< Ayubu 12 >

1 Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
Respondens autem Job, dixit:
2 “Hakuna shaka ninyi wanadamu; Hekima mtakufa nayo.
[Ergo vos estis soli homines, et vobiscum morietur sapientia?
3 Lakini nina ufahamu kama vile ninyi; Mimi siyo duni kwenu. Ni dhhiri, ni nani asiyefahamu vitu hivyo kama hivi?
Et mihi est cor sicut et vobis, nec inferior vestri sum; quis enim hæc quæ nostis ignorat?
4 Mimi ni kitu cha kuchekwa na jirani-Mimi, ni mmoja aliyemwita Mungu na ambaye alijibiwa na yeye! Mimi, ni mwenye haki na mtu asiyekuwa na hatia-Mimi sasa nimekuwa kitu cha kuchekwa.
Qui deridetur ab amico suo, sicut ego, invocabit Deum, et exaudiet eum: deridetur enim justi simplicitas.
5 Katika mawazo yake mtu fulani aliye katika kufurahi, kuna kudharau kwa mashaka; hufikiri katika njia ambayo huleta mambo mabaya zaidi kwa wale ambao miguu yao inateleza.
Lampas contempta apud cogitationes divitum parata ad tempus statutum.
6 Hema za wezi hufanikiwa, na wale ambao humkasirisha Mungu huhisi salama; mikono yao wenyewe ni miungu wao.
Abundant tabernacula prædonum, et audacter provocant Deum, cum ipse dederit omnia in manus eorum.
7 Lakini sasa waulize hao wanyama wa mwituni, na watakufundisha wewe; waulize ndege wa angani, na watakuambia wewe.
Nimirum interroga jumenta, et docebunt te; et volatilia cæli, et indicabunt tibi.
8 Au iambie ardhi, na itakufundisha wewe; samaki wa baharini watakutangazia wewe.
Loquere terræ, et respondebit tibi, et narrabunt pisces maris.
9 Ni myama yupi miongoni mwa hawa asiyefahamu kuwa mkono wa Yahwe umetenda haya?
Quis ignorat quod omnia hæc manus Domini fecerit?
10 Katika mkono wake mna uzima wa kila kiumbe hai na pumzi ya wanadamu wote.
In cujus manu anima omnis viventis, et spiritus universæ carnis hominis.
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile kaakaa lionjavyo chakula chake?
Nonne auris verba dijudicat? et fauces comedentis, saporem?
12 Kwa wazee mna hekima; katika wingi wa siku mna ufahamu.
In antiquis est sapientia, et in multo tempore prudentia.
13 Pamoja na Mungu mna hekima na ukuu; yeye anayo mashauri na ufahamu.
Apud ipsum est sapientia et fortitudo; ipse habet consilium et intelligentiam.
14 Tazama, yeye huangusha chini, na haiwezekani kujengwa tena; kama yeye akimtia gerezani mtu yeyote, hakutakuwa tena kufunguliwa.
Si destruxerit, nemo est qui ædificet; si incluserit hominem, nullus est qui aperiat.
15 Tazama, kama yeye akiyazuia maji, yanakauka; na kama akiyaachilia nje yanaitaabisha ardhi.
Si continuerit aquas, omnia siccabuntur; et si emiserit eas, subvertent terram.
16 Pamoja na yeye mna nguvu na hekima; watu ambao wamedanganywa na mdanganyi wote pamoja wako katika nguvu zake.
Apud ipsum est fortitudo et sapientia; ipse novit et decipientem, et eum qui decipitur.
17 Yeye huwaongoza washauri mbali bila kuvaa viatu katika huzuni; huwarudisha hakimu katika upumbavu.
Adducit consiliarios in stultum finem, et judices in stuporem.
18 Yeye Huondoa minyororo ya mamlaka kutoka kwa wafalme; yeye hufunika viuno vyao kwa nguo.
Balteum regum dissolvit, et præcingit fune renes eorum.
19 Yeye huwaongoza makuhani mbali bila kuvaa viatu na kuwapindua watu wakuu.
Ducit sacerdotes inglorios, et optimates supplantat:
20 Yeye huondoa hotuba ya wale waliokuwa wameaminiwa na huondoa mbali ufahamu wa wazee.
commutans labium veracium, et doctrinam senum auferens.
21 Yeye humwaga aibu juu ya binti za wafalme na hufungua mishipi ya watu wenye nguvu.
Effundit despectionem super principes, eos qui oppressi fuerant relevans.
22 Yeye huweka wazi vitu vya kina kutoka katika giza na kuvileta nje kumuika vivuli mahali ambapa watu waliokufa wapo.
Qui revelat profunda de tenebris, et producit in lucem umbram mortis.
23 Yeye huyafanya mataifa kuwa na nguvu, na pia huyaharibu; Yeye pia huyakuza mataifa, na pia yeye huyaongoza mbali kama wafungwa.
Qui multiplicat gentes, et perdit eas, et subversas in integrum restituit.
24 Yeye huondoa mbali ufahamu kutoka kwa viongozi wa watu wa nchi; huwafanya wao kutangatanga msituni mahali pasipo na njia.
Qui immutat cor principum populi terræ, et decipit eos ut frustra incedant per invium:
25 Wao wanapapasa katika giza bila kuwa na mwanga; yeye huwafanya wao kuweweseka kama mtu mlevi.
palpabunt quasi in tenebris, et non in luce, et errare eos faciet quasi ebrios.]

< Ayubu 12 >