< Yeremia 30 >

1 Neno lilokuja kwa Yeremia kutoka kwa Yahwe likisema,
The word that came to Jeremiah from Yahweh, saying,
2 “Hivi ndivyo Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema, 'Jiandikie mwenyewe katika baraua maneno yote niliyotangaza kwako katika barua.
“This is what Yahweh, God of Israel, says, 'Write in a scroll all the words that I have spoken to you.
3 Maana ona, siku zinakuja—hili ni tangazo la Yahwe—nitakapowarudisha mateka wa watu wangu Israeli na Yuda. Mimi, Yahwe, nimesema hili. Kwa maana nitawarudisha kwenye nchi ambayo niliwapa babu zao, na wataimiliki.”'
For look, days are coming—this is Yahweh's declaration—when I will restore the fortunes of my people, Israel and Judah. I, Yahweh, have said it. For I will bring them back to the land that I gave their ancestors, and they will possess it.'”
4 Haya ni maneno ambayo Yahwe anatangaza kuhusu Israeli na Yuda,
These are the words that Yahweh declared concerning Israel and Judah,
5 “Kwa maana Yahwe anasema hivi, 'Tumesikia sauti ya kutetemesha ya hofu na wala siyo ya amani.
“For Yahweh says this, 'We have heard a trembling voice of dread and not of peace.
6 Ulizeni na muone kama mwanaume anamwogopa mtoto. Mbona ninamwona kila mwanaume kijana ameshika mikono yake juu ya kiuno chake kama mwanamke anayejifungua mtoto? Kwa nini nyuso zao wote zimegeuka rangi?
Ask and see if a man bears a child. Why do I see every young man with his hand on his loins like a woman bearing a child? Why have all their faces become pale?
7 Ole! Kwa maana siku hiyo itakuwa kuu, isiyofanana na yoyote. Utakuwa wakati wa huzuni kwa Yakobo, lakini ataokolewa.
Woe! For that day will be great, with none like it. It will be a time of anxiety for Jacob, but he will be rescued from it.
8 Kwa maana itakuwa katika siku hiyo—hili ni tangazo la Yahwe wa majeshi—kwamba nitaivunja nira ya shingo zenu, na nitaisambaza minyororo yenu, kwa hiyo wageni hawatawafanya watumwa tena.
For it will be in that day—this is the declaration of Yahweh of hosts—that I will break the yoke off your neck, and I will shatter your chains, so foreigners will no longer enslave you.
9 Bali watamwabudu Yahwe Mungu wao na kumtumikia Daudi mfalme wao, ambaye nitamfanya mfalme juu yao.
But they will worship Yahweh their God and serve David their king, whom I will make king over them.
10 Kwa hiyo wewe, mtumishi wangu Yakobo, usiogope—hili ni tangazo la Yahwe—na usikate tamaa, Israeli. Maana ona, niko karibu kukurudisha kutoka mbali, na uzao wako kutoka nchi ya utumwa, Yakobo atarudi na kuwa katika amani; ataokolewa, na hapatakuwa na hofu zaidi.
So you, my servant Jacob, do not fear—this is Yahweh's declaration—and do not be dismayed, Israel. For see, I am about to bring you back from far away, and your descendants from the land of captivity. Jacob will return and be at peace; he will be secure, and there will be no more terror.
11 Kwa maana niko pamoja nawe—hili ni tangazo la Yahwe—ili kukuokoa. Kisha nitaleta mwisho kamili kwa mataifa yote ambako nimewatawanya. Bali sitaweka mwisho kwako, ingawa ninakuadhibu kwa haki na kwa hakika sitakuacha bila kukuadhibu.'
For I am with you—this is Yahweh's declaration—to save you. Then I will bring a complete end to all the nations where I have scattered you. But I will certainly not put an end to you, though I discipline you justly and will certainly not leave you unpunished.'
12 Kwa maana Yahwe anasema hivi, 'Jeraha lako si la kupona; kidonda chako kimeenea.
For Yahweh says this, 'Your injury is incurable; your wound is infected.
13 Hakuna mtu wa kukutetea kesi yako; hakuna utetezi kwa ajili ya kidonda chako ili upone.
There is no one to plead your case; there is no remedy for your wound to heal you.
14 Wapenzi wako wote wamekusahau. Hawatakuangalia, kwa maana nimekujeruhi kwa jeraha la adui na nidhimu ya bwana mkatili kwa sababu ya uovu wako mwingi na dhambi zako zisizohesabika.
All of your lovers have forgotten you. They will not look for you, for I have wounded you with the wound of an enemy and the discipline of a cruel master because of your many iniquities and your innumerable sins.
15 Kwa nini unaita msaada kwa ajili ya jeraha lako? Maumivu yako hayaponyeki. kwa sambabu ya uovu wako mwingi, dhambi zako zisizohesabika, nimefanya mambo haya kwako.
Why do you call for help for your injury? Your pain is incurable. Because of your many iniquities, your innumerable sins, I have done these things to you.
16 Kila mtu akulaye ataliwa, na adui zako wote wataenda utumwani. Kwa maana kila aliyekuteka nyara atatekwa, na nitawafanya wote wanaokuwinda kuwa mawindo.
So everyone who consumes you will be consumed, and all of your adversaries will go into captivity. For the ones who have plundered you will become plunder, and I will make all of the ones despoiling you a spoil.
17 Kwa maana nitaleta uponyaji juu yako; nitakuponya majeraha yako—hili ni tangazo la Yahwe—nitafanya hivyo kwa sababu walikuita: Mwenyekutupwa. Hakuna anayeujali Sayuni.”
For I will bring healing on you; I will heal you of your wounds—this is Yahweh's declaration— I will do this because they called you: Outcast. No one cares for this Zion.'”
18 Yahwe anasema hivi, “Ona, niko karibu kuwarudisha mateka wa hema za Yakobo na kuwa na huruma juu ya nyumba zake. Kisha mji utajengwa juu ya lundo la magofu, na jumba litakuwepo tena kama ilivyokuwa kawaida.
Yahweh says this, “See, I am about to bring back the fortunes of Jacob's tents and have compassion on his homes. Then a city will be built on the heap of ruins, and a stronghold will exist again where it used to be.
19 Kisha wimbo wa kusifu na sauti ya ya shangwe itasikika kutoka kwao, kwa maana nitawaongeza na wala sitawapunguza; nitawaheshimu ili kwamba wasifanywe wanyonge.
Then a song of praise and a sound of merriment will go out from them, for I will increase them and not diminish them; I will honor them so they will not be humbled.
20 Kisha watu watakuwa kama ilivyokuwa mwanzo, na kusanyiko lao litaanzishwa mbele yangu wakati nitakapowaadhibu wote wanaowatesa kwa sasa.
Then their people will be like before, and their assembly will be established before me when I punish all the ones who are now tormenting them.
21 Kiongozi wao atatoka miongoni mwao. Atatokeza kutoka kati yao nitakapomleta karibu na atakapanikaribia mimi. kama sitafanya hivyo, ni nani atakayethubutu kunisogelea? —hili ni tangazo la Yahwe.
Their leader will come from among them. He will emerge from their midst when I draw him near and when he approaches me. If I do not do this, who would dare come close to me?—this is Yahweh's declaration.
22 Kisha mtakuwa watu wangu, na nitakuwa Mungu wenu.
Then you will be my people, and I will be your God.
23 Ona, tufani ya Yahwe, ghadhabu yake, imekwenda nje. Ni tufani isiyokoma. Itazunguka juu ya vichwa vya watu waovu.
See, the tempest of Yahweh, his fury, has gone out. It is a continual tempest. It will whirl on the heads of the wicked people.
24 Hasira ya Yahwe haitarudi mpaka itoke na kutimiza makusudi ya moyo wake. Katika siku za mwisho mtalielewa hili.”
Yahweh's wrath will not return until it has carried out and brought into being his heart's intentions. In the final days, you will understand it.”

< Yeremia 30 >