL están seguros, aquellos que ʼEloah trae a su poder.
7 Lakini sasa waulize hao wanyama wa mwituni, na watakufundisha wewe; waulize ndege wa angani, na watakuambia wewe.
En efecto, pregunta ahora a las bestias, y ellas te enseñarán, a las aves del cielo, y ellas te lo dirán.
8 Au iambie ardhi, na itakufundisha wewe; samaki wa baharini watakutangazia wewe.
O habla a la tierra, y te enseñará. Los peces del mar también te lo declararán.
9 Ni myama yupi miongoni mwa hawa asiyefahamu kuwa mkono wa Yahwe umetenda haya?
¿Cuál de ellos no sabe que la mano de Yavé hizo esto,
10 Katika mkono wake mna uzima wa kila kiumbe hai na pumzi ya wanadamu wote.
que en su mano está la vida de todo viviente y el hálito de toda la humanidad?
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile kaakaa lionjavyo chakula chake?
¿No distingue el oído las palabras y el paladar prueba la comida?
12 Kwa wazee mna hekima; katika wingi wa siku mna ufahamu.
En los ancianos está la sabiduría y en la larga edad el entendimiento.
13 Pamoja na Mungu mna hekima na ukuu; yeye anayo mashauri na ufahamu.
Con Él están la sabiduría y el poder. Suyos son el consejo y el entendimiento.
14 Tazama, yeye huangusha chini, na haiwezekani kujengwa tena; kama yeye akimtia gerezani mtu yeyote, hakutakuwa tena kufunguliwa.
Si Él derriba, no será reedificado. Si Él encierra al hombre, no hay liberación.
15 Tazama, kama yeye akiyazuia maji, yanakauka; na kama akiyaachilia nje yanaitaabisha ardhi.
Si Él retiene las aguas, se secan, y si las suelta, inundan la tierra.
16 Pamoja na yeye mna nguvu na hekima; watu ambao wamedanganywa na mdanganyi wote pamoja wako katika nguvu zake.
Con Él están la fortaleza y la sana sabiduría. Suyos son el que yerra y el que hace errar.
17 Yeye huwaongoza washauri mbali bila kuvaa viatu katika huzuni; huwarudisha hakimu katika upumbavu.
Hace andar descalzos a los consejeros y entontece a los jueces.
18 Yeye Huondoa minyororo ya mamlaka kutoka kwa wafalme; yeye hufunika viuno vyao kwa nguo.
Suelta las ataduras que imponen los reyes y ata con una cuerda sus cinturas.
19 Yeye huwaongoza makuhani mbali bila kuvaa viatu na kuwapindua watu wakuu.
Hace ir descalzos a los sacerdotes y derriba a los poderosos.
20 Yeye huondoa hotuba ya wale waliokuwa wameaminiwa na huondoa mbali ufahamu wa wazee.
Priva del habla a los de confianza, y del discernimiento a los ancianos.
21 Yeye humwaga aibu juu ya binti za wafalme na hufungua mishipi ya watu wenye nguvu.
Derrama desprecio sobre los nobles y afloja el cinturón de los fuertes.
22 Yeye huweka wazi vitu vya kina kutoka katika giza na kuvileta nje kumuika vivuli mahali ambapa watu waliokufa wapo.
Descubre las profundidades de la oscuridad y saca a la luz la sombra de muerte.
23 Yeye huyafanya mataifa kuwa na nguvu, na pia huyaharibu; Yeye pia huyakuza mataifa, na pia yeye huyaongoza mbali kama wafungwa.
Engrandece las naciones y las destruye. Ensancha los pueblos y los suprime.
24 Yeye huondoa mbali ufahamu kutoka kwa viongozi wa watu wa nchi; huwafanya wao kutangatanga msituni mahali pasipo na njia.
Priva de discreción a los caudillos de los pueblos de la tierra y los hace deambular por un desierto sin camino.
25 Wao wanapapasa katika giza bila kuwa na mwanga; yeye huwafanya wao kuweweseka kama mtu mlevi.
No tienen luz. Palpan en la oscuridad, y los hace tambalearse como ebrios.

< Ayubu 12 >