< Yeremia 5 >

1 Kimbieni mkapite katika mitaa ya Yerusalemu, Tafuteni katika viwanja vyake. Kama mtaweza kumpata hata mtu mmoja anayetenda kwa haki na kufanya kwa uaminifu, basi nitaisamehe Yerusalemu.
"Run back and forth through the streets of Jerusalem, and see now, and know, and seek in the broad places of it, if you can find a man, if there are any who does justly, who seeks truth; and I will pardon her.
2 Hata kama wanasema, 'Kama BWANA aishivyo,' wanaapa uongo.”
Though they say, 'As the LORD lives;' surely they swear falsely."
3 BWANA, macho yako hayatazami uaminifu? Unawapiga watu, lakini hawasikii maumivu. Umewaangsmiza kabisa, lakini bado wanakataa kuwa waadilifu. Wanafanya nyuso zao kuwa ngumu kama mwamba. kwa kuwa wanakataa kutubu.
O LORD, do your eyes not look on truth? You have stricken them, but they were not grieved. You have consumed them, but they have refused to receive correction. They have made their faces harder than a rock. They have refused to return.
4 Kwa hiyo nilisema, “Hakika hawa ni watu masikini, Ni wapumbavu, Kwa kuwa hawazijui njia za BWANA, wala maagizo ya Mungu wao.
Then I said, "Surely these are poor. They are foolish; for they do not know the way of the LORD, nor the law of their God.
5 Nitaenda kwa watu wa muhimu na kutangaza ujumbe wa Mungu kwao, kwa kuwa angalau wanazijua njia za BWANA, maagizo ya Mungu wao. Lakini wote wanavunja nira yao pamoja; wote wanaivunja ile minyororo inayowafunga kwa ajili ya Mungu.
I will go to the great men, and will speak to them; for they know the way of the LORD, and the law of their God." But these with one accord have broken the yoke, and burst the bonds.
6 Kwa hiyo simba kutoka mwituni atawavamia. Mbweha kutoka Arabaha atawaangamiza. Chui ataivunja miji yao. Mtu yeyota anayeenda nje ya mji wake atavunjwavunjwa. Kwa kuwa maovu yao yameongezeka. Matendo yao ya uasi hayana ukomo.
Therefore a lion out of the forest shall kill them, a wolf of the evenings shall destroy them, a leopard shall watch against their cities; everyone who goes out there shall be torn in pieces; because their transgressions are many, and their backsliding is increased.
7 Kwa nini niwasamehe hawa watu? Wana wenu wameniacha na wamefanya viapo na wale ambao si miungu. Niliwalisha vya kutosha, lakini wamefanya uasherati na kuchukua alama za nyumba ya uzinzi.
"How can I pardon you? Your children have forsaken me, and sworn by what are no gods. When I had fed them to the full, they committed adultery, and assembled themselves in troops at the prostitutes' houses.
8 Walikuwa farasi wanaotafuta kupandwa. Walitembea huku na huku wakitafutwa kupandwa. Kila mwanamume alimkaribia mke wa jirani yake.
They were as fed horses roaming at large: everyone neighed after his neighbor's wife.
9 Kwa hiyo kwa nini nisiwaadhibu - asema BWANA - na kwa nini nisijilipizie kisasi juu ya taifa kama hili?
Shouldn't I punish them for these things?" says the LORD; "and shouldn't my soul be avenged on such a nation as this?
10 Nenda hadi kwenye kuta za shamba lake la mizabibu na zihariibuni. Lakini wao msiwaharibu kabisa. Ondoeni matawi kwa sababu hayatoki kwa BWANA.
"Go up on her walls, and destroy; but do not make a full end. Take away her branches; for they are not the LORD's.
11 Kwa sababu nyumba ya Yuda na Israeli wamenisaliti kabisa - asema BWANA -
For the house of Israel and the house of Judah have dealt very treacherously against me," says the LORD.
12 na wamenikataa. Wanasema, ''Yeye si halisi. Maovu hayawezi kutupata, wala hatutaona upanga wala njaa.
They have denied the LORD, and said, "It is not he; neither shall evil come on us; neither shall we see sword nor famine.
13 Kwa kuwa manabii wamekuwa si kitu kama upepo na hakuna mtu mwiingine wa kunena ujumbe wa BWANA kwetu. Vitisho vyao na viwjie wao wenyewe.”'
The prophets shall become wind, and the word is not in them. Thus shall it be done to them."
14 Kwa hiyo BWANA, Mungu wa majeshi asema hivi, tazama nataka kuweka maneno yangu katika kinywa chako. Yatakuwa kama moto na watu hawa watakuwa kama kuni! Kwa kuwa utawaramba.
Therefore thus says the LORD, the God of hosts, "Because you speak this word, look, I will make my words in your mouth fire, and this people wood, and it shall devour them.
15 Tazama nataka kuleta taifa dhidi yenu kutoka mbali, enyi nyumba ya Israeli - asema BWANA - ni taifa linalodumu, taifa la kale! Ni taifa ambalo lugha yake hamuijui, wala hamtaelewa wasemacho.
Look, I will bring a nation on you from far, house of Israel," says the LORD. "It is a mighty nation. It is an ancient nation, a nation whose language you do not know, neither understand what they say.
16 Podo lao ni kaburi wazi. Wote ni wanajeshi.
Their quiver is an open tomb, they are all mighty men.
17 Kwa hiyo mavuno yako yataliwa, wana wako na binti zako pia, na chakula chako. Watakula kondoo wako na ng'ombe wako, watakula matunda ya zabibu zako na ya mitiini. Wataiangusha chini miji yenu na boma zake ambazo mnazitumainia.
They shall eat up your harvest, and your bread, which your sons and your daughters should eat. They shall eat up your flocks and your herds. They shall eat up your vines and your fig trees. They shall beat down your fortified cities, in which you trust, with the sword.
18 Lakini hata katika siku hizo - asema BWANA - sikusudii kuwaharibu kabisa.
"But even in those days," says the LORD, "I will not make a full end with you.
19 Itatokea kwenu, ninyi Yuda na Israeli, mkisema, 'Kwa nini BWANA, Mungu wetu ametufanyia haya yote?' kwamba wewe Yeremia, utawaambia, 'Kama vile mlivyomwacha BWANA na kuabudu miungu mingine katika nchi yenu, vivyo hivyo mtawatumikia wageni katika nchi ambayo si yenu.'
It will happen, when you say, 'Why has the LORD our God done all these things to us?' Then you shall say to them, 'Thus says the LORD, Just like you have forsaken me, and served foreign gods in your land, so you shall serve strangers in a land that is not yours.'
20 Waambia haya watu wa nyumba ya Yakobo na yasikike katika Yuda. Waambie,
"Declare this in the house of Jacob, and publish it in Judah, saying,
21 'Sikilizeni hili, eny watu wapumbavu! Sanamu hazina matakwa; zina masikio lakini haziwawezi kusikia.
'Hear now this, foolish people, and without understanding; who have eyes, and do not see; who have ears, and do not hear:
22 Je, hamnihofu mimi - asema BWANA - au kutetemeka mbele ya uso wangu? Nimeweka mpaka wa mchanga kwenye bahari, ambao ni agizo la kudumu ambalo halibomoki - hata kama bahari ina kupwa na kujaa, bado hauwenzi kubomoka. Hata kama mawimbi yake yanaunguruma, hayawezi kuvuka.
Do you not fear me?' says the LORD 'Won't you tremble at my presence, who have placed the sand for the bound of the sea, by a perpetual decree, that it can't pass it? And though its waves toss themselves, yet they can't prevail; though they roar, yet they can't pass over it.'
23 Lakini hawa watu wana mioyo ya usumbufu. Hugeuka kuwa wapinzani na kuondoka.
"But this people has a revolting and a rebellious heart; they have revolted and gone.
24 Kwa kuwa hawasemi mioyoni mwao, “basi na tumche BWANA, Mungu wetu, yeye aletaye mvua za awali na mvua za vuli - kwa wakati wake, ambaye hutuzna majuma ya mavuno kwa ajili yetu.”
Neither do they say in their heart, 'Let us now fear the LORD our God, who gives rain, both the former and the latter, in its season; who preserves to us the appointed weeks of the harvest.'
25 uovu wako umezuia haya yasitokee. Dhambi zako zimeyazuia mambo mema yasitokee.
"Your iniquities have turned away these things, and your sins have withheld good from you.
26 Kwa watu waovu wamo kati ya watu wangu. Wanatazama kama mtu anayenyatia ili kukamata ndege; wanaweka mitego na kukamata watu;
For among my people are found wicked men. They watch, as fowlers lie in wait. They set a trap. They catch men.
27 Kama tundu la mtego lijaavyo ndege, nyumba zao zimejaa uongo. Kwa hiyo wanakua na kutajirika.
As a cage is full of birds, so are their houses full of deceit. Therefore they have become great, and grew rich.
28 Wamenenepa; wanang'aa na kupendeza. Wamepitiliza hata mipika ya maovu. Wala hawajali sababu ya kuwepo kwa watu na wala uwepo wa yatima. Wanafanikiwa hata kama hawatoi hukumu ya haki kwa yatima.
They have grown fat. They shine; yes, they excel in deeds of wickedness. They do not plead the cause, the cause of the fatherless, that they may prosper; and they do not judge the right of the needy.
29 Kwa nini nisiwadhibu kwa sababu ya haya - asema BWANA - sitajilipizia kisasi juu ya taifa la namna hii?
"Shall I not punish for these things?" says the LORD. "Shall not my soul be avenged on such a nation as this?
30 Jambo la ajabu na la kuchukiza limetokea katika nchi hii.
"An astonishing and horrible thing has happened in the land.
31 Mananbii wanatabiri kwa uongo, na makuhani wanatwala kwa msaada wa wa hao. Watu wangu wanapenda mambo ya hivyo, lakini mwisho kitatokea nini?
The prophets prophesy falsely, and the cohanim rule by their own authority; and my people love to have it so. What will you do in the end of it?

< Yeremia 5 >