< Yeremia 14 >

1 Neno la Bwana lilimjia Yeremia kuhusu ukame,
The word of the LORD that came to Jeremiah concerning the droughts.
2 “Wayahudi waomboleze; basi milango yake ianguke. Wao wanaomboleza kwa ajili ya ardhi; Kilio chao kwa Yerusalemu kimepaa juu.
Judah mourneth, and the gates thereof languish, they bow down in black unto the ground; and the cry of Jerusalem is gone up.
3 Wenye nguvu huwatuma watumishi wao kwa ajili ya maji. Wanapoingia kwenye visima, hawawezi kupata maji. Wote wanarudi hawajafanikiwa; Wao hufunika vichwa vyao na aibu.
And their nobles send their lads for water: they come to the pits, and find no water; their vessels return empty; they are ashamed and confounded, and cover their heads.
4 Kwa sababu hii ardhi imepasuka, kwa maana hakuna mvua katika nchi. Wakulima huwa na aibu na kufunika vichwa vyao.
Because of the ground which is cracked, for there hath been no rain in the land, the plowmen are ashamed, they cover their heads.
5 Kwa maana hata kunguru huwaacha wanawe katika mashamba, kwa maana hakuna nyasi.
Yea, the hind also in the field calveth, and forsaketh her young, because there is no grass,
6 Punda mwitu husimama kwenye mabonde yaliyo wazi na hupiga upepo kama mbweha. Macho yao yanashindwa kufanya kazi, kwa maana hakuna mimea.
And the wild asses stand on the high hills, they gasp for air like jackals; their eyes fail, because there is no herbage.
7 Hata ingawa maovu yetu yanatushuhudia, Bwana, tenda kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu matendo yetu yasiyo na imani yamezidi; tumekutenda dhambi.
Though our iniquities testify against us, O LORD, work Thou for Thy name's sake; for our backslidings are many, we have sinned against Thee.
8 Matumaini ya Israeli, yule anayemwokoa wakati wa dhiki, kwa nini utakuwa kama mgeni katika nchi, kama mtu akaaye nchi ya kigeni ambaye hujinyoosha na kutumia hutumia usiku mmoja tu?
O Thou hope of Israel, the Saviour thereof in time of trouble, why shouldest Thou be as a stranger in the land, and as a wayfaring man that turneth aside to tarry for a night?
9 Kwa nini utakuwa kama mtu aliyechanganyikiwa, kama shujaa ambaye hawezi kuokoa mtu yeyote? Kwa maana wewe u katikati yetu, Bwana! Jina lako limetangazwa juu yetu. Usiondoke
Why shouldest thou be as a man overcome, as a mighty man that cannot save? Yet Thou, O LORD, art in the midst of us, and Thy name is called upon us; leave us not.
10 Bwana awaambia hivi watu hawa “Kwa kuwa wanapenda kutanga tanga, hawakuzuia miguu yao kufanya hivyo.” Bwana hafurahi nao. Sasa anawakumbusha uovu wao na ameadhibu dhambi zao.
Thus saith the LORD unto this people: Even so have they loved to wander, they have not refrained their feet; therefore the LORD doth not accept them, now will He remember their iniquity, and punish their sins.
11 Bwana akaniambia, Usiombe kwa ajili ya watu hawa.
And the LORD said unto me: 'Pray not for this people for their good.
12 Maana ikiwa wanafunga, sitasikiliza kulia kwao; na wanapotoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za unga, sitawafurahia. Kwa maana nitawaangamiza kwa upanga, njaa, na tauni.
When they fast, I will not hear their cry; and when they offer burnt-offering and meal-offering, I will not accept them; but I will consume them by the sword, and by the famine, and by the pestilence.'
13 Ndipo nikasema, “Ee Bwana, Bwana! Angalia! mabii wanawaambia watu, 'Huwezi kuona upanga; hakutakuwa na njaa kwako, kwa kuwa nitakupa usalama wa kweli mahali hapa.'”
Then said I: 'Ah, Lord GOD! behold, the prophets say unto them: Ye shall not see the sword, neither shall ye have famine; but I will give you assured peace in this place.'
14 Bwana akaniambia, 'manabii wanatabiri uongo kwa jina langu. Sikuwafukuza, wala sikuwapa amri au kusema nao. Lakini maono ya udanganyifu na ya maana, uchawi wa udanganyifu unaotokana na akili zao ndicho wanachowahubiria.”
Then the LORD said unto me: 'The prophets prophesy lies in My name; I sent them not, neither have I commanded them, neither spoke I unto them; they prophesy unto you a lying vision, and divination, and a thing of nought, and the deceit of their own heart.
15 Kwa hiyo Bwana asema hivi, “Kwa habari ya manabii wakihubiri kwa jina langu, ambao mimi siwakutuma; wale wanaosema kuwa hakutakuwa na upanga wala njaa katika nchi hii mabii hawa wataangamia kwa upanga na njaa.
Therefore thus saith the LORD: As for the prophets that prophesy in My name, and I sent them not, yet they say: Sword and famine shall not be in this land, by sword and famine shall those prophets be consumed;
16 Na watu waliopewa utabiri watafukuzwa nje ya barabara za Yerusalemu kwa sababu ya njaa na upanga; kwa kuwa hakuna mtu wa kuwazikas-wao, na wake zao, na wana wao, wala binti zao; kwa maana nitamwaga uovu wao wenyewe juu yao.
and the people to whom they prophesy shall be cast out in the streets of Jerusalem because of the famine and the sword; and they shall have none to bury them, them, their wives, nor their sons, nor their daughters; for I will pour their evil upon them.'
17 Sema neno hili kwao 'Acha macho yangu yatokwe machozi, usiku na mchana. wala yasikome, kwa kuwa kutakuwa na kuanguka kwa bikira, binti ya watu wangu - jeraha kubwa lisilotibika.
And thou shalt say this word unto them: Let mine eyes run down with tears night and day, and let them not cease; for the virgin daughter of my people is broken with a great breach, with a very grievous blow.
18 Ikiwa nitatoka kwenye shamba basi angalia! kuna wale waliouawa kwa upanga. Na kama nitakuja mjini, basi, tazama! kuna wale walio na ugonjwa wa njaa. Hata nabii na kuhani wote wanatembea juu ya nchi bila maarifa.'”
If I go forth into the field, then behold the slain with the sword! And if I enter into the city, then behold them that are sick with famine! For both the prophet and the priest are gone about to a land, and knew it not.
19 Je! Umemkataa kabisa Yuda? Je, unaichukia Sayuni? Kwa nini umetupiga wakati hakuna uponyaji kwetu? Tulitumaini amani, lakini hapakuwa na kitu kizuri-na kwa wakati wa uponyaji, lakini tazama, kuna hofu tu.
Hast Thou utterly rejected Judah? Hath Thy soul loathed Zion? Why hast Thou smitten us, and there is no healing for us? We looked for peace, but no good came; and for a time of healing, and behold terror!
20 Tunakubali, Bwana, makosa yetu, uovu wa babu zetu, kwa kuwa tumekukosea.
We acknowledge, O LORD, our wickedness, even the iniquity of our fathers; for we have sinned against Thee.
21 Usitukatae! Kwa ajili ya jina lako, usikifedheheshe kiti chako cha enzi cha utukufu. Kumbuka na usivunje agano lako na sisi.
Do not contemn us, for Thy name's sake, do not dishonour the throne of Thy glory; remember, break not Thy covenant with us.
22 Je, kuna miongoni mwa sanamu za mataifa yeyote zinazoweza kuifanya mbingu kutoa mvua? Je, si wewe, Bwana Mungu wetu, ambaye hufanya jambo hili? Tunatumaini kwako, kwa kuwa umefanya mambo haya yote.
Are there any among the vanities of the nations that can cause rain? or can the heavens give showers? Art not Thou He, O LORD our God, and do we not wait for Thee? For Thou hast made all these things.

< Yeremia 14 >