< Ayubu 11 >

1 Ndipo Sofari Mnaamathi alijibu na kusema,
Entonces Sofar naamatita respondió:
2 “Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa? Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?
¿No habrá respuesta a la abundancia de palabras? ¿Será justificado el que habla mucho?
3 Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?
¿Harán callar a los hombres tus jactancias? ¿Harás escarnio sin que alguno te avergüence?
4 Kwa kuwa wewe unasema kwa Mungu, 'Imani yangu ni safi, Mimi sina waa lolote machoni pako.'
Pues dijiste: Mi enseñanza es pura, y soy inocente delante de Ti.
5 Lakini, laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;
Pero, quién diera que ʼElohim hable y abra su boca hacia ti.
6 hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima! Kwa kuwa yeye ni mkuu katika ufahamu. Tena tambua huyo Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.
Te declare secretos de sabiduría, porque Él es de múltiple entendimiento. Así entenderías que ʼElohim, en tu favor, te castiga menos de lo que merece tu iniquidad.
7 Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?
¿Descubrirás tú las profundidades de ʼElohim? ¿Puedes hallar los límites de ʼEL-Shadday?
8 Upeo uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu; waweza kufahamu nini wewe? (Sheol h7585)
Es más alto que los cielos, ¿qué puedes tú hacer? Es más profundo que el Seol, ¿qué puedes tú saber? (Sheol h7585)
9 Vipimo vyake ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.
Su dimensión es más extensa que la tierra y más ancha que el mar.
10 kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye?
Si Él pasa y aprisiona, o convoca una asamblea, ¿quién lo puede restringir?
11 Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka?
Porque Él conoce a los hombres vanos. Ve también su perversidad, ¿y no la considerará?
12 Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.
El hombre vano será entendido cuando un pollino de asno montés nazca hombre.
13 Lakini ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;
Si tú dispones tu corazón y extiendes a Él tus manos,
14 ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako, lakini hivyo tena unauweka mbali nawe, na haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.
si hay iniquidad en tus manos, la alejas de ti y no permites que la perversidad more en tus tiendas,
15 Ndipo kwa hakika ungeinua juu uso wako bila ishara ya aibu; Ni dhahiri, ungethibitika na usingeogopa.
entonces levantarías tu semblante libre de mancha, estarías firme y nada temerías,
16 Wewe ungesahau mateso yako; ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.
olvidarías tu aflicción y la recordarías como aguas que pasaron.
17 Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri; japokuwa kulikuwa na giza, litakuwa kama asubuhi.
Tu existencia sería más resplandeciente que el mediodía. Aunque haya oscuridad, sería como la alborada.
18 Ungekuwa salama kwa sababu kuna tumaini; ni dhahiri, wewe utapata usalama juu yako na utachukua pumziko lako katika usalama.
Estarías confiado, porque habría esperanza. Mirarías alrededor y descansarías seguro,
19 Pia ungelala chini katika pumziko, na hakuna ambaye angekufanya wewe uogope; hakika wengi wangetafuta upendeleo wako.
reposarías, sin que alguno te espante. Y muchos implorarían tu favor.
20 Lakini macho ya watu waovu yatashindwa; hawatakuwa na njia ya kukimbia; tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.
Pero los ojos de los perversos fallarán, y no habrá escape para ellos. Su esperanza será el último suspiro.

< Ayubu 11 >