< Yeremia 13 >

1 Bwana aliniambia hivi, “Nenda ukape nguo ya kitani na kuiweka karibu na kiuno chako, lakini usiiweke kwenye maji kwanza.”
Thus he said Yahweh to me go and you will buy for yourself a loincloth of linen and you will put it on loins your and in water not you must cause to go it.
2 Kwa hiyo nilinunua vazi kama vile Bwana alivyoagiza, na nikafunga karibu na kiuno changu.
And I bought the loincloth according to [the] word of Yahweh and I put [it] on loins my.
3 Ndipo neno la Bwana likanijia mara ya pili, kusema,
And it came [the] word of Yahweh to me a second [time] saying.
4 “Twaa vazi lako ulilolinunua lililo karibu na kiuno chako, uinuke, ukasafiri mpaka Frati. Ukaifiche huko katika mwamba wa jabali.
Take the loincloth which you bought which [is] on loins your and arise go Perath towards and hide it there in [the] cleft of the rock.
5 Basi nikaenda na kuificha katika Frati kama vile Bwana alivyoniamuru.
And I went and I hid it at Perath just as he had commanded Yahweh me.
6 Baada ya siku nyingi, Bwana akaniambia, “Simama, urudi Frati. Ukaichukue nguo ambayo nilikuambia ufiche.”
And it was from [the] end of days many and he said Yahweh to me arise go Perath towards and take from there the loincloth which I commanded you to hide it there.
7 Kwa hiyo nikarudi Frati na kuchimba na kuchukua nguo mahali pale nilipoificha. Lakini tazama! Nguo hiyo ilikuwa imeharibika; haikuwa nzuri kabisa.
And I went Perath towards and I dug and I took the loincloth from the place where I had hidden it there and there! it was ruined the loincloth not it was profitable for anything.
8 Ndipo neno la Bwana likanijia tena, kusema,
And it came [the] word of Yahweh to me saying.
9 “Bwana asema hivi, Nitakiangamiza kiburi cha Yuda na Yerusalemu.
Thus he says Yahweh thus I will ruin [the] pride of Judah and [the] pride of Jerusalem great.
10 Watu hawa waovu wanaokataa kusikia neno langu, ambao huenda katika ugumu wa mioyo yao, ambao hufuata miungu mingine ili kuabudu na kuinama-watakuwa kama hii nguo isiyofaa kwa lolote.
The people this wicked who are refusing - to hear words my who walk in [the] stubbornness of own heart their and they have walked after gods other to serve them and to bow down to them and let it be like the loincloth this which not it is profitable for anything.
11 Kwa maana kama vile vazi lililofungwa kwenye viuno vya mtu, ndivyo nimefainya nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda zimefungwa kwangu- hili ndilo tamko la Bwana-wawe watu wangu, ili kunifanya jina, sifa, na heshima. Lakini hawakunisikiliza.
For just as it clings loincloth to [the] loins of a person so I have made cling to me all [the] house of Israel and all [the] house of Judah [the] utterance of Yahweh to become for me a people and a name and praise and honor and not they listened.
12 Basi uwaambie neno hili, 'Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi Kila chupa itajazwa divai.' Watakuambia, 'Je, hatujui kwamba kila chupa itajazwa divai?'
And you will speak to them the word this. Thus he says Yahweh [the] God of Israel every wineskin it will be filled wine and they will say to you ¿ really not do we know that every wineskin it will be filled wine.
13 Basi uwaambie,' Bwana asema hivi: Tazama, nitawajaza kila mkaaji wa nchi hii ulevi, na wafalme wanaokaa kiti cha Daudi, na makuhani, na manabii, na wenyeji wote wa Yerusalemu.
And you will say to them thus he says Yahweh here I [am] about to fill all [the] inhabitants of the land this and the kings who sit for David on throne his and the priests and the prophets and all [the] inhabitants of Jerusalem drunkenness.
14 Ndipo nitawagonganisha kila mtu na mwenzake baba na watoto wao pamoja; hili ndilo tamko la Bwana-sitawahurumia au kuwa na huruma, wala sitawarehemu kutoka kwenye uharibifu.
And I will smash them each to brother his and the parents and the children alike [the] utterance of Yahweh not I will show pity and not I will have mercy and not I will have compassion from destroying them.
15 Sikilizeni na makini. Msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amesema.
Hear and give ear may not you be haughty for Yahweh he has spoken.
16 Mtukuze Bwana, Mungu wako, kabla ya hajaleta giza, na kabla ya kuifanya miguu yako kuwa na mashaka juu ya milima wakati wa jioni. Kwa maana unatarajia mwanga, lakini ataugeuza kuwa mahali pa giza, na kuwa giza nene.
Give to Yahweh God your glory before he will bring darkness and before they will stumble feet your on mountains of twilight and you will wait for light and he will make it into deep darkness (and he will make [it] *QK) into thick darkness.
17 Kwa hiyo ikiwa husikilizi, nitaomboleza peke yangu kwa sababu ya kiburi chako. Hakika macho yangu yatalia na kutoa machozi, kwa sababu kundi la Bwana limechukuliwa mateka.
And if not you will listen to it in secret places it will weep self my because of pride and utterly it will weep and it may run down eye my tear[s] for it has been taken captive [the] flock of Yahweh.
18 “Mwambieni mfalme na mama wa malkia, 'Jinyenyekezeni, na kukaa chini, kwa maana taji juu ya kichwa chako, kiburi chako na utukufu wako, umeanguka.'
Say to the king and to the queen-mother make low sit for it has come down [the] place of head your [the] crown of splendor your.
19 Miji ya Negebu itafungwa, bila mtu wa kufungua. Yuda watachukuliwa mateka, wote uhamishoni.
[the] cities of The Negev they have been shut up and there not [is one who] opens it has been taken into exile Judah all of it it has been taken into exile completeness.
20 Inua macho yako na angalia wale wanaokuja kutoka kaskazini. Je, ni kundi gani alilokupa, kundi ambalo lilikuwa zuri sana kwako?
(Lift up *Qk) eyes your (and see *Qk) those [who] are coming from [the] north where? [is] the flock [which] it was given to you [the] sheep of beauty your.
21 Je, unasema nini wakati Mungu anawaweka wale ambao uliwafundisha kuwa marafiki? Je, huu si mwanzo wa maumivu ya utungu ambayo yatakuchukua kama mwanamke aliye katika kuzaa?
What? will you say that he will appoint over you and you you taught them over you close friends to chief ¿ not labor-pains will they seize you like a woman giving birth.
22 Kisha unaweza kusema moyoni mwako, 'Kwa nini mambo haya yanatokea kwangu?' Itakuwa kwa uovu wa maovu yako ambapo marinda yako yamefunuliwa na umeumizwa.
And if you will say in heart your why? have they happened to me these [things] in [the] greatness of iniquity your they have been uncovered skirts your they have suffered violence heels your.
23 Je, watu wa Kushi hubadilisha rangi yao ya ngozi, au chui hubadilisha madoa yake? Ikiwa ndivyo, basi wewe mwenyewe, ingawa unazoea uovu, utaweza kufanya mema.
¿ Will he change a Cushite skin his and a leopard spots its also you you will be able to do good O [those] trained to do evil.
24 Kwa hiyo nitawaangamiza kama makapi ambayo yanaangamia katika upepo wa jangwa.
And I will scatter them like chaff [which] passes away to [the] wind of [the] wilderness.
25 Hii ndiyo niliyokupa, sehemu ambayo nimekuagiza kwako-hili ndilo tamko la Bwana - kwa sababu umenisahau na kuamini katika udanganyifu.
This [is] lot your [the] portion of measure your from with me [the] utterance of Yahweh that you have forgotten me and you have trusted in falsehood.
26 Kwa hiyo mimi mwenyewe nitaondoa nguo zako, na sehemu zako za siri zitaonekana.
And also I I will strip off skirts your on face your and it will be visible shame your.
27 Uzinzi na ubembe wako, aibu ya tabia yako ya uasherati kwenye milima na katika mashamba! Nitayafanya yaonekane, mambo haya ya machukizo! Ole wako, Yerusalemu! Hutaki kuwa safi. Je! Hili litaendelea kwa muda gani?”
Adulteri your and neighings your [the] wickedness of prostitution your on hills in the field I have seen detestable things your woe! to you O Jerusalem not you are clean after when? yet.

< Yeremia 13 >