< Yeremia 30 >

1 Neno lilokuja kwa Yeremia kutoka kwa Yahwe likisema,
A palavra que do Senhor veio a Jeremias, dizendo:
2 “Hivi ndivyo Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema, 'Jiandikie mwenyewe katika baraua maneno yote niliyotangaza kwako katika barua.
Assim diz o Senhor, Deus de Israel, dizendo: Escreve num livro todas as palavras que te tenho falado.
3 Maana ona, siku zinakuja—hili ni tangazo la Yahwe—nitakapowarudisha mateka wa watu wangu Israeli na Yuda. Mimi, Yahwe, nimesema hili. Kwa maana nitawarudisha kwenye nchi ambayo niliwapa babu zao, na wataimiliki.”'
Porque eis que dias veem, diz o Senhor, em que farei tornar o cativeiro do meu povo Israel e Judá, diz o Senhor; e torna-los-ei a trazer à terra que dei a seus pais, e a possuirão.
4 Haya ni maneno ambayo Yahwe anatangaza kuhusu Israeli na Yuda,
E estas são as palavras que falou o Senhor, acerca de Israel e de Judá.
5 “Kwa maana Yahwe anasema hivi, 'Tumesikia sauti ya kutetemesha ya hofu na wala siyo ya amani.
Porque assim diz o Senhor: Ouvimos uma voz de temor: temor há, porém não paz.
6 Ulizeni na muone kama mwanaume anamwogopa mtoto. Mbona ninamwona kila mwanaume kijana ameshika mikono yake juu ya kiuno chake kama mwanamke anayejifungua mtoto? Kwa nini nyuso zao wote zimegeuka rangi?
Perguntai, pois, e olhai, se o varão pare. Porque pois vejo a cada homem com as mãos sobre os lombos como a que está parindo? e porque se tem tornado todos os rostos em amarelidão?
7 Ole! Kwa maana siku hiyo itakuwa kuu, isiyofanana na yoyote. Utakuwa wakati wa huzuni kwa Yakobo, lakini ataokolewa.
Ah! porque aquele dia é tão grande, que não houve outro semelhante! e é tempo de angústia para Jacob: porém será livrado dela.
8 Kwa maana itakuwa katika siku hiyo—hili ni tangazo la Yahwe wa majeshi—kwamba nitaivunja nira ya shingo zenu, na nitaisambaza minyororo yenu, kwa hiyo wageni hawatawafanya watumwa tena.
Porque será naquele dia, diz o Senhor dos exércitos, que eu quebrarei o seu jugo de sobre o teu pescoço, e quebrarei as tuas ataduras; e nunca mais se servirão dele os estranhos.
9 Bali watamwabudu Yahwe Mungu wao na kumtumikia Daudi mfalme wao, ambaye nitamfanya mfalme juu yao.
Mas servirão ao Senhor, seu Deus, como também a David, seu rei, que lhes levantarei.
10 Kwa hiyo wewe, mtumishi wangu Yakobo, usiogope—hili ni tangazo la Yahwe—na usikate tamaa, Israeli. Maana ona, niko karibu kukurudisha kutoka mbali, na uzao wako kutoka nchi ya utumwa, Yakobo atarudi na kuwa katika amani; ataokolewa, na hapatakuwa na hofu zaidi.
Não temas pois tu, servo meu Jacob, diz o Senhor, nem te espantes, ó Israel; porque eis que te livrarei de terras de longe, como também à tua semente da terra do seu cativeiro; e Jacob tornará, e descançará, e ficará em sossego, e não haverá quem o atemorize.
11 Kwa maana niko pamoja nawe—hili ni tangazo la Yahwe—ili kukuokoa. Kisha nitaleta mwisho kamili kwa mataifa yote ambako nimewatawanya. Bali sitaweka mwisho kwako, ingawa ninakuadhibu kwa haki na kwa hakika sitakuacha bila kukuadhibu.'
Porque eu sou contigo, diz o Senhor, para te livrar; porquanto farei consumação de todas as nações entre as quais te espalhei; porém de ti não farei consumação, mas castigar-te-ei com medida, e de todo não te terei por inocente.
12 Kwa maana Yahwe anasema hivi, 'Jeraha lako si la kupona; kidonda chako kimeenea.
Porque assim diz o Senhor: Teu quebrantamento é mortal; a tua chaga é dolorosa.
13 Hakuna mtu wa kukutetea kesi yako; hakuna utetezi kwa ajili ya kidonda chako ili upone.
Não há quem julgue a tua causa para liga-la; não tens remédios que possam curar.
14 Wapenzi wako wote wamekusahau. Hawatakuangalia, kwa maana nimekujeruhi kwa jeraha la adui na nidhimu ya bwana mkatili kwa sababu ya uovu wako mwingi na dhambi zako zisizohesabika.
Todos os teus amantes já se esqueceram de ti, e não perguntam por ti; porque te feri de ferida de inimigo, e de castigo do cruel, pela grandeza da tua maldade e multidão de teus pecados.
15 Kwa nini unaita msaada kwa ajili ya jeraha lako? Maumivu yako hayaponyeki. kwa sambabu ya uovu wako mwingi, dhambi zako zisizohesabika, nimefanya mambo haya kwako.
Porque gritas por causa de teu quebrantamento? tua dor é mortal. Pela grandeza de tua maldade, e multidão de teus pecados, eu fiz estas coisas.
16 Kila mtu akulaye ataliwa, na adui zako wote wataenda utumwani. Kwa maana kila aliyekuteka nyara atatekwa, na nitawafanya wote wanaokuwinda kuwa mawindo.
Pelo que todos os que te devoram serão devorados; e todos os teus adversários, todos irão em cativeiro; e os que te roubam serão roubados, e a todos os que te despojam entregarei ao saque.
17 Kwa maana nitaleta uponyaji juu yako; nitakuponya majeraha yako—hili ni tangazo la Yahwe—nitafanya hivyo kwa sababu walikuita: Mwenyekutupwa. Hakuna anayeujali Sayuni.”
Porque te restaurarei a saúde, e te sararei das tuas chagas, diz o Senhor; porquanto te chamam a engeitada. Sião é, dizem, já não há quem pergunte por ela.
18 Yahwe anasema hivi, “Ona, niko karibu kuwarudisha mateka wa hema za Yakobo na kuwa na huruma juu ya nyumba zake. Kisha mji utajengwa juu ya lundo la magofu, na jumba litakuwepo tena kama ilivyokuwa kawaida.
Assim diz o Senhor: Eis que tornarei a trazer o cativeiro das tendas de Jacob, e apiedar-me-ei das suas moradas; e a cidade será reedificada sobre o seu montão, e o palácio estará posto como costuma.
19 Kisha wimbo wa kusifu na sauti ya ya shangwe itasikika kutoka kwao, kwa maana nitawaongeza na wala sitawapunguza; nitawaheshimu ili kwamba wasifanywe wanyonge.
E sairá deles o louvor e a voz de júbilo; e multiplica-los-ei, e não serão diminuídos, e glorifica-los-ei, e não serão acanhados.
20 Kisha watu watakuwa kama ilivyokuwa mwanzo, na kusanyiko lao litaanzishwa mbele yangu wakati nitakapowaadhibu wote wanaowatesa kwa sasa.
E seus filhos serão como da antiguidade, e a sua congregação será confirmada perante o meu rosto; e farei visitação sobre todos os seus opressores.
21 Kiongozi wao atatoka miongoni mwao. Atatokeza kutoka kati yao nitakapomleta karibu na atakapanikaribia mimi. kama sitafanya hivyo, ni nani atakayethubutu kunisogelea? —hili ni tangazo la Yahwe.
E o seu príncipe será deles; e o seu governador sairá do meio dele, e o farei aproximar, e ele se chegará a mim; porque quem será aquele que empenhe o seu coração para se chegar a mim? diz o Senhor.
22 Kisha mtakuwa watu wangu, na nitakuwa Mungu wenu.
E ser-me-eis por povo, e eu vos serei por Deus.
23 Ona, tufani ya Yahwe, ghadhabu yake, imekwenda nje. Ni tufani isiyokoma. Itazunguka juu ya vichwa vya watu waovu.
Eis que a tormenta do Senhor, a sua indignação, saiu, uma tormenta varredeira: cairá cruelmente sobre a cabeça dos ímpios.
24 Hasira ya Yahwe haitarudi mpaka itoke na kutimiza makusudi ya moyo wake. Katika siku za mwisho mtalielewa hili.”
Não voltará atráz o furor da ira do Senhor, até que tenha executado, e ate que tenha cumprido os desígnios do seu coração: no fim dos dias entendereis isto

< Yeremia 30 >