< Yeremia 9 >

1 Kama kichwa changu kingetoa maji, na macho yangu kuwa chemichemi ya machozi! kwa kuwa natamani kulia usiku na mchana kwa ajili yao waliokuwa binti za watu wangu ambao wameuawa.
Who will give water to my head, and a fountain of tears to my eyes? then would I weep for this my people day and night, [even] for the slain of the daughter of my people.
2 Kama mtu anganipatia mahali pa wasafiri nyikani ili nikae, mahali ambapo ningeenda kuwatelekeza watu wangu. Kama ningewaacha, kwa kuwa wote ni wazinzi, kundi la wenye hiana!
Who would give me a most distant lodge in the wilderness, that I might leave my people, and depart from them? for they all commit adultery, an assembly of treacherous men.
3 asema BWANA, “Huupinda ulimi wao kana kwamba ni upinde ili wapate kuongea uongo, lakini si kwa uamiinifu wao kwamba wanapata nguvu duniani. Wanatoka uovu mmoja hadi mwiingine. Hawanijui mimi.”
And they have bent their tongue like a bow: falsehood and not faithfulness has prevailed upon the earth; for they have gone on from evil to evil, and have not known me, says the Lord.
4 Kila mmoja wenu, awe mlinzi wa jirani yake na usimwamini hata ndugu yako yeyote. kwa kuwa kila ndugu ni mwongo,
Beware you each of his neighbour, and trust you not in your brethren: for every one will surely supplant, and every friend will walk craftily.
5 kila jirani anatembea akilaghai. Kila mwanamume anakejeli jirani yake na haongei ukweli. Ndimi zao hufundisha vitu vya uongo. Hujidhofisha ili kusema uongo.
Every one will mock his friend; they will not speak truth: their tongue has learnt to speak falsehoods; they have committed iniquity, they ceased not, so as to return.
6 Makazi yenu yako kati ya udanganyifu; kwa uongo wao wanakataa kunitambua mimi. Asema BWANA.”
[There is] usury upon usury, and deceit upon deceit: they would not know me, says the Lord.
7 Kwa hiyo BWANA wa majeshi asema hivi, “Tazama, Niko tayari kuwajaribu. Nitawajaribu nione. Jinsi gani niwezavyo kufanya kwa binti za watu wangu?
Therefore thus says the Lord, Behold, I will try them with fire, and prove them; for I will do [thus] because of the wickedness of the daughter of my people.
8 Ndimi zao ni mishale iliyochongoka; huongea vitu vya uasi. Kwa midomo yao wanatangaza amani pamoja na jirani zao, lakini katika mioyo yao wanadanganya wakati wa kusubri.
Their tongue is a wounding arrow; the words of their mouth are deceitful: [one] speaks peaceably to his neighbour, but in himself retains enmity.
9 Kwa nini nisiwaadhibu kwa sababu ya mambo haya - asema BWANA na kwa nini nisijilipizie kisasi kwa taifa ambalo liko kama hili?
Shall I not visit for these things? says the Lord: and shall not my soul be avenged on such a people as this?
10 Nitaimba wimbo wa kuomboleza na kulia kwa ajili ya milima, na wimbo wa mazishi utaimbwa nyikani. Kwa kuwa wameteketezwa kwa hiyo hakuna anAyeweza kupita kati kati yao. Hawatasikia sauti ya ng'ombe yeyote. Ndege wa angani na wanyama wote wamekimbia.
Take up a lamentation for the mountains, and a mournful dirge for the paths of the wilderness, for they are desolate for lack of men; they heard not the sound of life from the birds of the sky, nor the cattle: they were amazed, they are gone.
11 Kwa hiyo nitaigeuza Yerusalemu kuwa vifusi vya ukiwa, maficho ya mbweha. Nitaifanya miji ya Yuda kuwa miji iliyoharibiwa isiyokaliwa na watu.
And I will remove the inhabitants of Jerusalem, and make it a dwelling-place of dragons; and I will utterly waste the cities of Juda, so that they shall not be inhabited.
12 Ni nani mwenye hekima anayeyaelewa haya? Je, kinywa cha BWANA kinatangaza nini kwake ili aweze kuyasema? Kwa nini nchi imepotea? Imeharibiwa kama jangwa, ambapo hakuna apitaye kati kati yake.
Who is the wise man, that he may understand this? and he that has the word of the mouth of the Lord [addressed] to him, let him tell you therefore the land has been destroyed, has been ravaged by fire like a desert, so that no one passes through it.
13 BWANA asema, “Ni kwa sababu wameziacha sheria zake ambazo niliwatengenezea, kwa sababu hawaisikilizi sauti yangu au kuishi kwa kuifuta.
And the Lord said to me, Because they have forsaken my law, which I set before them, and have not listened to my voice;
14 Ni kwa sababu wameishi kwa ushupavu wa mioyo yao na wamewafuata Mabaali kama baba zao walivyowafundisha kufanya.
but went after the lusts of their evil heart, and after the idols which their fathers taught them [to worship]:
15 Kwa hiyo BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, 'Tazama, Ninataka kuwafanya hawa watu wale pakanga na kunywa maji ya sumu.
therefore thus says the Lord God of Israel, Behold, I will feed them with trouble and will cause them to drink water of gall:
16 Ndipo nitakapowasambaza kati ya mataifa ambayo hawajayajua, wao wala mababu zao. Nitatuma upanga kwa ajili yao mpaka nimewaangamiza wote kabisa.'”
and I will scatter them amongst the nations, to them whom neither they nor their fathers knew; and I will send a sword upon them, until I have consumed them with it.
17 BWANA wa majeshi asema hivi, “Yafikirini haya: Waiteni waliaji; waje. Tumeni wanawake wenye taaluma ya kuomboleza, waje.
Thus says the Lord, Call you the mourning women, and let them come; and send to the wise women, and let them utter their voice;
18 Waje haraka waimbe wimbo wa maombolezo juu yetu, ili macho yetu yatokwe na machozi na kope zetu zibubujikwe na maji.
and let them take up a lamentation for you, and let your eyes pour down tears, and your eyelids drop water.
19 Kwa kuwa sauti ya kilio imesikika Sayuni, 'Jinsi tulivyoharibiwa. Tumeaibishwa sana, kwa kuwa tumeitelekeza nchi tangu walIpoangusha nyumba zetu.'
For a voice of lamentation has been heard in Sion, How are we become wretched! we are greatly ashamed, for we have forsaken the land, and have abandoned our tabernacles!
20 Kwa hiyo ninyi wanawake, sikieni neno la BWANA; zingatieni ujumbe unaokuja toka kinywani mwake. Kisha wafundisheni binti zenu wimbo wa maombolezo, na kila mwanamke wa jirani wimbo wa kilio.
Hear now, you women, the word of God, and let your ears receive the words of his mouth, and teach your daughters lamentation, and [every] woman her neighbour a dirge.
21 Kwa kuwa vifo vimekuja kupitia dirishani; vinaelekea mahali petu. Vinawaharibu watoto kutoka nje na vijana kwenye viwanja vya miji.
For death has come up through your windows, it has entered into our land, to destroy the infants without, and the young men from the streets.
22 Uyatangaze haya, 'Asema BWANA - mizoga ya wanaume itaanguka kama mavi kwenye mashamba na kama mabua baada ya mvunaji, na hapatakuwa na mtu wa kuyakusanya.'”
And the carcases of the men shall be for an example on the face of the field of your land, like grass after the mower, and there shall be none to gather [them].
23 BWANA asema hivi, “Usimwache mtu mwenye busara ajivune kwa ajili ya hekima yake, au shujaa kwa sababu ya uwezo wake. Usimwache mtu tajiri ajivunie utajiri wake.
Thus says the Lord, Let not the wise man boast in his wisdom, and let not the strong man boast in his strength, and let not the rich man boast in his wealth;
24 Kwa kuwa kama mtu atajivunia chochote kile, acha iwe hivi, yeye awe na busra na kunijua mimi. Kwa kuwa mimi ni BWANA, atendaye katika agano la wema, haki, na hukumu duniani. Ni katika hili kwamba ninafurahia- asema BWANA.
but let him that boasts boast in this, the understanding and knowing that I am the Lord that exercise mercy, and judgement, and righteousness, upon the earth; for in these things is my pleasure, says the Lord.
25 Tazama, siku zaja - asema BWANA wakati nitakapowaadhibu wote ambao hawajatahiriwa ambao wako hivyo hivyo katika miili yao.
Behold, the days come, says the Lord, when I will visit upon all the circumcised their uncircumcision;
26 Nitaiadhibu Misri na Yuda, Edomu, watu wa Amoni, Moabu, na watu wote wanaonyoa denge. Kwani mataifa yote haya hayajatahiriwa, na nyumba yote ya Israeli ina moyo ambao haujatahiriwa.”
on Egypt, and on Idumea, and on Edom, and on the children of Ammon, and on the children of Moab, and on every one that shaves his face round about, [even] them that dwell in the wilderness; for all the Gentiles are uncircumcised in flesh, and all the house of Israel are uncircumcised [in] their hearts.

< Yeremia 9 >