< Yeremia 19 >

1 Bwana akasema hivi, “Nenda ukanunue chupa ya udongo wakati ukiwa na wazee wa watu na makuhani.
Thus said Jehovah, 'Go, and thou hast got a potter's earthen vessel, and of the elders of the people, and of the elders of the priests,
2 Kisha uende mpaka bonde la Ben Hinomu wakati wa kuingia kwenye mlango uliovunjika wa mfinyanzi, na huko utangaza maneno nitakayokuambia.
and thou hast gone forth unto the valley of the son of Hinnom, that [is] at the opening of the gate of the pottery, and hast proclaimed there the words that I speak unto thee,
3 Ukisema, 'Sikilizeni neno la Bwana, wafalme wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu! Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, “Tazameni, na nitaletea msiba juu ya mahali hapa, na masikio ya kila mtu anayesikia yatawaka.
and hast said, Hear a word of Jehovah, ye kings of Judah, and inhabitants of Jerusalem, Thus said Jehovah of Hosts, God of Israel: 'Lo, I am bringing in evil on this place, at which the ears of every one who is hearing it do tingle,
4 Nitafanya hivyo kwa sababu wameniacha na kudharau mahali hapa. Katika mahali hapa wanatoa sadaka kwa miungu mingine ambayo hawakuijua. Wao, baba zao, na wafalme wa Yuda pia wamejaza mahali damu isiyo na hatia.
because that they have forsaken Me, and make known this place, and make perfume in it to other gods, that they knew not, they and their fathers, and the kings of Judah, and they have filled this place [with] innocent blood,
5 Walimjengea Baali mahali pa juu na kuwachoma watoto wao kwa moto kama sadaka za kuteketezwa kwake-kitu ambacho sijawaamuru au kutaja, wala hakuingia ndani ya akili yangu.
and have built the high places of Baal to burn their sons with fire, burnt-offerings to Baal, that I commanded not, nor spake of, nor did it come up on My heart.
6 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja-hili ndilo tamko la Bwana-ambapo mahali hapa hapataitwa tena Tofethi, bonde la Ben Hinomu, kwa kuwa litakuwa bonde la machinjo.
'Therefore, lo, days are coming — an affirmation of Jehovah — and this place is not called any more, Tophet, and Valley of the son of Hinnom, but, Valley of slaughter.
7 Katika mahali hapa nitatamgua mipango ya Yuda na Yerusalemu. Nitawafanya wapate kuuawa kwa upanga mbele ya adui zao na kwa mkono wa wale wanaotafuta maisha yao. Ndipo nitawapa miili yao kuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa dunia.
And I have made void the counsel of Judah and Jerusalem in this place, and have caused them to fall by the sword before their enemies, and by the hand of those seeking their life, and I have given their carcase for food to the fowl of the heavens, and to the beast of the earth,
8 Ndipo nitaifanya mji huu kuwa uharibifu na kitu cha kuzomewa, kila mtu anayepita atashangaa na kuzomea kwa sababu mateso yake yote.
and I have made this city for a desolation, and for a hissing, every passer by it is astonished, and doth hiss for all its plagues.
9 Nitawafanya wale nyama ya wana wao na binti zao; kila mtu atakula mwili wa jirani yake katika dhiki na katika uchungu ambao umeletwa kwao na maadui zao na wale wanaotaka maisha yao.'”
And I have caused them to eat the flesh of their sons, and the flesh of their daughters, and each the flesh of his friend they do eat, in the siege and in the straitness with which straiten them do their enemies, and those seeking their life.
10 Kisha utavunja chupa ya udongo mbele ya watu ambao walikwenda pamoja nawe.
'And thou hast broken the bottle before the eyes of the men who are going with thee,
11 Uwaambie,'Bwana wa majeshi asema hivi: nitafanya jambo hili kwa watu hawa na mji huu- hii ndiyo ahadi ya Bwana, kama vile Yeremia alivyovunja chupa ya udongo ili isiweze kutengenezwa tena. Watu watazika wafu huko Tofethi hata hapatabaki mahali pa kuzika.
and hast said unto them: Thus said Jehovah of Hosts, Thus do I break this people and this city, as one breaketh the potter's vessel, that is not able to be repaired again, and in Tophet they bury — without place to bury;
12 Hivyo ndivyo nitakavyopafanya mahali hapa na wenyeji wake nitakapofanya jiji hili kama Tofethi, hili ndio tamko la Bwana;
so I do to this place — an affirmation of Jehovah — and to its inhabitants, so as to make this city as Tophet;
13 kwa hiyo nyumba za Yerusalemu na wafalme wa Yuda watakuwa kama Tofethi, nyumba zote zilizo juu ya watu waovu wanaoabudu nyota zote za mbinguni na kumwaga sadaka za kinywaji kwa miungu mingine.'”
and the houses of Jerusalem, and the houses of the kings of Judah, have been — as the place of Tophet — defiled, even all the houses on whose roofs they have made perfume to all the host of the heavens, so as to pour out oblations to other gods.'
14 Ndipo Yeremia akatoka Tofethi, ambako Bwana amemtuma ahubiri. Akasimama katika ua wa nyumba ya Bwana, akawaambia watu wote,
And Jeremiah cometh in from Tophet, whither Jehovah had sent him to prophesy, and he standeth in the court of the house of Jehovah, and he saith unto all the people:
15 “Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazameni, nitawaletea mji huu na miji yake yote maafa yote niliyonena dhidi yake, kwa kuwa walifanya shingo zao kuwa ngumu na kukataa kusikiliza maneno yangu.'”
'Thus said Jehovah of Hosts, God of Israel: Lo, I am bringing in unto this city, and on all its cities, all the evil that I have spoken against it, for they have hardened their neck — not to hear My words!'

< Yeremia 19 >