< Yeremia 8 >

1 Wakati huo - BWANA asema - wataleta kutoka makaburini mifupa ya wafalme wa Yuda na wakuu wake, mifupa ya makuhani na ya manabii na mifupa ya wakazi wa Yerusalemu.
"At that time," says Jehovah, "they shall bring out the bones of the kings of Judah, and the bones of his officials, and the bones of the priests, and the bones of the prophets, and the bones of the inhabitants of Jerusalem, out of their graves;
2 Kisha wataitandaza nje mchana kweupe na mbalamwezi na nyota zote za angani; hivi vitu katika anga vimenifuata na kunitumikia, na kwamba vimetembea na kutafuta, na kwamba vimeniabudu. Mifupa haitakusanywa na kuzikwa tena. Itakuwa kama mavi juu ya uso wa dunia.
and they shall spread them before the sun, and the moon, and all the host of heaven, which they have loved, and which they have served, and after which they have walked, and which they have sought, and which they have worshiped: they shall not be gathered, nor be buried, they shall be for dung on the surface of the earth.
3 Na katika kila eneo lililobaki ambalo nimewafukuza, Watachagua mauti badala ya uzima kwa ajili yao, wote ambao watasalia kutokana na taifa hili ovu - asema BWANA wa majeshi.
Death shall be chosen rather than life by all the residue that remain of this evil family, that remain in all the places where I have driven them," says Jehovah of hosts.
4 Kwa hiyo uwaambie, 'BWANA asema hivi: Je, kuna mtu anyeanguka na hasimami? Je, kuna mtu anayepotea na hawezi kujaribu kurudi?
"Moreover you shall tell them, 'Thus says Jehovah: Shall men fall, and not rise up again? Shall one turn away, and not return?
5 Kwa nini hawa watu, Yerusalemu, wamegeukia uasi daima? Wanashikilia uongo na wanakataa kutubu.
Why then do these people of Jerusalem turn away in perpetual backsliding? They hold fast deceit; they refuse to return.
6 Nilikaa kwa uangalifu na nikasikiliza, lakini hawakuongea kilicho sahihi; hakuna aliyetubia uovu wake, hakuna asemaye, “Nimefanya nini?” Kila mmoja wao huenda kule anakotaka, kama farasi aendaye kasi vitani.
I listened and heard, but they did not speak what is right: no man repents him of his wickedness, saying, "What have I done?" Everyone turns to his course, as a horse that rushes headlong in the battle.
7 Hata koikoi angani hujua wakati sahihi; na njiwa, na mbayuayu, n a korongo. Huhama kwa wakati sahihi, lakini watu wangu hawayajui maagizo ya BWANA.
Yes, the stork in the sky knows her appointed times; and the turtledove and the swallow and the crane observe the time of their coming; but my people do not know Jehovah's law.
8 Kwa nini mnasema, “Sisi tuna hekima! na sheria ya BWANA tunayoi?” Hakika, Tazama! Kalamu yenye uongo ya mwandishi imefanya uongo.
How can you say, "We are wise, and the law of Jehovah is with us?" But, look, the lying pen of the scribes has worked falsehood.
9 Wenye hekima wataaibishwa. Wameyeyuka na na kunaswa. Tazama! wanakataa neno la BWANA, kwa hiyo hekima yao ni kwa ajili ya matumizi gani?
The wise men are disappointed, they are dismayed and taken: look, they have rejected the word of Jehovah; and what kind of wisdom is in them?
10 Kwa wake zao nitawapa wengine, na mashamba yao kwa wale watakaowamiliki, kwa kuwa kuanzia kijana hadi mkuu, kwa pamoja ni wachoyo! Kuanzia nabii hadi kuhani, wote wanasema uongo.
therefore I will give their wives to others, and their fields to those who shall possess them: for everyone from the least even to the greatest is given to covetousness; from the prophet even to the priest every one deals falsely.
11 Kwa kuwa wametibu jeraha ya binti za watu wangu kwa juu juu. Walijisemea, “Amani, Amani,” na kumbe hapakuwa na amani.
They have healed the hurt of the daughter of my people superficially, saying, "Peace, peace;" when there is no peace.
12 Je, waliona aibu walipofanya machukizo? Hawakuaibika. Hawakuwa na utu. Kwa hiyo wataanguka wakati wa adhabu, pamoja na wale walioanguka. Watatupwa chini, asema BWANA.
Were they ashamed when they had committed abomination? No. They were not at all ashamed, neither could they blush: therefore shall they fall among those who fall; in the time of their visitation they shall be cast down, says Jehovah.
13 Nitawaondoa kabisa - asema BWANA - hapatakuwa na zabibu kwenye mizabibu yao, wala tini katika mitini yao. kwa kuwa jani litanyauka, na kile nilichowapatia kitaisha.
I will utterly consume them, says Jehovah: no grapes shall be on the vine, nor figs on the fig tree, and the leaf shall fade; and the things that I have given them shall pass away from them.'"
14 Kwa nini tunakaa hapa? Njoni pamoja; twendeni kwenye hiyo miji yenye maboma, na tutakaa kimya kule katika kifo. Kwa kuwa BWANA, Mungu wetu atatunyamazisha. Atatufanya tunywe sumu, kwa kuwa tumemtenda dhambi.
"Why do we sit still? Assemble yourselves, and let us enter into the fortified cities, and let us be silent there; for Jehovah our God has put us to silence, and given us water of gall to drink, because we have sinned against Jehovah.
15 Tunatumainia amani, lakini hakutakuwa na jema. Tunatumainia wakati wa uponyaji, lakini tazama kutakuwa na hofu.
We looked for peace, but no good came; and for a time of healing, and look, dismay.
16 Mkoromo wa farasi wake umesikika kutoka Dani. Dunia nzima inatikisika kwa sababu ya sauti ya kukaribia kwa farasi wake wenye nguvu. Kwa kuwa watakuja kuiangamiza nchi na utajiri wake, mji na wote wakaao nadani yake.
The snorting of his horses is heard from Dan: at the sound of the neighing of his strong ones the whole land trembles; for they have come, and have devoured the land and all that is in it; the city and those who dwell in it.
17 Hebu tazama, ninawatuma nyoka kati yenu, fira ambao hawawezi kuzuiliwa kwa uganga. Watawauma - asema BWANA,”
For, look, I will send serpents, adders, among you, which will not be charmed; and they shall bite you," says Jehovah.
18 Huzuni yangu haina ukomo, na moyo wangu unaugua.
"My joy for me is sorrow. My heart is faint within me.
19 Tazama! sauti ya maumivu ya binti wa watu wangu kutoka mbali! Je, BWANA hayumo Sayuni? Je, mfalme wake hayumo ndani yake? Kwa nini sasa wananichukiza kwa vitu vya kuchongwa na sanamu za kigeni zilizo batili?
Look, the voice of the cry of the daughter of my people from a land that is very far off: 'Isn't Jehovah in Zion? Isn't her King in her?'" "Why have they provoked me to anger with their engraved images, and with foreign vanities?"
20 Mavuno yamepita, wakati wa hari umekwisha. Lakini sisi hatujaokoka.
"'The harvest is past, the summer is ended, and we are not saved.'
21 Nimeumia kwa sababu ya maumivu ya binti wa watu wangu. Ninaomboleza kwa sababu ya mambo ya kushangaza ambayo yametokea kwake; Nimeyeyuka.
For the hurt of the daughter of my people am I hurt: I mourn; dismay has taken hold on me.
22 Je, kule Gileadi hakuan dawa? Je, huko hayuko mponyaji? Kwa nini uponyaji wa binti wa watu wangu hautokei?
Is there no balm in Gilead? Is there no physician there? Why then isn't the health of the daughter of my people recovered?

< Yeremia 8 >