< Yeremia 33 >

1 Kisha neno la Yahwe likaja kwa Yeremia mara ya pili, alipokuwa bado amefungwa ndani ya uwanja wa walinzi, likisema,
Then the word of Yahweh came to Jeremiah a second time, while he was still shut within the courtyard of the guard, saying,
2 Yahwe muumbaji, anasema hivi—Yahwe, aumbaye ili athibitishishe—Yahwe ndilo jina lake,
“Yahweh the maker, says this—Yahweh, who forms in order to establish—Yahweh is his name,
3 'Niite, na nitakuitika, nitakuelezea mambo makuu, siri ambazo huzielewi.'
'Call to me, and I will answer you. I will demonstrate great things to you, mysteries that you do not understand.'
4 Kwa maana Yahwe, Mungu wa Israel, anasema hivi kuhusu nyumba zilizo katika mji huu na nyumba za wafalme wa Yuda zilizobomolewa kwa sababu ya maboma na upanga,
For Yahweh, God of Israel, says this concerning the houses in this city and the houses of the kings of Judah that are torn down because of the siege ramps and the sword,
5 Wakaldayao wanakuja kupigana na kuzijaza nyumba kwa hizi kwa majeshi ya watu ambao wataua katika hasira yangu na ghadhabu yangu, nitakapouficha mji huu uso wangu kwa sababu ya uovu wao wote.
'The Chaldeans are coming to fight and to fill the houses with corpses of people whom I will kill in my wrath and fury, when I hide my face from this city because of all their wickedness.
6 Lakini ona, niko karibu kuleta uponyaji na tiba, kwa maana nitawaponya na nitawapa wingi wa, amani na uamainifu.
But see, I am about to bring healing and a cure, for I will heal them and will bring to them abundance, peace, and faithfulness.
7 Kwa maana nitawarudhisha wafungwa wao wa Yuda na Israeli; nitawajenga tena kama ilivyokuw mwanzo.
For I will bring back the fortunes of Judah and Israel; I will build them up as in the beginning.
8 Kisha nitawatakasa uovu wote walioufanya dhidi yangu. Nitasamehe makosa yote waliyonitenda, na na njia zote walizo asi dhidi yangu.
Then I will purify them from all the iniquity that they have committed against me. I will pardon all the iniquities that they have done against me, and all the ways that they rebelled against me.
9 Kwa maana mji huu kwa ajili yangu utakuwa chombo cha furaha, nyimbo, sifa na heshima kwa mataiafa yote ya dunia ambao watasikia mambo yote mema ninayokwenda kufanya kwa ajili ya huu mji. Kisha wataogopa na kutetemeka kwa sababu ya mambo yote mema na amani nitayoupa mji huu.'
For this city will become for me an object of joy, a song of praise and honor for all the nations of the earth who will hear of all the good things that I am going to do for it. Then they will fear and tremble because of all the good things and the peace that I will give to it.'
10 Yahwe anasema hivi, 'Katika sehemu hii ambayo sasa mnaisema, “Imetengwa, sehemu isiyo na mwanadamu wala mnyama,” katika mji huu wa Yuda, na katika mitaa ya Yerusalemu ambayo imetengwa bila mwanadamu wala mnyama, zitasikika tena
Yahweh says this, 'In this place about which you are now saying, “It is desolate, a place with neither man nor beast,” in the cities of Judah, and in the streets of Jerusalem that are desolate having neither man nor beast, there will be heard again
11 sauti za furaha na sauti za shangwe, sauti ya bwana arusi na sauti ya bibi arusi, sauti za wale wasemao, wanapoleta shukrani katika nyumba ya Yahwe, “Mshukuruni Yahwe wa majeshi, kwa maana Yahwe ni mwema, na upendo wake usioshindwa wadumu milele!” Kwa maana nitawafanaya tena wafungwa wa nchi kuwa walivyokuwa mwanzo,' asema Yahwe.
the sound of joy and the sound of gladness, the sound of the groom and the sound of the bride, the sound of those who say, while they bring thank offerings to the house of Yahweh, “Give thanks to Yahweh of hosts, for Yahweh is good, and his unfailing love lasts forever!” For I will restore the fortunes of the land to what they were before,' says Yahweh.
12 Yahwe wa majeshi asema hivi: Katika sehemu hii ya ukiwa, ambamo sasa hakuna mwanadamu wala mnyama—katika miji yake yote kutakuwepo tena malisho ambapo wachungaji wataweza kupumzisha makundi yao.
Yahweh of hosts says this: 'In this desolate place, where now there is neither man nor beast—in all its cities there will again be pastures where shepherds can rest their flocks.
13 Katika miji hii katika nchi ya vilima, nchi tambarare, na Negevu katika nchi ya Benyamini na kuzunguka Yerusalemu yote, na katika miji ya Yuda, makundi yatapata njia chini ya mkono wa yule anayewahesabu,' asema Yahwe.
In the cities in the hill country, the lowlands, and the Negev, in the land of Benjamin and all around Jerusalem, and in the cities of Judah, the flocks will again pass under the hands of the ones counting them,' says Yahweh.
14 Angalia! Siku zinakuja—hili ni tangazo la Yahwe—ambapo nitafanya niliyoahidi kwa nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda.
'Look! Days are coming—this is Yahweh's declaration—when I will do what I have promised for the house of Israel and the house of Judah.
15 Katika siku hizo na katika wakati huo nitachipua shina la haki kwa ajili ya Daudi, na litafanaya hukumu na haki katika nchi.
In those days and in that time I will make a righteous branch to grow for David, and he will carry out justice and righteousness in the land.
16 Katika siku hizo Yuda wataokolewa, na Yurusalemu utaishi katika usalama, kwa maana hivi ndivyo atakavyoitwa, “Yahwe ni haki ni haki yetu.”
In those days Judah will be saved, and Jerusalem will live in security, for this is what she will be called, “Yahweh is our righteousness.”'
17 Kwa maana Yahwe anasema hivi: 'Mwana kutoka ukoo wa Daudi hatakosa kuketi katika kiti cha nyumba ya Israeli,
For Yahweh says this: 'A man from David's line will never be lacking to sit on the throne of the house of Israel,
18 wala mtu kutoka ukuhani wa Kilawi hatakosa kutoa sadaka za kuteketezwa mbele zangu, kutoa sadaka za chakula, na kutoa sadaka za nafaka wakati wote.”'
nor will a man from the Levitical priests be lacking before me to raise burnt offerings, to burn food offerings, and to perform grain offerings all the time.'”
19 Neno la Yahwe likaja kwa Yeremia, likisema,
The word of Yahweh came to Jeremiah, saying,
20 “Yahwe anasema hivi: 'Kama mkiweza kulivunja agano langu la mchana na usiku ili kwamba siku isikawie wala usiku usikawie kuja kwa wakati wake,
“Yahweh says this: 'If you can break my covenant with day and night so that there will no longer be day or night at their proper times,
21 basi mtaweza u kulivunja agano langu na Daudi mtumishi wangu, ili kwamba aspate mwana wa kuketi juu ya kiti chake cha enzi, na gano langu na makuhuni wa Kilawi, watumishsi wangu.
then you will be able to break my covenant with David my servant, so that he will no longer have a son to sit on his throne, and my covenant with the Levitical priests, my servants.
22 Kama vile majeshsi ya mbinguni yasivyoweza kuhesabika, na kama vile mchanga wa ufukwe wa bahari usivyoweza kupimwa, ndivyo nitakavyouongeza uzao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi watumikao mbele zangu.”
As the hosts of heaven cannot be counted, and as the sand of the seashores cannot be measured, so I will increase the descendants of David my servant and the Levites who serve before me.'”
23 Neno la Mungu likaja kwa Yeremia, likisema,
The word of Yahweh came to Jeremiah, saying,
24 Hamkuzingatia walichotangaza watu hawa waliposema, 'Zile Familia mbili ambazo Yahwe alizichagua, sasa amezikataa'? Kwa jinsi hii hii waliwapuuza watu wangu, wakisema kwamba si taifa tena katika macho yao.
“Have you not considered what this people has declared when they said, 'The two families that Yahweh chose, now he has rejected them'? In this way they despise my people, saying that they are no longer a nation in their sight.
25 Mimi, Yahwe, nasema hivi, 'Kama sijalithibitisha agano la mchana na usiku, na kama sijaziweka sheria za mbingu na dunia,
I, Yahweh, say this, 'If I have not established the covenant of day and night, and if I have not fixed the laws of heaven and earth,
26 basi nitawakataa uzao wa Yakobo na Daudi mtumishi wangu, na nisilete mtu kutoka kati yao wa kutawala juu ya uzao wa Abrahamu, Isaka, na Yakobo. Kwa maana nitawarudisha wafubgwa wao na kuonesha huruma kwao.”'
then I will reject the descendants of Jacob and David my servant, and not bring from them a person to rule over the descendants of Abraham, Isaac, and Jacob. For I will restore their fortunes and show mercy to them.'”

< Yeremia 33 >