< Ayubu 12 >

1 Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
Respondió Job y dijo:
2 “Hakuna shaka ninyi wanadamu; Hekima mtakufa nayo.
“De veras, vosotros sois hombres, y con vosotros morirá la sabiduría.
3 Lakini nina ufahamu kama vile ninyi; Mimi siyo duni kwenu. Ni dhhiri, ni nani asiyefahamu vitu hivyo kama hivi?
También yo tengo seso como vosotros; ninguna ventaja tenéis sobre mí; ¿y quién no sabe lo que decís?
4 Mimi ni kitu cha kuchekwa na jirani-Mimi, ni mmoja aliyemwita Mungu na ambaye alijibiwa na yeye! Mimi, ni mwenye haki na mtu asiyekuwa na hatia-Mimi sasa nimekuwa kitu cha kuchekwa.
¡Ludibrio soy de mis amigos! ¡Yo, que clamaba a Dios, y Él le respondía! ¡Yo, el recto e inocente, ahora objeto de oprobio!
5 Katika mawazo yake mtu fulani aliye katika kufurahi, kuna kudharau kwa mashaka; hufikiri katika njia ambayo huleta mambo mabaya zaidi kwa wale ambao miguu yao inateleza.
¡Ignominia al que sufre! —así piensa el que vive sin cuidados—. ¡Caiga desprecio sobre aquel cuyo pie resbala!
6 Hema za wezi hufanikiwa, na wale ambao humkasirisha Mungu huhisi salama; mikono yao wenyewe ni miungu wao.
Las guaridas de los salteadores gozan de paz, seguros están los que irritan a Dios; a ellos Dios se lo otorga (todo).
7 Lakini sasa waulize hao wanyama wa mwituni, na watakufundisha wewe; waulize ndege wa angani, na watakuambia wewe.
Pregunta, te ruego, a las bestias, y ellas te enseñarán, a las aves del cielo, y te lo dirán;
8 Au iambie ardhi, na itakufundisha wewe; samaki wa baharini watakutangazia wewe.
o habla con la tierra, y ella te instruirá; te lo contarán los peces del mar.
9 Ni myama yupi miongoni mwa hawa asiyefahamu kuwa mkono wa Yahwe umetenda haya?
¿Quién de todos estos seres no sabe que la mano de Yahvé ha hecho (todas) las cosas?
10 Katika mkono wake mna uzima wa kila kiumbe hai na pumzi ya wanadamu wote.
En su mano está el alma de todo viviente, y el soplo de toda carne humana.
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile kaakaa lionjavyo chakula chake?
¿No se ha hecho el oído para discernir las palabras; el paladar para gustar los manjares?
12 Kwa wazee mna hekima; katika wingi wa siku mna ufahamu.
En los ancianos reside la sabiduría, y en la larga vida la prudencia;
13 Pamoja na Mungu mna hekima na ukuu; yeye anayo mashauri na ufahamu.
con Él, empero, están la sabiduría y el poder, suyo es el consejo y suya la inteligencia.
14 Tazama, yeye huangusha chini, na haiwezekani kujengwa tena; kama yeye akimtia gerezani mtu yeyote, hakutakuwa tena kufunguliwa.
Lo que Él derriba, no será reedificado; si Él encierra al hombre, no hay quien lo libre.
15 Tazama, kama yeye akiyazuia maji, yanakauka; na kama akiyaachilia nje yanaitaabisha ardhi.
Si detiene las aguas, estas se secan; si las suelta, devastan la tierra.
16 Pamoja na yeye mna nguvu na hekima; watu ambao wamedanganywa na mdanganyi wote pamoja wako katika nguvu zake.
En Él están el poder y el saber, suyos son el engañado y el que engaña.
17 Yeye huwaongoza washauri mbali bila kuvaa viatu katika huzuni; huwarudisha hakimu katika upumbavu.
Él hace andar a los consejeros privados (de consejo), y entontece a los jueces.
18 Yeye Huondoa minyororo ya mamlaka kutoka kwa wafalme; yeye hufunika viuno vyao kwa nguo.
Él quita a los reyes la faja, y les ciñe los lomos, con una soga.
19 Yeye huwaongoza makuhani mbali bila kuvaa viatu na kuwapindua watu wakuu.
Hace andar a los sacerdotes descalzos, y a los grandes derriba.
20 Yeye huondoa hotuba ya wale waliokuwa wameaminiwa na huondoa mbali ufahamu wa wazee.
Quita el habla a los más respetados, y a los ancianos los priva del juicio.
21 Yeye humwaga aibu juu ya binti za wafalme na hufungua mishipi ya watu wenye nguvu.
Vacía desprecio sobre los príncipes, y afloja el cinto de los fuertes.
22 Yeye huweka wazi vitu vya kina kutoka katika giza na kuvileta nje kumuika vivuli mahali ambapa watu waliokufa wapo.
Descubre lo oculto en las tinieblas, y saca a luz la sombra de la muerte.
23 Yeye huyafanya mataifa kuwa na nguvu, na pia huyaharibu; Yeye pia huyakuza mataifa, na pia yeye huyaongoza mbali kama wafungwa.
Da prosperidad a los pueblos y los destruye, dilata a las naciones, y las reduce.
24 Yeye huondoa mbali ufahamu kutoka kwa viongozi wa watu wa nchi; huwafanya wao kutangatanga msituni mahali pasipo na njia.
Quita la inteligencia a los príncipes de los pueblos de la tierra, y los hace vagar por un desierto sin camino;
25 Wao wanapapasa katika giza bila kuwa na mwanga; yeye huwafanya wao kuweweseka kama mtu mlevi.
andan a tientas en tinieblas, sin tener luz; Él los hace errar como a embriagados.”

< Ayubu 12 >