< Yeremia 42 >

1 Kisha amri wote wa jeshi na Yonathan mwana wa Karea, Jezania mwana wa Hoshaia, na watu wote kutoka mdogo kwa mkubwa walimkaribia Yeremia nabii.
Then all the captains of the forces, and Johanan the son of Kareah, and Jezaniah the son of Hoshaiah, and all the people from the least even unto the greatest, came near,
2 Walisema naye, “Acha maombi yetu yaje mbele yako. Omba kwa ajili yetu kwa Yahwe Mungu wako kwa ajili ya watu hawa ambao wanabaki kwani tuko wachache katika idadi, kama unavyoona.
and said unto Jeremiah the prophet: 'Let, we pray thee, our supplication be accepted before thee, and pray for us unto the LORD thy God, even for all this remnant; for we are left but a few of many, as thine eyes do behold us;
3 Muulize Yahwe Mungu wako atuambia sisi njia yakuendea na nini tufanye.”
that the LORD thy God may tell us the way wherein we should walk, and the thing that we should do.'
4 Basi Yeremia nabii alisema nao, “Nimewasikia, Tazama, Nitaomba kwa Yahwe Mungu wenu kama mlivyoomba. Vyovyote Yahwe ananijibu, Nitawambia. Sitawaficha chochote ninyi.”
Then Jeremiah the prophet said unto them: 'I have heard you; behold, I will pray unto the LORD your God according to your words; and it shall come to pass, that whatsoever thing the LORD shall answer you, I will declare it unto you; I will keep nothing back from you.'
5 Walisema na Yeremia, “Na Yawhe awe shahidi mkweli na mwaminifu dhidi yenu, kama hatutafanya kila kitu ambacho Yahwe Mungu wenu anatuambia kufanya.
Then they said to Jeremiah: 'The LORD be a true and faithful witness against us, if we do not even according to all the word wherewith the LORD thy God shall send thee to us.
6 Hata kama ni vizuri au vibaya, tutatii sauti ya Yahwe Mungu wetu, ambaye tunawatuma ninyi, ili kwamba iwe vizuri pamoja nasi wakati tunatii sauti ya Yahwe Mungu wetu.”
Whether it be good, or whether it be evil, we will hearken to the voice of the LORD our God, to whom we send thee; that it may be well with us, when we hearken to the voice of the LORD our God.'
7 Basi ilitokea kwamba baada ya siku kumi, neno la Yahwe lilikuja kwa Yeremia.
And it came to pass after ten days, that the word of the LORD came unto Jeremiah.
8 Kwa hiyo Yeremia alimwita Yonathan mwana wa Karea na amri wote jeshi pamoja naye, na watu wote kutoka mdogo kwa mkubwa.
Then called he Johanan the son of Kareah, and all the captains of the forces that were with him, and all the people from the least even to the greatest,
9 Na alisema nao, “Yahwe, Mungu wa Israel, ambaye umenituma mimi ili niweze kuweka maombi yako mbele zake. Yahwe asema hivi,
and said unto them: 'Thus saith the LORD, the God of Israel, unto whom ye sent me to present your supplication before Him:
10 Kama mtarudi na kuishi katika nchi hii, basi nitawajenga na sitawararua chini; Nitapanda na sitawangoa, kwa kuwa nitageuza maafa ambayo nimeleta juu yako.
If ye will still abide in this land, then will I build you, and not pull you down, and I will plant you, and not pluck you up; for I repent Me of the evil that I have done unto you.
11 Msimugope mfalme wa Babeli, ambaye mnamuogopa. Msimuogope-hili ni tamko la Yahwe kwani niko pamoja nanyi kuwahifadhi na kuwaokoa toka mkono wake.
Be not afraid of the king of Babylon, of whom ye are afraid; be not afraid of him, saith the LORD; for I am with you to save you, and to deliver you from his hand.
12 Kwa kuwa nitawapa rehema. Nitakuwa na huruma juu yenu, na nitawarudisha kwenye nchi yenu.
And I will grant you compassion, that he may have compassion upon you, and cause you to return to your own land.
13 Lakini tudhani kusema kwamba, “Hatutakaa katika nchi hii”- kama hamtasikiliza sauti yangu, sauti ya Yahwe Mungu wenu.
But if ye say: We will not abide in this land; so that ye hearken not to the voice of the LORD your God;
14 Tudhani kwamba mnasema, “Hapana! Tutaenda kwenye nchi ya Misri, ambayo hatutaona vita yoyote, ambayo hatutasikia sauti ya tarumbeta, na hatutaona njaa ya chakula. Tutaishi huko.”
saying: No; but we will go into the land of Egypt, where we shall see no war, nor hear the sound of the horn, nor have hunger of bread; and there will we abide;
15 Sasa sikiliza neno hili la Yahwe, wewe mabaki ya Yuda. Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israel, asema hivi, 'Kama kweli mtatoka kwenda Misri, kwenda na kuishi huko,
now therefore hear ye the word of the LORD, O remnant of Judah: Thus saith the LORD of hosts, the God of Israel: If ye wholly set your faces to enter into Egypt, and go to sojourn there;
16 basi upanga ambao mnauogopa utawapita huko kwenye nchi ya Misri. Njaa ambayo mnawasiwasi nayo itawafatilia huko Misri. Na mtakufa huko.
then it shall come to pass, that the sword, which ye fear, shall overtake you there in the land of Egypt, and the famine, whereof ye are afraid, shall follow hard after you there in Egypt; and there ye shall die.
17 Basi itatokea kwamba wanaume wote waliondoka kwenda Misri kuishi huko watakufa kwa upanga, njaa, au pigo. Hapatakuwa na mwathirika wao, hakuna atakayetoroka maafa ambayo nitaleta juu yao.
So shall it be with all the men that set their faces to go into Egypt to sojourn there; they shall die by the sword, by the famine, and by the pestilence; and none of them shall remain or escape from the evil that I will bring upon them.
18 Kwa kuwa Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israel, asema hivi: Kama gadhabu yangu na hasira yangu imemwanga juu ya wakazi wa Yerusalem, kwa njia hiyo hasira yangu itamwangwa juu yenu kama mtaenda Misri. Mtakuwa sababu ya hasira na hofu, sababu la kuzungumza laana, na kitu kisichokuwa na heshima. Na hamtaona eneo hili tena.”
For thus saith the LORD of hosts, the God of Israel: As Mine anger and My fury hath been poured forth upon the inhabitants of Jerusalem, so shall My fury be poured forth upon you, when ye shall enter into Egypt; and ye shall be an execration, and an astonishment, and a curse, and a reproach; and ye shall see this place no more.
19 Basi Yeremia alisema, “Yahwe amezungumza kuhusu ninyi - mabaki ya Yuda. Msiende Misri! Unajua kwa hakika kwamba nimekuwa shahidi dhidi yenu leo.
The LORD hath spoken concerning you, O remnant of Judah: Go ye not into Egypt; know certainly that I have forewarned you this day.
20 Kwa kuwa mmejidanganya vibaya wenyewe wakati mliponituma mimi kwenda kwa Yahwe Mungu wenu na kusema, 'Omba kwa Yahwe Mungu wetu kwa ajili yetu. Kila kitu ambacho Yahwe Mungu wetu asema, tuambie, na tutaibeba.'
For ye have dealt deceitfully against your own souls; for ye sent me unto the LORD your God, saying: Pray for us unto the LORD our God; and according unto all that the LORD our God shall say, so declare unto us, and we will do it;
21 Kwa kuwa nimekwisha toa taarifa kwako leo, lakini hajusikiliza sauti ya Yahwe Mungu wenu au kwa chochote kuhusu ambacho alinituma mimi kwako.
and I have this day declared it to you; but ye have not hearkened to the voice of the LORD your God in any thing for which He hath sent me unto you.
22 Basi sasa, utajua kwa hakika kwamba utakufa kwa upanga, njaa, na pigo katika eneo ambalo ulitamani kwenda kuishi.”
Now therefore know certainly that ye shall die by the sword, by the famine, and by the pestilence, in the place whither ye desire to go to sojourn there.'

< Yeremia 42 >