< Yeremia 51 >

1 Yahwe asema hivi: Tazama, ninakwenda kuleta upepo wa maangamizi dhidi ya Babeli na dhidi yao waishio ndani ya Leb Kamei.
thus to say LORD look! I to rouse upon Babylon and to(wards) to dwell Leb (Leb)-kamai spirit to ruin
2 Nitawatuma Babeli wageni. Watamtawanya na wataifanya ukiwa nchi yake, maana watakuja kinyume chake kutoka pote siku ya madhara.
and to send: depart to/for Babylon be a stranger and to scatter her and to empty [obj] land: country/planet her for to be upon her from around: side in/on/with day distress: harm
3 Msiwaache wapiga mishale wakapinda pinde zao; msiwache wakavaa silaha zao. Msiwahifadhi vijana wake wa kiume; litengeni jeshi lake lote kwa maangamizi.
not to tread (to tread *QK) [the] to tread bow his and not to ascend: rise in/on/with armor his and not to spare to(wards) youth her to devote/destroy all army her
4 Maana watu waliojeruhiwa wataanguka katika nchi ya Wakaldayo; waliouawa wataanguka katika mitaa yake.
and to fall: fall slain: killed in/on/with land: country/planet Chaldea and to pierce in/on/with outside her
5 Maana Israeli na Yuda hawajaachwa na Mungu wao, na Yahwe wa majeshi, japokuwa nchi yao imejaa na maasi yaliyotendwa kinyume cha Mmoja aliye Mtakatifu wa Israeli.
for not forsaken Israel and Judah from God his from LORD Hosts for land: country/planet their to fill guilt (offering) from holy Israel
6 Kimbieni kutoka Babeli; kila mtu na ajiokoe mwenyewe. Msiangamie katika maasi yake. Maana ni wakati wa kisasi cha Yahwe. Atamlipa kwa yote.
to flee from midst Babylon and to escape man: anyone soul: life his not to silence: destroyed in/on/with iniquity: punishment her for time vengeance he/she/it to/for LORD recompense he/she/it to complete to/for her
7 Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa Yahwe kilichoinywesha nchi yote; mataifa walikunywa mvinyo wake wakawa wendawazimu.
cup gold Babylon in/on/with hand LORD be drunk all [the] land: country/planet from wine her to drink nation upon so to be foolish nation
8 Babeli utaanguka ghafla na kuangamizwa. Mwombolezeeni! mpeni dawa kwa maumivu yake; pengine aweza kupona.
suddenly to fall: fall Babylon and to break to wail upon her to take: take balsam to/for pain her perhaps to heal
9 Tulinuia kumponya Babeli, lakini hajaponywa, haya na tumwache twende, katika nchi yetu. Maana hatia yake imefika juu mbinguni; imerundikwa kufika mawinguni.
(to heal *Qk) [obj] Babylon and not to heal to leave: forsake her and to go: went man: anyone to/for land: country/planet his for to touch to(wards) [the] heaven justice: judgement her and to lift: raise till cloud
10 Yahwe ametamka kwamba sisi hatuna hatia. Njooni, teseme katika Sayuni matendo ya Yahwe Mungu wetu.'
to come out: send LORD [obj] righteousness our to come (in): come and to recount in/on/with Zion [obj] deed: work LORD God our
11 Noweni mishale na kuchukua ngao. Yahwe anaiimiza roho ya mfalme wa Umedi katika mpango wa kuiangamiza Babeli. Hii ni kwa kisasi cha Yahwe, kisasi kwa maangamizi ya hekalu lake.
to purify [the] arrow to fill [the] shield to rouse LORD [obj] spirit king Mede for upon Babylon plot his to/for to ruin her for vengeance LORD he/she/it vengeance temple his
12 Inueni bendela juu ya kuta za Babeli; wekeni walinzi. Wekeni waangalizi; wekeni askari waviziao ili kumkamata kila akimbiliaye mjini, maana Yahwe atafanya kile alichokipanga. Atafanya alichokisema juu ya wakaao Babeli.
to(wards) wall Babylon to lift: raise ensign to strengthen: strengthen [the] custody to arise: establish to keep: guard to establish: prepare [the] to ambush for also to plan LORD also to make: do [obj] which to speak: speak to(wards) to dwell Babylon
13 Enyi mwishio kati ya chemchemi nyingi za maji, ninyi mlio na wingi wa hazina, mwisho wenu umefika. upindo wa maisha yenu umepunguzwa.
(to dwell *Qk) upon water many many treasure to come (in): come end your cubit unjust-gain your
14 Yahwe wa majeshi ameapa kwa maisha yake, 'nitakujaza na adui zako, kama pigo la nzige; watainua kelele za vita juu yako.'
to swear LORD Hosts in/on/with soul: myself his that if: except if: except to fill you man like/as locust and to sing upon you shout
15 Ameifanya dunia kwa nguvu zake; akaiweka dunia mahali kwa hekima yake. Kwa ufahamu wake alizitanda mbingu.
to make land: country/planet in/on/with strength his to establish: make world in/on/with wisdom his and in/on/with understanding his to stretch heaven
16 Anapovuma, kunakuwa na mvumo wa maji mbinguni, maana huleta umande kutoka miisho ya dunia. Hufanya radi kwa ajili ya mvua na kuituma na kuutuma upepo kutoka katika maghala ya nyumba zake.
to/for voice to give: cry out he crowd water in/on/with heaven and to ascend: rise mist from end land: country/planet lightning to/for rain to make and to come out: send spirit: breath from treasure his
17 Kila mtu anakuwa kama mnyama asiye na akili; kila mfua chuma ameaibishwa na sanamu zake. Maana mwonekano wake unadanganya; maana hakuna uzima ndani yake.
be brutish all man from knowledge be ashamed all to refine from idol for deception drink offering his and not spirit: breath in/on/with them
18 Hazifai, kazi ya wafanya mzaa; wataangamizwa wakati wa kuadhibiwa kwao.
vanity they(masc.) deed: work delusion in/on/with time punishment their to perish
19 Lakini Mungu, urithi wa Yakobo, siyo kama hawa, maana yeye ndiye afanyaye vitu vyote. Israeli ni kabila ya urithi wake; Yahwe wa majeshi ni jina lake.
not like/as these portion Jacob for to form: formed [the] all he/she/it and tribe inheritance his LORD Hosts name his
20 Wewe ni nyundo ya vita yao, silaha ya vita yangu. Kwa wewe nitawaponda mataifa na kuharibu falme.
war-club you(m. s.) to/for me article/utensil battle and to shatter in/on/with you nation and to ruin in/on/with you kingdom
21 Kwa wewe nitaponda farasi na wawapandao; kwa wewe nitaponda vibandawazi na madereva wake.
and to shatter in/on/with you horse and to ride his and to shatter in/on/with you chariot and to ride his
22 Kwa wewe nitawafutilia mbali mme na mke; kwa wewe nitafutilia mbali mzee na kijana. Kwa wewe nitafutilia mbali kijana wa kiume na wasichana bikra.
and to shatter in/on/with you man and woman and to shatter in/on/with you old and youth and to shatter in/on/with you youth and virgin
23 Kwa wewe nitafutilia mbali wachungaji na makundi yao; kwa wewe nitawafutilia mbali wakulima na jozi zao za kulimia. kwa wewe nitawafutilia mbali watawala na maafsa.
and to shatter in/on/with you to pasture and flock his and to shatter in/on/with you farmer and pair his and to shatter in/on/with you governor and ruler
24 Maana mbele yako nitamlipa Babeli na wote wakaao Ukaldayo kwa maovu yote waliyoyafanya huko Sayuni - hili ni tamko la Yahwe.
and to complete to/for Babylon and to/for all to dwell Chaldea [obj] all distress: evil their which to make: do in/on/with Zion to/for eye your utterance LORD
25 Tazama, mimi ni kinyume chako, ewe mlima, wewe unayewaharibu watu wengine - hili ni tamko la Yahwe - kuiharibu dunia yote. Nitakupiga na mikono yangu na kuvingirisha chini kutoka ukingo wa kilima. Kisha nitakufanya mlima ulioteketezwa kabisa kwa moto.
look! I to(wards) you mountain: mount [the] destruction utterance LORD [the] to ruin [obj] all [the] land: country/planet and to stretch [obj] hand my upon you and to roll you from [the] crag and to give: make you to/for mountain: mount fire
26 Hivyo hawatachukua kwako jiwe lolote ili kujengea pembe ya nyumba au msingi; kwani utakuwa ukiwa wa milele - hili ni tamko la Yahwe.
and not to take: take from you stone to/for corner and stone to/for foundation for devastation forever: enduring to be utterance LORD
27 Inua bendela ya vita juu ya nchi. Piga tarumbeta katika mataifa. Yaite mataifa yamshambuliye: Ararati, Mini na Ashkenazi. Teua majemedari wa kumshambulia; leta farasi kama nzige warukao.
to lift: raise ensign in/on/with land: country/planet to blow trumpet in/on/with nation to consecrate: prepare upon her nation to hear: proclaim upon her kingdom Ararat Minni and Ashkenaz to reckon: overseer upon her official to ascend: attack horse like/as locust rough
28 Waandae mataifa kumshambulia: wafalme wa Umedi na magavana wao, maafsa wake wote na nchi yake yete.
to consecrate: prepare upon her nation [obj] king Mede [obj] governor her and [obj] all ruler her and [obj] all land: country/planet dominion his
29 Maana nchi itatikisika na kudhoofika, kwa kuwa mipango ya Yahwe inaendelea juu ya Babeli, kuifanya nchi ya Babeli kuwa nchi isiyofaa mahali pasipo na mtu.
and to shake [the] land: country/planet and to twist: writh in pain for to arise: establish upon Babylon plot LORD to/for to set: make [obj] land: country/planet Babylon to/for horror: destroyed from nothing to dwell
30 Maaskari wameacha kupigana huko Babeli; wamekaa katika ngome zao. Nguvu zao zimeshindwa; wamekuwa wanawake - nyumba zake zipo motoni, makomeo ya malango yake yamevunjika.
to cease mighty man Babylon to/for to fight to dwell in/on/with stronghold be dry might their to be to/for woman to kindle tabernacle her to break bar her
31 Mjumbe hukimbia ili amwambie mjumbe mwingine, na mtoa habari humwambia mtoa habari mwingine ili amwambie mfalme wa Babeli kwamba mji wake umetwaliwa kutoka mwisho hata mwisho.
to run: run to/for to encounter: meet to run: run to run: run and to tell to/for to encounter: meet to tell to/for to tell to/for king Babylon for to capture city his from end
32 Hivyo vivuko katika mito vimekamatwa; adui anaunguza mafunjo ya bwawa, na wapiganaji wa Babeli wamechanganyikiwa.
and [the] ford to capture and [obj] [the] pool to burn in/on/with fire and human [the] battle to dismay
33 Maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi: Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria. Ni muda wa kumkanyaga. Ni kitambo kidogo wakati wa mavuno utakuja juu yake.
for thus to say LORD Hosts God Israel daughter Babylon like/as threshing floor time to tread her still little and to come (in): come time [the] harvest to/for her
34 Yerusalemu husema, 'Nebukadneza mfalme wa Babeli amenirarua. Amenikausha na amenifanya kuwa mtungi mtupu. Amenimeza kama joka. Alijishibisha kwa chakula changu chema. Amenitupa mbali.'
(to eat me to confuse me *QK) Nebuchadnezzar king Babylon (to set me *QK) article/utensil vain (to swallow up me *QK) like/as serpent: monster to fill belly his from delicacy my (to wash me *QK)
35 Wenyeji wa Sayuni watasema, 'Gasia nilizofanyiwa na mwili wangu na ziwe kwa Babeli.' Yerusalem atasema, Damu yangu na iwe juu ya wakaao Ukaldayo.'
violence my and flesh my upon Babylon to say to dwell Zion and blood my to(wards) to dwell Chaldea to say Jerusalem
36 Kwa hiyo Yahwe asema hivi: Tazama, nikotayari kulitetea shitaka lako na kuleta kisasi kwa ajili yako. Maana nitayakausha maji ya Babeli na kufanya vyanzo vyake kukauka.
to/for so thus to say LORD look! I to contend [obj] strife your and to avenge [obj] vengeance your and to dry [obj] sea her and to wither [obj] fountain her
37 Babeli utakuwa rundo la magofu, pango la mbwea, sehemu itishayo, kitu cha kutoa sauti ya nyoka, pasipo na watu.
and to be Babylon to/for heap habitation jackal horror: appalled and hissing from nothing to dwell
38 Wababeli wataunguruma kwa pamoja kama wanasimba. Watanguruma kama watoto wa simba.
together like/as lion to roar to growl like/as whelp lion
39 wanapopashwa moto kwa hasira, nitawafanyia sherehe; nitawalewesha hata wafurahi, na kisha kulala usingizi usio na mwisho hata wasiamke - hili ni tamko la Yahwe -
in/on/with to warm they to set: make [obj] feast their and be drunk them because to exult and to sleep sleep forever: enduring and not to awake utterance LORD
40 nitawapeleka chini kama wanakondoo kwa mchinjaji, kama kondoo dume pamoja na mbuzi majike.
to go down them like/as ram to/for to slaughter like/as ram with goat
41 Jinsi Babeli ulivyotekwa! Hivyo fahari ya dunia yote imekamatwa. Jinsi Babeli ulivyofanyika sehemu yenye magofu kati ya mataifa.
how? to capture Babylon and to capture praise all [the] land: country/planet how? to be to/for horror: appalled Babylon in/on/with nation
42 Bahari imekuja juu ya Babeli! Amefunikwa na mawimbi yavumayo.
to ascend: rise upon Babylon [the] sea in/on/with crowd heap: wave his to cover
43 Miji yake imekuwa ukiwa, sehemu kame na nyika, nchi isiyo na watu, na hakuna mtu apitaye hapo.
to be city her to/for horror: appalled land: country/planet dryness and plain land: country/planet not to dwell in/on/with them all man and not to pass in/on/with them son: child man
44 Hivyo nitamwadhibu Beli huko Babeli; nitakitoa kinywani mwake alichokimeza, na mataifa hawatamminikia tena pamoja na wazao wao. Kuta za Babeli zitaanguka.
and to reckon: punish upon Bel in/on/with Babylon and to come out: send [obj] swallowing his from lip his and not to flow to(wards) him still nation also wall Babylon to fall: fall
45 Tokeni kati yake, enyi watu wangu. Kila mmoja wenu aokowe maisha yake kutoka katika hasira ya gadhabu yangu.
to come out: come from midst her people my and to escape man: anyone [obj] soul: life his from burning anger face: anger LORD
46 Msiache mioyo yenu ikaogopa au kuhofu habari iliyosikiwa nchini, maana habari itakuja siku moja. Baada yake mwaka unaofuata kutakuwa na habari, na ghasia zitakuwa nchini. Mtawala atakuwa kinyume cha mtawala.
and lest be tender heart your and to fear in/on/with tidings [the] to hear: hear in/on/with land: country/planet and to come (in): come in/on/with year [the] tidings and after him in/on/with year [the] tidings and violence in/on/with land: country/planet and to rule upon to rule
47 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja nitakapoadhibu sanamu za Babeli. Nchi yake yote itaaibika, na wote waliochinjwa wataanguka ndani yake.
to/for so behold day to come (in): come and to reckon: punish upon idol Babylon and all land: country/planet her be ashamed and all slain: killed her to fall: kill in/on/with midst her
48 Kisha mbingu na nchi, na vyote vilivyomo ndani yake vitafurahi juu ya Babeli. Maana mwalibifu atamwijia kutoka kaskazini - hili ni tamko la Yahwe.
and to sing upon Babylon heaven and land: country/planet and all which in/on/with them for from north to come (in): come to/for her [the] to ruin utterance LORD
49 “Kama Babeli alivyowafanya waliouawa wa Israeli kuanguka, hivyo waliouawa katika nchi yake wataanguka katika Babeli.
also Babylon to/for to fall: kill slain: killed Israel also to/for Babylon to fall: kill slain: killed all [the] land: country/planet
50 Ondokeni!, manusura wa vita, Msikawiye. Mkumbukeni Yahwe tokea mbali; Yerusalemu na ikumbukwe.
survivor from sword to go: went not to stand: stand to remember from distant [obj] LORD and Jerusalem to ascend: rise upon heart your
51 Tumeaibika, maana tumesikia matusi; dhihaka imefunika nyuso zetu, maana wageni wameingia mahali patakatifu pa nyumba ya Yahwe.
be ashamed for to hear: hear reproach to cover shame face our for to come (in): come be a stranger upon sanctuary house: temple LORD
52 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja - hivi ndivyo asemavyo Yahwe - nitakapoziadhibu sanamu zake, na waliojeruhiwa watanung'unika kwa maumivu katika nchi yake yote.
to/for so behold day to come (in): come utterance LORD and to reckon: punish upon idol her and in/on/with all land: country/planet her to groan slain: wounded
53 Maana hata kama Babeli angepanda mbinguni au kujenga ngome zake ndefu, aharibuye kutoka kwangu angemwendea - hili ni tamko la Yahwe.
for to ascend: rise Babylon [the] heaven and for to gather/restrain/fortify height strength her from with me to come (in): come to ruin to/for her utterance LORD
54 Kelele ya maangamizi ilitoka Babeli, anguko kubwa kutoka nchi ya Wakaldayo.
voice outcry from Babylon and breaking great: large from land: country/planet Chaldea
55 Maana Yahwe anaiharibu Babeli. Anaifanya kelele ya sauti yake kuisha. Adui zake wanaunguruma kama mawimbi ya maji mengi; kelele yao imekuwa na nguvu.
for to ruin LORD [obj] Babylon and to perish from her voice great: large and to roar heap: wave their like/as water many to give: cry out roar voice their
56 Maana aharibuye amekuja kinyume chake - kinyume cha Babeli! - na shujaa wake wametekwa. Pinde zao zimevunjwa, maana Yahwe ni Mungu wa kisasi; atatekeleza kisasi hiki.
for to come (in): come upon her upon Babylon to ruin and to capture mighty man her to to be dismayed bow their for God recompense LORD to complete to complete
57 Maana nitawafanya wana wafalme wake, wenye hekima wake, maofsa wake, na maaskari wake kulewa, nao watalala usingizi kwa usingizi usioisha na bila kuamka - hili ni tamko la mfalme: Yahwe wa majeshi ndilo jina lake.
and be drunk ruler her and wise her governor her and ruler her and mighty man her and to sleep sleep forever: enduring and not to awake utterance [the] king LORD Hosts name his
58 Yahwe wa majeshi asema hivi: Ukuta mnene wa Babeli utaangushwa kabisa, na malango marefu yataunguzwa. Kisha watu wanaokuja kumsaidia watafanya kazi isiyofaa; kila mataifa wanachojaribu kikifanya kwa ajili yake kitateketezwa kwa moto.”
thus to say LORD Hosts wall Babylon [the] broad: wide to strip to strip and gate her [the] high in/on/with fire to kindle and be weary/toil people in/on/with sufficiency vain and people in/on/with sufficiency fire and to faint
59 Hili ndilo neno Yeremia nabii alilomwamru Seraya mwana wa Neria mwana wa Makseya alipokwenda na Sedekia mfalme wa Yuda huko Babeli katika mwaka wa nne wa kutawala kwake. Basi Seraya alikuwa afsa mwandamizi.
[the] word which to command Jeremiah [the] prophet [obj] Seraiah son: child Neriah son: child Mahseiah in/on/with to go: went he with Zedekiah king Judah Babylon in/on/with year [the] fourth to/for to reign him and Seraiah ruler resting
60 Maana Yeremia alikuwa ameandika katika gombo kuhusu madhara yote yeliyokuwa yakienda kutendeka juu ya Babeli - maneno haya yote yaliyokuwa yameandikwa juu ya Babeli
and to write Jeremiah [obj] all [the] distress: harm which to come (in): come to(wards) Babylon to(wards) scroll: book one [obj] all [the] word [the] these [the] to write to(wards) Babylon
61 Yeremia akamwambia Seraya, “Unapokwenda Babeli, hakikisha unayasoma maneno haya yote.
and to say Jeremiah to(wards) Seraiah like/as to come (in): come you Babylon and to see: see and to call: read out [obj] all [the] word [the] these
62 Nawe utasema, 'Yahwe, wewe! - wewe mwenyewe umesema kwamba utapaharibu mahali hapa. Hapatakuwa na wa kukaa, kwamba ni watu au wanyama. Patakuwa nchi isiyofaa daima.'
and to say LORD you(m. s.) to speak: speak to(wards) [the] place [the] this to/for to cut: eliminate him to/for lest to be in/on/with him to dwell to/for from man and till animal for devastation forever: enduring to be
63 Kisha mtakapomaliza kusoma gombo hili, funga jiwe kubwa juu yake na ulitupe katikati ya Frati.
and to be like/as to end: finish you to/for to call: read out [obj] [the] scroll: book [the] this to conspire upon him stone and to throw him to(wards) midst Euphrates
64 Sema, 'Babeli utazama kama hivi. Hautainuka kwa sababu ya mabaya ninayoyapeleka juu yake, nao wataanguka.” Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.
and to say thus to sink Babylon and not to arise: rise from face: because [the] distress: harm which I to come (in): bring upon her and to faint till here/thus word Jeremiah

< Yeremia 51 >