< Yeremia 49 >

1 Juu ya watu wa Amoni, Yahwe asema hivi, “Je Israeli hana watoto? Je hakuna mtu wa kurithi chochote katika Israeli? Kwa nini Moleki aikalie Gadi, na watu wake kukaa katika miji yake?
Of [the] people of Ammon thus he says Yahweh ¿ [do] children not [belong] to Israel or? [does] an heir not [belongs] to it why? has he dispossessed Milcom Gad and people his in cities its has it dwelt?
2 Hivyo angalia, siku zinakuja - asema Yahwe - nitakapo sikizisha ishara ya vita juu ya Raba miongoni mwa watu wa Amoni, hivyo itakuwa rundo lililoachwa na binti zake watawasha moto. Maana Israeli atawamiliki wanaommiliki,” asema Yahwe.
Therefore here! days [are] coming [the] utterance of Yahweh and I will sound aloud against Rabbah of [the] people of Ammon a shout of battle and it will become a mound of desolation and daughters its with fire they will be kindled and it will dispossess Israel [those who] dispossessed it he says Yahweh.
3 Piga kelele kwa maombolezo, Heshboni, maana Ai utaangamizwa! Piga kelele, Binti za Raba! Vaeni nguo za magunia. Ombolezeni na kukimbia kwa kuchanganyikiwa, maana Moleki anakwenda matekani, pamoja na makuhani na viongozi wake.
Wail O Heshbon for it has been devastated Ai cry out O daughters of Rabbah gird yourselves sackcloth mourn and run to and fro among the walls for Milcom in exile he will go priests his and officials his together.
4 Kwa nini mnajivunia nguvu zenu? Nguvu zenu zitakwisha, binti wasioamini, ninyi mnaotumaini utajiri wenu. Mwasema, “Nani atakayekuja kinyume changu?'
Why? do you boast in the valleys [is] flowing valley your O daughter apostate who trusts in treasures her who? will he come against me.
5 Tazama, nitaleta kitisho juu yenu - hili ni tamko la Yahwe, Bwana wa majeshi - kitisho hiki kitatoka kwao wote wanaowazunguka. Kila mmoja wenu atatawanyika mbele yake. Hakutakuwa na wa kuwakusanya wanaotawanyika.
Here I [am] about to bring on you terror [the] utterance of [the] Lord Yahweh of hosts from all around you and you will be driven away everyone before it and not [one who] gathers together [belongs] to the fugitive.
6 Lakini baada ya haya nitarejesha mema ya watu wa Amoni - hili ni tamko la Yahwe.”
And after thus I will turn back [the] captivity of [the] people of Ammon [the] utterance of Yahweh.
7 Juu ya Edomu, Yahwe wa majeshi asema hivi, Je hakuna tena hekima katika Temani? Je ushauri mwema umepotea kutoka kwa wenye ufahamu? Je hekima yao imeharibika?
Of Edom thus he says Yahweh of hosts ¿ [is] there not still wisdom in Teman has it been lost? counsel from understanding [people] has it been corrupted? wisdom their.
8 Kimbieni! Rudini nyuma! Bakini katika mashimo katika ardhi, wenyeji wa Dedani. Maana naleta maafa ya Esau juu yake wakati ninaomwadhibu.
Flee be turned back make deep to dwell O inhabitants of Dedan for [the] disaster of Esau I will bring on it a time [when] I will visit it.
9 Ikiwa wavunaji wa zabibu walikuja kwako, je wasinge acha kidogo? Ikiwa wezi walikuja usiku, je wasingeiba kiasi walichotaka?
If grape gatherers they came to you not will they leave? gleanings if thieves in the night they destroyed sufficiency their.
10 Lakini nimempiga Esau kwa ukiwa. Nimefunua maficho yao. Hivyo hataweza kujificha mwenyewe. Watoto wake, ndugu zake, na jirani zake wameharibiwa, wamepotea.
For I I will strip bare Esau I will uncover hiding places its and it will hide itself not it will be able it will be devastated offspring its and relatives its and neighbors its and there not [will be] it.
11 Acha nyuma yatima wako. Nitachukua uhai wao, na wajane wako wanaweza kuniamini.”
Leave! fatherless your I I will preserve [them] alive and widows your on me let them rely.
12 Maana Yahwe asema hivi, “Tazama, wasiostahili ni lazima wanywe sehemu ya kikombe. Je mnadhani mtaachwa bila kuhadhibiwa? Hapana, maana hakika mtakunywa.
For thus - he says Yahweh there! [those] who not sentence their [was] to drink the cup completely they will drink [it] and you he completely will you be exempt from punishment? not you will be exempt from punishment for certainly you will drink [it].
13 Maana nimekwisha apa kwangu mimi mwenyewe - asema Yahwe - Hiyo Bozra itakuwa hofu, aibu, magofu, na kitu cha laana. Miji yake yote itakuwa magofu daima.
For by myself I swear [the] utterance of Yahweh that a waste a reproach a desolation and a curse it will become Bozrah and all cities its they will become ruins of perpetuity.
14 Nimesikia habari kutoka kwa Yahwe, na mjumbe ametumwa katika mataifa, 'Kusanyikeni na kumpiga. Jiandaeni kwa vita.'
A report I have heard from with Yahweh and an envoy among the nations [has been] sent gather together and come on it and rise up for battle.
15 “Maana tazama, nimekufanya kuwa mdogo kulinganisha na mataifa mengine, yenye kudharauliwa na watu.
For here! small I will make you among the nations despised among humankind.
16 Na kwa hofu yenu, kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wakaaji wa maeneo ya mwinuko, ninyi mliomiliki vilele vya vilima ili mfanye viota vyenu kama tai. Nitawashusha kutoka huko - asema Yahwe.
Horror your it has deceived you [the] arrogance of heart your O dweller in [the] clefts of the rock O occupant of [the] height[s] of a hill for you will make high like eagle nest your from there I will bring down you [the] utterance of Yahweh.
17 Edomu atakuwa kitisho kwa kila aipitaye. Kila mtu atatetemeka na kutoa sauti kwa sababu ya maafa yake.
And it will become Edom a horror every [one who] passes by at it he will be appalled and he may hiss on all wounds its.
18 Kama maangamizi ya Sodoma na Gomora na jirani zake,” asema Yahwe, “hakuna atakayeishi pale; hakuna mtu atakayekaa huko.
Like [the] overthrow of Sodom and Gomorrah and neighbors its he says Yahweh not he will dwell there anyone and not he will sojourn in it a child of humankind.
19 Tazama, nitapanda kama simba kutoka katika misitu ya Yordani hata eneo la malisho mabichi. Maana nitaharakisha kumfanya Edomu kumkimbia, nami nitamweka mwingine atakayekuwa amechaguliwa kwa usimamizi huo. Maana ni nani aliyekama mimi, ni nani atakayeniagiza kuja? Mchungaji gani awezaye kunizuia?
There! like a lion [which] it goes up from [the] thicket[s] of the Jordan to pastureland of an ever-flowing [stream] for I will act in a moment I will cause to run it from on it and whoever [is] chosen to it I will appoint for who? [is] like me and who? will he summon me and who? this [is] a shepherd who he will stand before me.
20 Hivyo sikiliza mipango ambayo Yahwe ameamua dhidi ya Edom, mipango aliyoifanya kinyume cha wakaao Temani. Bila shaka wataondolewa, hata kundi dogo kuliko yote. Nchi yao yenye malisho yao mabichi itageuzwa kuwa sehemu zenye magofu.
Therefore hear [the] plan of Yahweh which he has planned against Edom and purposes his which he has purposed against [the] inhabitants of Teman if not people will drag away them [the] young [ones] of the flock if not he will devastate on them pastureland their.
21 Kwa kishindo cha kuanguka kwao nchi hutikisika. Sauti ya milio ya kukata tamaa inasikika katika Bahari ya Shamu.
From [the] sound of falling they it will shake the earth of [the] calling out at [the] sea of reed[s] it will be heard sound its.
22 Tazama, mtu fulani atapiga kama tai, na kushuka chini kwa kasi na kueneza mabawa yake juu ya Bozra. Kisha katika siku hiyo, mioyo ya askari wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika kuzaa.”
There! like eagle someone will ascend and he may swoop down so he may spread out wings his over Bozrah and it will be [the] heart of [the] warriors of Edom on the day that like [the] heart of a woman in labor.
23 Juu ya Dameski: “Hamathi na Arpadi zitaaibika, maana wamesikia habari ya madhara. Wanayeyuka! Wamesumbuka kama bahari, isiyotulia.
Of Damascus it will be ashamed Hamath and Arpad for new[s] bad they have heard they will melt away [is] in the sea anxiety to be quiet not it will be able.
24 Dameski umekuwa dhaifu sana. Unageuka kukimbia; hofu imeushika, Maangaiko na maumivu yameupata, kama uchungu wa mwanamke ajifunguaye.
It will be disheartened Damascus it will turn back to flee and panic - it will take hold distress and pains it will seize it like [woman] giving birth.
25 Watu wake wanasema, “Umekuwaje mji maarufu, mji ambao nimeufurahia, kabla haujaachwa?
How! not it has been forsaken a city of (praise *Qk) [the] town of joy my.
26 Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika mitaa yake na askari wake wote watateketea siku hiyo - hili ni tamko la Yahwe wa majeshi.”
Therefore they will fall young men its in open places its and all [the] men of war they will be silenced in the day that [the] utterance of Yahweh of hosts.
27 “Maana nitawasha moto katika kuta za Dameski, nami nitazivunja ngome za Beni Hadadi.”
And I will kindle a fire at [the] wall of Damascus and it will consume [the] fortresses of Ben Hadad.
28 Juu ya Kedari na falme za Hazori, Yahwe amwambia hivi Nebukadneza (Basi Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa akienda kuyashambulia maeneo haya): “Inuka na uipige Kedari na kuwaharibu wale watu wa mashariki.
Of Kedar - and of [the] kingdoms of Hazor which he attacked (Nebuchadnezzar *QK) [the] king of Babylon thus he says Yahweh arise go up against Kedar and devastate [the] people of [the] east.
29 Jeshi lake litachukua hema zao na makundi yao, nguzo za hema yao, na vitu vyao vyote. Watachukua ngamia wao kutoka kwa watu wa Kedari na kuwambia, 'Hofu ipo pande zote!”
Tents their and flock[s] their people will take away tent curtains their and all equipment their and camels their they will carry off for themselves and people will call out to them terror [is] from round about.
30 Kimbia, Tangatanga mbali! Kaa katika maandaki ardhini, mkaao Hazori - asema Yahwe - maana Nebukadneza mfalme wa Babeli amepanga mpango kinyume chenu. Kimbieni! Geukeni!
Flee take flight exceedingly make deep to dwell O inhabitants of Hazor [the] utterance of Yahweh that he has planned on you Nebuchadnezzar [the] king of Babylon a plan and he has purposed (on you *QK) a purpose.
31 Simama! lishambulie taifa lililokatika amani, waishio salama,” asema Yahwe. Hawana malango wala nguzo ndani yao, na watu wake wanakaa wenyewe.
Arise go up against a nation at ease [which] dwells to security [the] utterance of Yahweh not a pair of gates and not a bar [belong] to it alone they dwell.
32 Maana farasi wao watakuwa mateka, na wingi wa mali zao utakuwa mateka wa vita. Kisha nitawatawanya katika kila upepo wanaonyoa pembe za nywele zao, nami nitaleta madhara juu yao kutoka kila upande - hili ni tamko ya Yahwe.
And they will become camels their spoil and [the] abundance of livestock their plunder and I will scatter them to every wind [those who] are cut off of [the] corner and from all sides its I will bring disaster their [the] utterance of Yahweh.
33 Hazori utakuwa makao ya mbwea, nchi isiyofaa daima. Hakuna atakayeishi huko; hakuna mwanadamu atakayekaa huko.”
And it will become Hazor a habitation of jackals a desolation until perpetuity not he will dwell there anyone and not he will sojourn in it a child of humankind.
34 Hili ni neno la Yahwe lililomwijia Yeremia nabii kuhusu Elamu. Ilikuwa wakati wa mwanzo wa kutawala kwake Sedekia mfalme wa Yuda, naye akasema,
Which it came [the] word of Yahweh to Jeremiah the prophet concerning Elam at [the] beginning of [the] reign of Zedekiah [the] king of Judah saying.
35 “Yahwe wa majeshi asema hivi: Tazama, ninakaribia kumvunja mpiga upinde wa Elamu, sehemu kuu ya nguvu zao.
Thus he says Yahweh of hosts here I [am] about to break [the] bow of Elam [the] beginning of strength their.
36 Maana nitaleta pepo nne kutoka katika pande nne za mbingu, nami nitawatawanya watu wa Elamu katika pepo hizo zote. Hakuta kuwa na taifa ambalo kwalo waliotawanywa kutoka Elamu hawatakwenda.
And I will bring against Elam four winds from [the] four [the] ends of the heavens and I will scatter them to all the winds these and not it will be the nation where not it will go there [the] outcasts of (Elam. *QK)
37 Hivyo nitawavunjavunja Elamu mbele ya adui zao na mbele ya watafutao uhai wao. Maana nitaleta maangamizo dhidi yao, hasira ya gadhabu yangu - hili ni tamko la Yahwe - nami nitapeleka upanga nyuma yao hata nitakapowafuta wote.
And I will shatter Elam before enemies their and before - [those who] seek life their and I will bring on them - calamity [the] burning of anger my [the] utterance of Yahweh and I will send after them the sword until have made an end of I them.
38 Kisha nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme na viongozi wao kutoka huko - asema Yahwe -
And I will set throne my in Elam and I will destroy from there king and officials [the] utterance of Yahweh.
39 na itakuwa siku zijazo kwamba nitarejesha mema ya Elamu - asema Yahwe.”
And it will be - at [the] end of the days (I will turn back *Qk) ([the] captivity of *Qk) Elam [the] utterance of Yahweh.

< Yeremia 49 >