< Ayubu 12 >

1 Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
And Job answered and said,
2 “Hakuna shaka ninyi wanadamu; Hekima mtakufa nayo.
So then you [alone] are men, and wisdom shall die with you?
3 Lakini nina ufahamu kama vile ninyi; Mimi siyo duni kwenu. Ni dhhiri, ni nani asiyefahamu vitu hivyo kama hivi?
[But] I also have a heart as well as you.
4 Mimi ni kitu cha kuchekwa na jirani-Mimi, ni mmoja aliyemwita Mungu na ambaye alijibiwa na yeye! Mimi, ni mwenye haki na mtu asiyekuwa na hatia-Mimi sasa nimekuwa kitu cha kuchekwa.
For a righteous and blameless man has become a subject for mockery.
5 Katika mawazo yake mtu fulani aliye katika kufurahi, kuna kudharau kwa mashaka; hufikiri katika njia ambayo huleta mambo mabaya zaidi kwa wale ambao miguu yao inateleza.
For it had been ordained that he should fall under others at the appointed time, and that his houses should be spoiled by transgressors: let not however any one trust that, being evil, he shall be [held] guiltless,
6 Hema za wezi hufanikiwa, na wale ambao humkasirisha Mungu huhisi salama; mikono yao wenyewe ni miungu wao.
even as many as provoke the Lord, as if there were indeed to be no inquisition [made] of them.
7 Lakini sasa waulize hao wanyama wa mwituni, na watakufundisha wewe; waulize ndege wa angani, na watakuambia wewe.
But ask now the beasts, if they may speak to you; and the birds of the air, if they may declare to you.
8 Au iambie ardhi, na itakufundisha wewe; samaki wa baharini watakutangazia wewe.
Tell the earth, if it may speak to you: and the fishes of the sea shall explain to you.
9 Ni myama yupi miongoni mwa hawa asiyefahamu kuwa mkono wa Yahwe umetenda haya?
Who then has not known in all these things, that the hand of the Lord has made them?
10 Katika mkono wake mna uzima wa kila kiumbe hai na pumzi ya wanadamu wote.
Whereas the life of all living things is in his hand, and the breath of every man.
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile kaakaa lionjavyo chakula chake?
For the ear tries words, and the palate tastes meats.
12 Kwa wazee mna hekima; katika wingi wa siku mna ufahamu.
In length of time is wisdom, and in long life knowledge.
13 Pamoja na Mungu mna hekima na ukuu; yeye anayo mashauri na ufahamu.
With him are wisdom and power, with him counsel and understanding.
14 Tazama, yeye huangusha chini, na haiwezekani kujengwa tena; kama yeye akimtia gerezani mtu yeyote, hakutakuwa tena kufunguliwa.
If he should cast down, who will build up? if he should shut up against man, who shall open?
15 Tazama, kama yeye akiyazuia maji, yanakauka; na kama akiyaachilia nje yanaitaabisha ardhi.
If he should withhold the water, he will dry the earth: and if he should let it loose, he overthrows and destroys it.
16 Pamoja na yeye mna nguvu na hekima; watu ambao wamedanganywa na mdanganyi wote pamoja wako katika nguvu zake.
With him are strength and power: he has knowledge and understanding.
17 Yeye huwaongoza washauri mbali bila kuvaa viatu katika huzuni; huwarudisha hakimu katika upumbavu.
He leads counselors away captive, and maddens the judges of the earth.
18 Yeye Huondoa minyororo ya mamlaka kutoka kwa wafalme; yeye hufunika viuno vyao kwa nguo.
He seats kings upon thrones, and girds their loins with a girdle.
19 Yeye huwaongoza makuhani mbali bila kuvaa viatu na kuwapindua watu wakuu.
He sends away priests into captivity, and overthrows the mighty ones of the earth.
20 Yeye huondoa hotuba ya wale waliokuwa wameaminiwa na huondoa mbali ufahamu wa wazee.
He changes the lips of the trusty, and he knows the understanding of the elders.
21 Yeye humwaga aibu juu ya binti za wafalme na hufungua mishipi ya watu wenye nguvu.
He pours dishonor upon princes, and heals the lowly.
22 Yeye huweka wazi vitu vya kina kutoka katika giza na kuvileta nje kumuika vivuli mahali ambapa watu waliokufa wapo.
Revealing deep things out of darkness: and he has brought into light the shadow of death.
23 Yeye huyafanya mataifa kuwa na nguvu, na pia huyaharibu; Yeye pia huyakuza mataifa, na pia yeye huyaongoza mbali kama wafungwa.
Causing the nations to wander, and destroying them: overthrowing the nations, and leading them [away].
24 Yeye huondoa mbali ufahamu kutoka kwa viongozi wa watu wa nchi; huwafanya wao kutangatanga msituni mahali pasipo na njia.
Perplexing the minds of the princes of the earth: and he causes them to wander in a way, they have not known, [saying],
25 Wao wanapapasa katika giza bila kuwa na mwanga; yeye huwafanya wao kuweweseka kama mtu mlevi.
Let them grope [in] darkness, and [let there be] no light, and let them wander as a drunken man.

< Ayubu 12 >