< Ayubu 11 >

1 Ndipo Sofari Mnaamathi alijibu na kusema,
Then Zophar, the Naamathite, answered,
2 “Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa? Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?
"Shouldn't the multitude of words be answered? Should a man full of talk be justified?
3 Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?
Should your boastings make men hold their peace? When you mock, shall no man make you ashamed?
4 Kwa kuwa wewe unasema kwa Mungu, 'Imani yangu ni safi, Mimi sina waa lolote machoni pako.'
For you say, 'My doctrine is pure. I am clean in your eyes.'
5 Lakini, laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;
But oh that God would speak, and open his lips against you,
6 hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima! Kwa kuwa yeye ni mkuu katika ufahamu. Tena tambua huyo Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.
that he would show you the secrets of wisdom. For true wisdom has two sides. Know therefore that God exacts of you less than your iniquity deserves.
7 Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?
"Can you fathom the mystery of God? Or can you probe the limits of Shaddai?
8 Upeo uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu; waweza kufahamu nini wewe? (Sheol h7585)
They are high as heaven. What can you do? They are deeper than Sheol. What can you know? (Sheol h7585)
9 Vipimo vyake ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.
Its measure is longer than the earth, and broader than the sea.
10 kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye?
If he passes by, or confines, or convenes a court, then who can oppose him?
11 Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka?
For he knows false men. He sees iniquity also, even though he doesn't consider it.
12 Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.
An empty-headed man becomes wise when a man is born as a wild donkey's colt.
13 Lakini ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;
"If you set your heart aright, stretch out your hands toward him.
14 ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako, lakini hivyo tena unauweka mbali nawe, na haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.
If iniquity is in your hand, put it far away. Do not let unrighteousness dwell in your tents.
15 Ndipo kwa hakika ungeinua juu uso wako bila ishara ya aibu; Ni dhahiri, ungethibitika na usingeogopa.
Surely then you shall lift up your face without spot; Yes, you shall be steadfast, and shall not fear:
16 Wewe ungesahau mateso yako; ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.
for you shall forget your misery. You shall remember it as waters that are passed away.
17 Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri; japokuwa kulikuwa na giza, litakuwa kama asubuhi.
Life shall be clearer than the noonday. Though there is darkness, it shall be as the morning.
18 Ungekuwa salama kwa sababu kuna tumaini; ni dhahiri, wewe utapata usalama juu yako na utachukua pumziko lako katika usalama.
You shall be secure, because there is hope. Yes, you shall search, and shall take your rest in safety.
19 Pia ungelala chini katika pumziko, na hakuna ambaye angekufanya wewe uogope; hakika wengi wangetafuta upendeleo wako.
Also you shall lie down, and none shall make you afraid. Yes, many shall court your favor.
20 Lakini macho ya watu waovu yatashindwa; hawatakuwa na njia ya kukimbia; tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.
But the eyes of the wicked shall fail. They shall have no way to flee. Their hope shall be the giving up of the spirit."

< Ayubu 11 >