< Ayubu 10 >

1 Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
My soul is weary of my life; I will give free course to my complaint; I will speak in the bitterness of my soul.
2 Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
I will say unto God: Do not condemn me; make me know wherefore Thou contendest with me.
3 ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
Is it good unto Thee that Thou shouldest oppress, that Thou shouldest despise the work of Thy hands, and shine upon the counsel of the wicked?
4 Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
Hast Thou eyes of flesh? or seest Thou as man seeth?
5 Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
Are Thy days as the days of man, or Thy years as a man's days,
6 hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
That Thou inquirest after mine iniquity, and searchest after my sin,
7 ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
Although Thou knowest that I shall not be condemned; and there is none that can deliver out of Thy hand?
8 Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
Thy hands have framed me and fashioned me together round about; yet Thou dost destroy me!
9 Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
Remember, I beseech Thee, that Thou hast fashioned me as clay; and wilt Thou bring me into dust again?
10 Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
Hast Thou not poured me out as milk, and curdled me like cheese?
11 Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
Thou hast clothed me with skin and flesh, and knit me together with bones and sinews.
12 Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
Thou hast granted me life and favour, and Thy providence hath preserved my spirit.
13 Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
Yet these things Thou didst hide in Thy heart; I know that this is with Thee;
14 kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
If I sin, then Thou markest me, and Thou wilt not acquit me from mine iniquity.
15 Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
If I be wicked, woe unto me; and if I be righteous, yet shall I not lift up my head — being filled with ignominy and looking upon mine affliction.
16 Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
And if it exalt itself, Thou huntest me as a lion; and again Thou showest Thyself marvellous upon me.
17 Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
Thou renewest Thy witnesses against me, and increasest Thine indignation upon me; host succeeding host against me.
18 Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
Wherefore then hast Thou brought me forth out of the womb? Would that I had perished, and no eye had seen me!
19 Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
I should have been as though I had not been; I should have been carried from the womb to the grave.
20 Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
Are not my days few? Cease then, and let me alone, that I may take comfort a little,
21 kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
Before I go whence I shall not return, even to the land of darkness and of the shadow of death;
22 ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”
A land of thick darkness, as darkness itself; a land of the shadow of death, without any order, and where the light is as darkness.

< Ayubu 10 >