< Yeremia 13 >

1 Bwana aliniambia hivi, “Nenda ukape nguo ya kitani na kuiweka karibu na kiuno chako, lakini usiiweke kwenye maji kwanza.”
This is what the Lord said to me: Go and get yourself a linen band and put it round you and do not put it in water.
2 Kwa hiyo nilinunua vazi kama vile Bwana alivyoagiza, na nikafunga karibu na kiuno changu.
So, as the Lord said, I got a band for a price and put it round my body.
3 Ndipo neno la Bwana likanijia mara ya pili, kusema,
And the word of the Lord came to me a second time, saying,
4 “Twaa vazi lako ulilolinunua lililo karibu na kiuno chako, uinuke, ukasafiri mpaka Frati. Ukaifiche huko katika mwamba wa jabali.
Take the band which you got for a price, which is round your body, and go to Parah and put it in a secret place there in a hole of the rock.
5 Basi nikaenda na kuificha katika Frati kama vile Bwana alivyoniamuru.
So I went and put it in a secret place by Parah, as the Lord had said to me.
6 Baada ya siku nyingi, Bwana akaniambia, “Simama, urudi Frati. Ukaichukue nguo ambayo nilikuambia ufiche.”
Then after a long time, the Lord said to me, Up! go to Parah and get the band which I gave you orders to put there.
7 Kwa hiyo nikarudi Frati na kuchimba na kuchukua nguo mahali pale nilipoificha. Lakini tazama! Nguo hiyo ilikuwa imeharibika; haikuwa nzuri kabisa.
So I went to Parah and, uncovering the hole, took the band from the place where I had put it away: and the band was damaged and of no use for anything.
8 Ndipo neno la Bwana likanijia tena, kusema,
Then the word of the Lord came to me, saying,
9 “Bwana asema hivi, Nitakiangamiza kiburi cha Yuda na Yerusalemu.
The Lord has said, In this way I will do damage to the pride of Judah and to the great pride of Jerusalem.
10 Watu hawa waovu wanaokataa kusikia neno langu, ambao huenda katika ugumu wa mioyo yao, ambao hufuata miungu mingine ili kuabudu na kuinama-watakuwa kama hii nguo isiyofaa kwa lolote.
These evil people who say they will not give ear to my words, who go on in the pride of their hearts and have become servants and worshippers of other gods, will become like this band which is of no use for anything.
11 Kwa maana kama vile vazi lililofungwa kwenye viuno vya mtu, ndivyo nimefainya nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda zimefungwa kwangu- hili ndilo tamko la Bwana-wawe watu wangu, ili kunifanya jina, sifa, na heshima. Lakini hawakunisikiliza.
For as a band goes tightly round a man's body, so I made all the people of Israel and all the people of Judah tightly united to me; so that they might be a people for me and a name and a praise and a glory: but they would not give ear.
12 Basi uwaambie neno hili, 'Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi Kila chupa itajazwa divai.' Watakuambia, 'Je, hatujui kwamba kila chupa itajazwa divai?'
So you are to say this word to them: This is the word of the Lord, the God of Israel: Every skin bottle will be full of wine; and they will say to you, Is it not quite clear to us that every skin bottle will be full of wine?
13 Basi uwaambie,' Bwana asema hivi: Tazama, nitawajaza kila mkaaji wa nchi hii ulevi, na wafalme wanaokaa kiti cha Daudi, na makuhani, na manabii, na wenyeji wote wa Yerusalemu.
Then you are to say to them, The Lord has said, I will make all the people of this land, even the kings seated on David's seat, and the priests and the prophets and all the people of Jerusalem, overcome with strong drink.
14 Ndipo nitawagonganisha kila mtu na mwenzake baba na watoto wao pamoja; hili ndilo tamko la Bwana-sitawahurumia au kuwa na huruma, wala sitawarehemu kutoka kwenye uharibifu.
I will have them smashed against one another, fathers and sons together, says the Lord: I will have no pity or mercy, I will have no feeling for them to keep me from giving them to destruction.
15 Sikilizeni na makini. Msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amesema.
Give ear and let your ears be open; be not lifted up: for these are the words of the Lord.
16 Mtukuze Bwana, Mungu wako, kabla ya hajaleta giza, na kabla ya kuifanya miguu yako kuwa na mashaka juu ya milima wakati wa jioni. Kwa maana unatarajia mwanga, lakini ataugeuza kuwa mahali pa giza, na kuwa giza nene.
Give glory to the Lord your God, before he makes it dark, and before your feet are slipping on the dark mountains, and, while you are looking for a light, he makes it into deep dark, into black night.
17 Kwa hiyo ikiwa husikilizi, nitaomboleza peke yangu kwa sababu ya kiburi chako. Hakika macho yangu yatalia na kutoa machozi, kwa sababu kundi la Bwana limechukuliwa mateka.
But if you do not give ear to it, my soul will be weeping in secret for your pride; my eye will be weeping bitterly, streaming with water, because the Lord's flock has been taken away as prisoners.
18 “Mwambieni mfalme na mama wa malkia, 'Jinyenyekezeni, na kukaa chini, kwa maana taji juu ya kichwa chako, kiburi chako na utukufu wako, umeanguka.'
Say to the king and to the queen-mother, Make yourselves low, be seated on the earth: for the crown of your glory has come down from your heads.
19 Miji ya Negebu itafungwa, bila mtu wa kufungua. Yuda watachukuliwa mateka, wote uhamishoni.
The towns of the south are shut up, and there is no one to make them open: Judah is taken away as prisoners; all Judah is taken away as prisoners.
20 Inua macho yako na angalia wale wanaokuja kutoka kaskazini. Je, ni kundi gani alilokupa, kundi ambalo lilikuwa zuri sana kwako?
Let your eyes be lifted up (O Jerusalem), and see those who are coming from the north. Where is the flock which was given to you, your beautiful flock?
21 Je, unasema nini wakati Mungu anawaweka wale ambao uliwafundisha kuwa marafiki? Je, huu si mwanzo wa maumivu ya utungu ambayo yatakuchukua kama mwanamke aliye katika kuzaa?
What will you say when he puts over you those whom you yourself have made your friends? will not pains take you like a woman in childbirth?
22 Kisha unaweza kusema moyoni mwako, 'Kwa nini mambo haya yanatokea kwangu?' Itakuwa kwa uovu wa maovu yako ambapo marinda yako yamefunuliwa na umeumizwa.
And if you say in your heart, Why have these things come on me? because of the number of your sins, your skirts have been uncovered and violent punishment overtakes you.
23 Je, watu wa Kushi hubadilisha rangi yao ya ngozi, au chui hubadilisha madoa yake? Ikiwa ndivyo, basi wewe mwenyewe, ingawa unazoea uovu, utaweza kufanya mema.
Is it possible for the skin of the Ethiopian to be changed, or the markings on the leopard? Then it might be possible for you to do good, who have been trained to do evil.
24 Kwa hiyo nitawaangamiza kama makapi ambayo yanaangamia katika upepo wa jangwa.
So I will send them in all directions, as dry grass is taken away by the wind of the waste land.
25 Hii ndiyo niliyokupa, sehemu ambayo nimekuagiza kwako-hili ndilo tamko la Bwana - kwa sababu umenisahau na kuamini katika udanganyifu.
This is your fate, the part measured out to you by me, says the Lord, because you have put me out of your memory and put your faith in what is false.
26 Kwa hiyo mimi mwenyewe nitaondoa nguo zako, na sehemu zako za siri zitaonekana.
So I will have your skirts uncovered before your face, in order that your shame may be seen.
27 Uzinzi na ubembe wako, aibu ya tabia yako ya uasherati kwenye milima na katika mashamba! Nitayafanya yaonekane, mambo haya ya machukizo! Ole wako, Yerusalemu! Hutaki kuwa safi. Je! Hili litaendelea kwa muda gani?”
I have seen your disgusting acts, even your false behaviour and your cries of desire and your loose ways on the hills in the field. Unhappy are you, O Jerusalem, you have no desire to be made clean; how long will you be in turning back to me?

< Yeremia 13 >