< Yeremia 23 >

1 “Ole wao wachungaji ambao huangamiza na kuwatawanya kondoo wa malisho yangu-hii ndiyo ahadi ya Bwana.”
Malheur aux pasteurs qui perdent et dispersent les brebis de mon pâturage, — oracle de Yahweh!
2 Kwa hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi juu ya wachungaji ambao wanawachunga watu wake, “Ninyi mnawatawanya kundi langu na kuwafukuza. Hamuwajali hata kidogo. Tambueni hili! Mimi nitawalipiza uovu wa matendo yenu-hili ni tamko la Bwana.
C’est pourquoi ainsi parle Yahweh, Dieu d’Israël, touchant les pasteurs qui paissent mon peuple: Vous avez dispersé mes brebis, vous les avez chassées, vous n’en avez pas pris soin; voici que je vais prendre soin, contre vous, de la méchanceté de vos actions, — oracle de Yahweh.
3 Mimi mwenyewe nitakusanya mabaki ya kondoo wangu kutoka nchi zote nilizowafukuza, nami nitawarejesha kwenye eneo la malisho, ambako watazaa na kuongezeka.
Et moi je rassemblerai le reste de mes brebis, de tous les pays où je les aurai chassées, et je les ramènerai dans leur pâturage; elles croîtront et se multiplieront.
4 Ndipo nitawainua wachungaji juu yao ambao watawachunga hivyo hawataogopa tena au kupotezwa. Hakuna hata mmoja atakayepotea-hili ni tamko la Bwana.
Et je susciterai sur elles des pasteurs qui les paîtront; elles n’auront plus ni crainte ni terreur, et il n’en manquera plus aucune, — oracle de Yahweh!
5 Angalia, siku zinakuja-hili ndilo tamko la Bwana-nitakapomuinulia Daudi tawi la haki. Atatawala kama mfalme; atatenda kwa busara na kusababisha hukumu na haki katika nchi.
Voici que des jours viennent, — oracle de Yahweh, où je susciterai à David un germe juste; il régnera en roi et il sera sage, et il fera droit et justice dans le pays.
6 Katika siku zake Yuda ataokolewa, na Israeli wataishi kwa usalama. Na jina lake atakayeitwa Bwana ni haki yetu.
Dans ses jours, Juda sera sauvé, Israël habitera en assurance, et voici le nom dont on l’appellera: Yahweh-notre-justice.
7 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja-hili ndilo tamko la Bwana-hawatasema tena, 'Kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya Misri.'
C’est pourquoi voici que des jours viennent, — oracle de Yahweh, où l’on ne dira plus: « Yahweh est vivant, lui qui a fait monter les enfants d’Israël du pays d’Égypte, » —
8 Badala yake watasema, 'Kama Bwana aishivyo, ambaye aliwaleta na ambaye aliwaongoza wana wa nyumba ya Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote walizofukuzwa.' Nao watakaa katika nchi yao wenyewe.”
mais « Yahweh est vivant, lui qui a fait monter et fait revenir la race de la maison d’Israël du pays du septentrion et de tous les pays où je les avais chassés; » et ils habiteront sur leur sol.
9 Kuhusu manabii, moyo wangu umevunjika ndani yangu, na mifupa yangu yote imetetemeka. Nimekuwa kama mlevi, kama mtu ambaye ameshindwa na divai, kwa sababu ya Bwana na maneno yake matakatifu.
Aux prophètes. Mon cœur est brisé au-dedans de moi, tous mes os tremblent; je suis comme un homme ivre, comme un homme pris de vin, en présence de Yahweh et en présence de sa parole sainte,
10 Kwa maana nchi imejaa wazinzi. Kwa sababu ya hayo nchi imeuka. Milima katika jangwa imekauka. Njia hizi za manabii ni mbaya; nguvu zao hazitumiwi kwa namna sahihi.
Car le pays est rempli d’adultères; car, à cause de la malédiction, le pays est en deuil; les pâturages du désert sont desséchés. L’objet de leur course est le mal; leur force est l’injustice,
11 Kwa maana manabii na makuhani wote wamekufuru. Nimeona uovu wao ndani ya nyumba yangu! - hili ndilo tamko la Bwana;
Prophètes et prêtres eux-mêmes sont des profanes, et dans ma maison même j’ai trouvé leur méchanceté, — oracle de Yahweh.
12 kwa hiyo njia yao itakuwa kama mahali pa kupumzika katika giza. Watasukumwa chini. Wao wataanguka ndani yake. Kwa maana nitawatuma mabaya juu yao katika mwaka wa adhabu yao; hili ndilo tamko la Bwana.
Aussi leur chemin sera pour eux comme des lieux glissants dans les ténébres; ils seront poussés, ils y tomberont; car j’amènerai sur eux le malheur l’année où je les visiterai, — oracle de Yahweh.
13 kwa maana nimeona uchungu kati ya manabii huko Samaria. Walitabiri kwa Baali na wakawaongoza watu wangu Israeli kwenye njia sahihi.
Dans les prophètes de Samarie, j’ai vu de la sottise: ils prophétisaient par Baal, et ils égaraient mon peuple d’Israël;
14 Na miongoni mwa manabii huko Yerusalemu nimeona mambo ya kutisha: wanafanya uzinzi na huenda kwa udanganyifu. Wanaimarisha mikono ya waovu; hakuna mtu anarejea na kuacha uovu wake. Wote wamekuwa kama Sodoma kwangu na wenyeji wake kama Gomora!”
et dans les prophètes de Jérusalem, j’ai vu l’horreur: ils commettent l’adultère et marchent dans le mensonge; ils affermissent les mains des méchants, afin qu’aucun d’eux ne revienne de sa méchanceté. Ils sont tous pour moi comme Sodome, et les habitants de Jérusalem comme Gomorrhe.
15 Kwa hiyo, Bwana wa majeshi asema hivi juu ya manabii, “Tazameni, nitawafanya wale magugu na kunywa maji yenye sumu, kwa maana kufuru imetoka kwa manabii wa Yerusalemu na kuingia katika nchi yote.”
C’est pourquoi ainsi parle Yahweh des armées touchant les prophètes: Je vais leur faire manger de l’absinthe et leur faire boire des eaux empoisonnées! car c’est des prophètes de Jérusalem que la profanation est venue dans tout le pays.
16 Bwana wa majeshi asema hivi, “Usisikilize maneno ya manabii wanaokuhubiri. Wamekudanganya! Wanatangaza maono kutoka kwenye mawazo yao wenyewe, si kwa kinywa cha Bwana.
Ainsi parle Yahweh des armées: N’écoutez pas les paroles des prophètes qui vous prophétisent. Ils vous entraînent à la vanité, ils disent les visions de leur propre cœur, et non ce qui sort de la bouche de Yahweh.
17 Wanasema daima kwa wale wanaonidharau mimi, 'Bwana asema kutakuwa na amani kwako.' Na kila mtu anayetembea katika ukaidi wa moyo wake anasema, 'mabaya hayatakuja kwenu.'
Ils disent à ceux qui me méprisent: « Yahweh a dit: Vous aurez la paix; » et à tous ceux qui marchent dans la perversersité de leur cœur ils disent: « Il ne vous arrivera aucun mal. »
18 Lakini nani amesimama katika mkutano wa baraza la Bwana? Ni nani anayeona na kusikia neno lake? Ni nani anayezingatia maneno yake na kusikiliza?
Mais qui a assisté au conseil de Yahweh pour voir et entendre sa parole? Qui a été attentif à sa parole et l’a entendue?
19 Tazama, kuna dhoruba inayotoka kwa Bwana! Hasira yake inatoka, na dhoruba inazunguka. Inazunguka vichwa vya waovu.
Voici que la tempête de Yahweh, la fureur, va éclater; l’orage tourbillonne, il fond sur la tête des impies.
20 Hasira za Bwana hazitarejea mpaka zitakapotimiza nia ya moyo wake. Katika siku za mwisho, utaelewa.
La colère de Yahweh ne retournera pas en arrière qu’elle n’ait agi et réalisé les desseins de son cœur; à la fin des temps vous en aurez la pleine intelligence.
21 Sikuwatuma manabii hawa. Wao tu walionekana. Sikuwahubiri jambo lolote kwao, lakini bado wanatabiri.
Je n’ai pas envoyé ces prophètes, et ils courent! Je ne leur ai pas parlé, et ils prophétisent!
22 Kwa kuwa kama walisimama katika mkutano wangu wa baraza, wangeweza kuwasababisha watu wangu kusikia neno langu; wangewafanya wapate kuacha maneno yao mabaya na mazoea mabaya.
S’ils avaient assisté à mon conseil, ils auraient fait entendre mes paroles à mon peuple; ils les auraient ramenés de leur voie mauvaise, de la méchanceté de leurs actions.
23 Mimi ni Mungu aliye karibu-hili ni tamko la Bwana-mimi sio Mungu aliye mbali?
Ne suis-je un Dieu que de près, — oracle de Yahweh, et ne suis-je pas aussi un Dieu de loin?
24 Je, kuna mtu yeyote anayejificha mahali penye siri ili nisiweze kumwona? -Hili ndilo tamko la Bwana-Je mbingu na nchi hazikujawa nami? -hili Ndilo tamko la Bwana.
Un homme peut-il se cacher dans des cachettes sans que je le voie — oracle de Yahweh? Est-ce que le ciel et la terre je ne les remplis pas, moi — oracle de Yahweh?
25 Nimesikia yale waliyosema manabii, wale waliokuwa wanatabiri uongo kwa jina langu. Wakisema, 'Nilikuwa na ndoto!
J’ai entendu ce que disent ces prophètes qui prophétisent en mon nom des mensonges, en disant: « J’ai eu un songe; j’ai eu un songe! »
26 Nilikuwa na ndoto!' Je, hii itaendelea mpaka lini, manabii wanaotabiri uongo kutoka kwa akili zao, na wanasema nini kutokana na udanganyifu mioyoni mwao?
Jusques à quand?... Veulent-ils, ces prophètes, qui prophétisent le mensonge, ces prophètes de l’imposture de leur cœur,
27 Wana mpango wa kuwafanya watu wangu kusahau jina langu kwa ndoto ambazo wanazoripoti, kila mmoja kwa jirani yake, kama vile babu zao walivyosahau jina langu kwa ajili ya jina la Baali.
pensent-ils faire oublier mon nom à mon peuple, pour les rêves qu’ils se racontent les uns aux autres, comme leurs pères ont oublié mon nom pour Baal?
28 Nabii aliye na ndoto, aseme ndoto hiyo. Lakini yule ambaye nimemwambia kitu fulani, basi aseme neno langu kwa kweli. Je, majani yanahusiana na nafaka? - hili ni tamko la Bwana-
Que le prophète qui a eu un songe raconte ce songe; que celui qui a ma parole rapporte fidèlement ma parole. Qu’a de commun la paille avec le froment, — oracle de Yahweh?
29 Na neno langu si kama moto? -Hili ni tamko la Bwana-na kama mwamba wenye kupiga nyundo?
Ma parole n’est-elle pas comme un feu, — oracle de Yahweh, comme un marteau qui brise le roc?
30 Tazameni, ninapingana na nabii-hii ndiyo ahadi ya Bwana-yeyote anayeiba maneno kutoka kwa mtu mwingine na anasema yanatoka kwangu.
C’est pourquoi, voici que je viens à ces prophètes qui se dérobent mes paroles les uns aux autres.
31 Tazama, ninapingana na manabii-hili ndilo tamko la Bwana-ambao hutumia lugha zao kutabiri maneno.
Voici que je viens à ces prophètes, — oracle de Yahweh, qui agitent leur langue et qui disent: « Oracle de Yahweh! »
32 Tazameni, ninapingana na manabii wanaoota ndoto-hii ndiyo ahadi ya Bwana-na kisha kuwahubiri na kwa njia hii kuwadanganya watu wangu kwa udanganyifu wao na kujivunia. Mimi ni juu yao, kwa kuwa sikuwatuma wala kuwapa amri. Kwa hivyo hawatawasaidia watu hawa - hili ndilo tamko la Bwana.
Voici que je viens à ceux qui prophétisent des songes menteurs, — oracle de Yahweh, qui les racontent, qui égarent mon peuple par leurs mensonges et par leur extravagance. Je ne les ai pas envoyés, et je ne leur ai rien commandé; ils ne servent de rien à ce peuple; — oracle de Yahweh.
33 Watu hawa au nabii au kuhani wakakuuliza, 'Je, ni nini tamko la Bwana?' basi lazima uwaambie, 'Ni tamko gani? Kwa maana nimekuacha wewe-hili ndilo tamko la Bwana.
Quand ce peuple, ou des prophètes, ou un prêtre t’interrogent en ces termes: « Quel est le fardeau de Yahweh? » tu leur répondras: « C’est vous qui êtes le fardeau, et je vous rejetterai, » — oracle de Yahweh.
34 Kwa habari ya manabii, makuhani, na watu wanaosema, 'Hili ndilo tamko la Bwana,' nitamuadhibu mtu huyo na nyumba yake.
Et le prophète, le prêtre ou l’homme du peuple qui dira: « Fardeau de Yahweh, » je visiterai cet homme et sa maison.
35 Endelea kusema, kila mtu kwa jirani yake na kila mtu kwa ndugu yake, 'Bwana alijibu nini?' na 'Bwana alitangaza nini?'
Voici comment vous parlerez l’un à l’autre et chacun à son frère: « Qu’a répondu Yahweh? » et « Qu’a dit Yahweh? »
36 Lakini usizungumze tena juu ya tamko la Bwana, kwa kuwa kila tamko kutoka kwa kila mtu limekuwa ujumbe wake mwenyewe, na umepotosha maneno ya Mungu aliye hai, Bwana wa majeshi, Mungu wetu.
Mais vous ne répéterez plus: « Fardeau de Yahweh! » Car le fardeau de chacun sera sa parole, parce que vous tordez les paroles du Dieu vivant, de Yahweh des armées, notre Dieu.
37 Utamuuliza nabii hivi, 'Bwana alikujibu nini? Je, Bwana alisema nini? Kisha unasema tamko kutoka kwa Bwana;
Tu parleras ainsi au prophète: « Que t’a répondu Yahweh? qu’a dit Yahweh? »
38 lakini Bwana asema hivi, Sema hivi, “Hili ni tamko la Bwana” ingawa nimekuagiza na kusema, “Usiseme: Hili ni tamko kutoka kwa Bwana.”
Mais si vous dites: « Fardeau de Yahweh, » alors Yahweh parle ainsi: Parce que vous dites ce mot: « Fardeau de Yahweh, » après que j’ai envoyé vers vous pour vous dire: « Ne dites plus: Fardeau de Yahweh, »
39 Kwa hiyo, angalia, nitawachukua na kukutupa mbali na mimi, pamoja na jiji ambalo nilikupa wewe na baba zako.
à cause de cela, voici que je vous oublierai entièrement et que je vous rejetterai de devant ma face, vous et la ville que j’avais donnée à vous et à vos pères;
40 Ndipo nitaweka aibu ya milele na fedheha juu yenu ambayo haitasahauliwa.'”
et je ferai venir sur vous un opprobre éternel, une honte éternelle, qui ne s’oublieront jamais.

< Yeremia 23 >