< Yeremia 30 >

1 Neno lilokuja kwa Yeremia kutoka kwa Yahwe likisema,
The word that came to Jeremiah from the LORD, saying:
2 “Hivi ndivyo Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema, 'Jiandikie mwenyewe katika baraua maneno yote niliyotangaza kwako katika barua.
'Thus speaketh the LORD, the God of Israel, saying: Write thee all the words that I have spoken unto thee in a book.
3 Maana ona, siku zinakuja—hili ni tangazo la Yahwe—nitakapowarudisha mateka wa watu wangu Israeli na Yuda. Mimi, Yahwe, nimesema hili. Kwa maana nitawarudisha kwenye nchi ambayo niliwapa babu zao, na wataimiliki.”'
For, lo, the days come, saith the LORD, that I will turn the captivity of My people Israel and Judah, saith the LORD; and I will cause them to return to the land that I gave to their fathers, and they shall possess it.'
4 Haya ni maneno ambayo Yahwe anatangaza kuhusu Israeli na Yuda,
And these are the words that the LORD spoke concerning Israel and concerning Judah.
5 “Kwa maana Yahwe anasema hivi, 'Tumesikia sauti ya kutetemesha ya hofu na wala siyo ya amani.
For thus saith the LORD: We have heard a voice of trembling, of fear, and not of peace.
6 Ulizeni na muone kama mwanaume anamwogopa mtoto. Mbona ninamwona kila mwanaume kijana ameshika mikono yake juu ya kiuno chake kama mwanamke anayejifungua mtoto? Kwa nini nyuso zao wote zimegeuka rangi?
Ask ye now, and see whether a man doth travail with child; wherefore do I see every man with his hands on his loins, as a woman in travail, and all faces are turned into paleness?
7 Ole! Kwa maana siku hiyo itakuwa kuu, isiyofanana na yoyote. Utakuwa wakati wa huzuni kwa Yakobo, lakini ataokolewa.
Alas! for that day is great, so that none is like it; and it is a time of trouble unto Jacob, but out of it shall he be saved.
8 Kwa maana itakuwa katika siku hiyo—hili ni tangazo la Yahwe wa majeshi—kwamba nitaivunja nira ya shingo zenu, na nitaisambaza minyororo yenu, kwa hiyo wageni hawatawafanya watumwa tena.
And it shall come to pass in that day, saith the LORD of hosts, that I will break his yoke from off thy neck, and will burst thy bands; and strangers shall no more make him their bondman;
9 Bali watamwabudu Yahwe Mungu wao na kumtumikia Daudi mfalme wao, ambaye nitamfanya mfalme juu yao.
But they shall serve the LORD their God, and David their king, whom I will raise up unto them.
10 Kwa hiyo wewe, mtumishi wangu Yakobo, usiogope—hili ni tangazo la Yahwe—na usikate tamaa, Israeli. Maana ona, niko karibu kukurudisha kutoka mbali, na uzao wako kutoka nchi ya utumwa, Yakobo atarudi na kuwa katika amani; ataokolewa, na hapatakuwa na hofu zaidi.
Therefore fear thou not, O Jacob My servant, saith the LORD; neither be dismayed, O Israel; for, lo, I will save thee from afar, and thy seed from the land of their captivity; and Jacob shall again be quiet and at ease, and none shall make him afraid.
11 Kwa maana niko pamoja nawe—hili ni tangazo la Yahwe—ili kukuokoa. Kisha nitaleta mwisho kamili kwa mataifa yote ambako nimewatawanya. Bali sitaweka mwisho kwako, ingawa ninakuadhibu kwa haki na kwa hakika sitakuacha bila kukuadhibu.'
For I am with thee, saith the LORD, to save thee; for I will make a full end of all the nations whither I have scattered thee, but I will not make a full end of thee; for I will correct thee in measure, and will not utterly destroy thee.
12 Kwa maana Yahwe anasema hivi, 'Jeraha lako si la kupona; kidonda chako kimeenea.
For thus saith the LORD: Thy hurt is incurable, and thy wound is grievous.
13 Hakuna mtu wa kukutetea kesi yako; hakuna utetezi kwa ajili ya kidonda chako ili upone.
None deemeth of thy wound that it may be bound up; thou hast no healing medicines.
14 Wapenzi wako wote wamekusahau. Hawatakuangalia, kwa maana nimekujeruhi kwa jeraha la adui na nidhimu ya bwana mkatili kwa sababu ya uovu wako mwingi na dhambi zako zisizohesabika.
All thy lovers have forgotten thee, they seek thee not; for I have wounded thee with the wound of an enemy, with the chastisement of a cruel one; for the greatness of thine iniquity, because thy sins were increased.
15 Kwa nini unaita msaada kwa ajili ya jeraha lako? Maumivu yako hayaponyeki. kwa sambabu ya uovu wako mwingi, dhambi zako zisizohesabika, nimefanya mambo haya kwako.
Why criest thou for thy hurt, that thy pain is incurable? For the greatness of thine iniquity, because thy sins were increased, I have done these things unto thee.
16 Kila mtu akulaye ataliwa, na adui zako wote wataenda utumwani. Kwa maana kila aliyekuteka nyara atatekwa, na nitawafanya wote wanaokuwinda kuwa mawindo.
Therefore all they that devour thee shall be devoured, and all thine adversaries, every one of them, shall go into captivity; and they that spoil thee shall be a spoil, and all that prey upon thee will I give for a prey.
17 Kwa maana nitaleta uponyaji juu yako; nitakuponya majeraha yako—hili ni tangazo la Yahwe—nitafanya hivyo kwa sababu walikuita: Mwenyekutupwa. Hakuna anayeujali Sayuni.”
For I will restore health unto thee, and I will heal thee of thy wounds, saith the LORD; because they have called thee an outcast: 'She is Zion, there is none that careth for her.'
18 Yahwe anasema hivi, “Ona, niko karibu kuwarudisha mateka wa hema za Yakobo na kuwa na huruma juu ya nyumba zake. Kisha mji utajengwa juu ya lundo la magofu, na jumba litakuwepo tena kama ilivyokuwa kawaida.
Thus saith the LORD: Behold, I will turn the captivity of Jacob's tents, and have compassion on his dwelling-places; and the city shall be builded upon her own mound, and the palace shall be inhabited upon its wonted place.
19 Kisha wimbo wa kusifu na sauti ya ya shangwe itasikika kutoka kwao, kwa maana nitawaongeza na wala sitawapunguza; nitawaheshimu ili kwamba wasifanywe wanyonge.
And out of them shall proceed thanksgiving and the voice of them that make merry; and I will multiply them, and they shall not be diminished, I will also increase them, and they shall not dwindle away.
20 Kisha watu watakuwa kama ilivyokuwa mwanzo, na kusanyiko lao litaanzishwa mbele yangu wakati nitakapowaadhibu wote wanaowatesa kwa sasa.
Their children also shall be as aforetime, and their congregation shall be established before Me, and I will punish all that oppress them.
21 Kiongozi wao atatoka miongoni mwao. Atatokeza kutoka kati yao nitakapomleta karibu na atakapanikaribia mimi. kama sitafanya hivyo, ni nani atakayethubutu kunisogelea? —hili ni tangazo la Yahwe.
And their prince shall be of themselves, and their ruler shall proceed from the midst of them; and I will cause him to draw near, and he shall approach unto Me; for who is he that hath pledged his heart to approach unto Me? saith the LORD.
22 Kisha mtakuwa watu wangu, na nitakuwa Mungu wenu.
And ye shall be My people, and I will be your God.
23 Ona, tufani ya Yahwe, ghadhabu yake, imekwenda nje. Ni tufani isiyokoma. Itazunguka juu ya vichwa vya watu waovu.
Behold, a storm of the LORD is gone forth in fury, a sweeping storm; it shall whirl upon the head of the wicked.
24 Hasira ya Yahwe haitarudi mpaka itoke na kutimiza makusudi ya moyo wake. Katika siku za mwisho mtalielewa hili.”
The fierce anger of the LORD shall not return, until He have executed, and till He have performed the purposes of His heart; in the end of days ye shall consider it.

< Yeremia 30 >