< Yeremia 13 >

1 Bwana aliniambia hivi, “Nenda ukape nguo ya kitani na kuiweka karibu na kiuno chako, lakini usiiweke kwenye maji kwanza.”
Thus said the LORD unto me, Go, and buy thee a linen girdle, and put it upon thy loins, and put it not in water.
2 Kwa hiyo nilinunua vazi kama vile Bwana alivyoagiza, na nikafunga karibu na kiuno changu.
So I bought a girdle according to the word of the LORD, and put it upon my loins.
3 Ndipo neno la Bwana likanijia mara ya pili, kusema,
And the word of the LORD came unto me the second time, saying,
4 “Twaa vazi lako ulilolinunua lililo karibu na kiuno chako, uinuke, ukasafiri mpaka Frati. Ukaifiche huko katika mwamba wa jabali.
Take the girdle that thou hast bought, which is upon thy loins, and arise, go to Euphrates, and hide it there in a hole of the rock.
5 Basi nikaenda na kuificha katika Frati kama vile Bwana alivyoniamuru.
So I went, and hid it by Euphrates, as the LORD commanded me.
6 Baada ya siku nyingi, Bwana akaniambia, “Simama, urudi Frati. Ukaichukue nguo ambayo nilikuambia ufiche.”
And it came to pass after many days, that the LORD said unto me, Arise, go to Euphrates, and take the girdle from thence, which I commanded thee to hide there.
7 Kwa hiyo nikarudi Frati na kuchimba na kuchukua nguo mahali pale nilipoificha. Lakini tazama! Nguo hiyo ilikuwa imeharibika; haikuwa nzuri kabisa.
Then I went to Euphrates, and digged, and took the girdle from the place where I had hid it: and, behold, the girdle was marred, it was profitable for nothing.
8 Ndipo neno la Bwana likanijia tena, kusema,
Then the word of the LORD came unto me, saying,
9 “Bwana asema hivi, Nitakiangamiza kiburi cha Yuda na Yerusalemu.
Thus saith the LORD, After this manner will I mar the pride of Judah, and the great pride of Jerusalem.
10 Watu hawa waovu wanaokataa kusikia neno langu, ambao huenda katika ugumu wa mioyo yao, ambao hufuata miungu mingine ili kuabudu na kuinama-watakuwa kama hii nguo isiyofaa kwa lolote.
This evil people, which refuse to hear my words, which walk in the stubbornness of their heart, and are gone after other gods to serve them, and to worship them, shall even be as this girdle, which is profitable for nothing.
11 Kwa maana kama vile vazi lililofungwa kwenye viuno vya mtu, ndivyo nimefainya nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda zimefungwa kwangu- hili ndilo tamko la Bwana-wawe watu wangu, ili kunifanya jina, sifa, na heshima. Lakini hawakunisikiliza.
For as the girdle cleaveth to the loins of a man, so have I caused to cleave unto me the whole house of Israel and the whole house of Judah, saith the LORD; that they might be unto me for a people, and for a name, and for a praise, and for a glory: but they would not hear.
12 Basi uwaambie neno hili, 'Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi Kila chupa itajazwa divai.' Watakuambia, 'Je, hatujui kwamba kila chupa itajazwa divai?'
Therefore thou shalt speak unto them this word: Thus saith the LORD, the God of Israel, Every bottle shall be filled with wine: and they shall say unto thee, Do we not know that every bottle shall be filled with wine?
13 Basi uwaambie,' Bwana asema hivi: Tazama, nitawajaza kila mkaaji wa nchi hii ulevi, na wafalme wanaokaa kiti cha Daudi, na makuhani, na manabii, na wenyeji wote wa Yerusalemu.
Then shalt thou say unto them, Thus saith the LORD, Behold, I will fill all the inhabitants of this land, even the kings that sit upon David’s throne, and the priests, and the prophets, and all the inhabitants of Jerusalem, with drunkenness.
14 Ndipo nitawagonganisha kila mtu na mwenzake baba na watoto wao pamoja; hili ndilo tamko la Bwana-sitawahurumia au kuwa na huruma, wala sitawarehemu kutoka kwenye uharibifu.
And I will dash them one against another, even the fathers and the sons together, saith the LORD: I will not pity, nor spare, nor have compassion, that I should not destroy them.
15 Sikilizeni na makini. Msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amesema.
Hear ye, and give ear; be not proud: for the LORD hath spoken.
16 Mtukuze Bwana, Mungu wako, kabla ya hajaleta giza, na kabla ya kuifanya miguu yako kuwa na mashaka juu ya milima wakati wa jioni. Kwa maana unatarajia mwanga, lakini ataugeuza kuwa mahali pa giza, na kuwa giza nene.
Give glory to the LORD your God, before he cause darkness, and before your feet stumble upon the dark mountains; and, while ye look for light, he turn it into the shadow of death, and make it gross darkness.
17 Kwa hiyo ikiwa husikilizi, nitaomboleza peke yangu kwa sababu ya kiburi chako. Hakika macho yangu yatalia na kutoa machozi, kwa sababu kundi la Bwana limechukuliwa mateka.
But if ye will not hear it, my soul shall weep in secret for [your] pride; and mine eye shall weep sore, and run down with tears, because the LORD’S flock is taken captive.
18 “Mwambieni mfalme na mama wa malkia, 'Jinyenyekezeni, na kukaa chini, kwa maana taji juu ya kichwa chako, kiburi chako na utukufu wako, umeanguka.'
Say thou unto the king and to the queen-mother, Humble yourselves, sit down: for your headtires are come down, even the crown of your glory.
19 Miji ya Negebu itafungwa, bila mtu wa kufungua. Yuda watachukuliwa mateka, wote uhamishoni.
The cities of the South are shut up, and there is none to open them: Judah is carried away captive all of it; it is wholly carried away captive.
20 Inua macho yako na angalia wale wanaokuja kutoka kaskazini. Je, ni kundi gani alilokupa, kundi ambalo lilikuwa zuri sana kwako?
Lift up your eyes, and behold them that come from the north: where is the flock that was given thee, thy beautiful flock?
21 Je, unasema nini wakati Mungu anawaweka wale ambao uliwafundisha kuwa marafiki? Je, huu si mwanzo wa maumivu ya utungu ambayo yatakuchukua kama mwanamke aliye katika kuzaa?
What wilt thou say, when he shall set [thy] friends over thee as head, seeing thou thyself hast instructed them against thee? shall not sorrows take hold of thee, as of a woman in travail?
22 Kisha unaweza kusema moyoni mwako, 'Kwa nini mambo haya yanatokea kwangu?' Itakuwa kwa uovu wa maovu yako ambapo marinda yako yamefunuliwa na umeumizwa.
And if thou say in thine heart, Wherefore are these things come upon me? for the greatness of thine iniquity are thy skirts discovered, and thy heels suffer violence.
23 Je, watu wa Kushi hubadilisha rangi yao ya ngozi, au chui hubadilisha madoa yake? Ikiwa ndivyo, basi wewe mwenyewe, ingawa unazoea uovu, utaweza kufanya mema.
Can the Ethiopian change his skin, or the leopard his spots? then may ye also do good, that are accustomed to do evil.
24 Kwa hiyo nitawaangamiza kama makapi ambayo yanaangamia katika upepo wa jangwa.
Therefore will I scatter them, as the stubble that passeth away, by the wind of the wilderness.
25 Hii ndiyo niliyokupa, sehemu ambayo nimekuagiza kwako-hili ndilo tamko la Bwana - kwa sababu umenisahau na kuamini katika udanganyifu.
This is thy lot, the portion measured unto thee from me, saith the LORD; because thou hast forgotten me, and trusted in falsehood.
26 Kwa hiyo mimi mwenyewe nitaondoa nguo zako, na sehemu zako za siri zitaonekana.
Therefore will I also discover thy skirts upon thy face, and thy shame shall appear.
27 Uzinzi na ubembe wako, aibu ya tabia yako ya uasherati kwenye milima na katika mashamba! Nitayafanya yaonekane, mambo haya ya machukizo! Ole wako, Yerusalemu! Hutaki kuwa safi. Je! Hili litaendelea kwa muda gani?”
I have seen thine abominations, even thine adulteries, and thy neighings, the lewdness of thy whoredom, on the hills in the field. Woe unto thee, O Jerusalem! thou wilt not be made clean; how long shall it yet be?

< Yeremia 13 >