< Yeremia 24 >

1 Bwana alinionyeshea kitu. Tazama, vikapu viwili vya tini viliwekwa mbele ya hekalu la Bwana. (Maono haya yalitokea baada ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, kumchukua mateka Yekonia mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, maofisa wa Yuda, mafundi na wafua vyuma kutoka Yerusalemu na kuwapeleka Babeli.)
He showed me Yahweh and there! two baskets of figs [were] set before [the] temple of Yahweh after took into exile Nebuchadnezzar [the] king of Babylon Jeconiah [the] son of Jehoiakim [the] king of Judah and [the] officials of Judah and the craftsman and the smith[s] from Jerusalem and he brought them Babylon.
2 Kikapu kimoja cha tini kilikuwa nzuri sana, kama tini za kwanza zilizoiva, lakini kikapu kingine cha tini zilizokuwa mbaya sana zisizoweza kuliwa.
The basket one [was] figs good very like [the] figs of the early figs and the basket one [was] figs bad very which not they will be eaten from badness.
3 Bwana akaniambia, “Unaona nini Yeremia?” Nikasema, “Tini. Tini ambazo ni nzuri sana na tini ambazo ni mbaya sana haziwezi kuliwa.”
And he said Yahweh to me what? [are] you seeing O Jeremiah and I said figs the figs good [are] good very and the bad [figs] [are] bad very which not they will be eaten from badness.
4 Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,
And it came [the] word of Yahweh to me saying.
5 “Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi: nitawaangalia mateka wa Yuda kwa manufaa yao, kama vile tini hizi nzuri, nilipowatoa mateka kutoka hapa mpaka nchi ya Wakaldayo.
Thus he says Yahweh [the] God of Israel like the figs good these so I will regard [the] exile[s] of Judah whom I have sent from the place this [the] land of [the] Chaldeans for good.
6 Nitaweka macho yangu kwao wapate mema na kuwarejeshea nchi hii. Nitawajenga, wala sitawaangamiza.
And I will set eye my on them for good and I will bring back them to the land this and I will build up them and not I will tear [them] down and I will plant them and not I will pluck [them] up.
7 Nitawapanda, wala sitawang'oa. Ndipo nitawapa moyo wa kunijua; kwa kuwa mimi ndimi Bwana. Watakuwa watu wangu na mimi nitakuwa Mungu wao, hivyo watanirudia kwa moyo wao yote.
And I will give to them a heart to know me that I [am] Yahweh and they will become for me a people and I I will become for them God for they will return to me with all heart their.
8 Lakini kama vile tini mbaya ambazo ni hazifai kuliwa - asema Bwana - nitatenda hivi kwa Sedekia, mfalme wa Yuda, pamoja na viongozi wake, na pamoja na wengine wa Yerusalemu ambao wanabaki katika nchi hii au kwenda kukaa katika nchi ya Misri.
And like the figs bad which not they will be eaten from badness for thus - he says Yahweh so I will make Zedekiah [the] king of Judah and officials his and - [the] remnant of Jerusalem those [who] remain in the land this and those [who] dwell in [the] land of Egypt.
9 Nitawafanya kuwa kitu cha kutisha, wapate maafa, mbele ya falme zote duniani, aibu na somo kwa mithali, matusi, na laana mahali pote nitakapowafukuza.
And I will make them (into a terror *QK) into an evil to all [the] kingdoms of the earth into a reproach and into a byword into a taunt and into a curse in all the places where I will banish them there.
10 Nitatuma upanga, njaa, na tauni dhidi yao watapotelea mbali kutoka kwenye nchi niliyowapa wao na baba zao.”
And I will send on them the sword the famine and the pestilence until are finished they from on the ground which I gave to them and to ancestors their.

< Yeremia 24 >