< Yeremia 11 >

1 Hili ndilo neno lililojia Yeremia kutoka kwa Bwana, akasema,
The word that came to Jeremiah from Jehovah, saying,
2 “Sikiliza maneno ya agano hili, uwaambie kila mtu wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu.
"Hear the words of this covenant, and speak to the men of Judah, and to the inhabitants of Jerusalem;
3 Uwaambie, 'Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi: na alaaniwe yeyote asiyesikiliza maneno ya agano hili.
and say to them, 'Thus says Jehovah, the God of Israel: "Cursed is the man who doesn't hear the words of this covenant,
4 Hili ndilo agano nililowaamuru baba zenu walishike siku nilipowatoa kutoka katika nchi ya Misri, kutoka tanuru ya chuma. Nikawaambia, “Sikilizeni sauti yangu na mfanye mambo yote kama nilivyowaamuru, kwa kuwa mtakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu.”
which I commanded your fathers in the day that I brought them forth out of the land of Egypt, out of the iron furnace, saying, "Obey my voice, and do them, according to all which I command you: so you shall be my people, and I will be your God;
5 Nisikilizeni ili nipate kukitimiza kiapo nilichoapa kwa baba zenu, kiapo kwamba nitawapa nchi iliyojaa maziwa na asali kama ilivyo leo.'” Kisha mimi Yeremia nikajibu na kusema, “Ndio, Bwana!”
that I may establish the oath which I swore to your fathers, to give them a land flowing with milk and honey," as at this day.'" Then I answered, and said, "Amen, Jehovah."
6 Bwana akaniambia, “Hubiri habari hizi yote katika miji ya Yuda, na katika njia za Yerusalemu. Sema, “Sikilizeni maneno ya agano hili na mkayafanye.
Jehovah said to me, "Proclaim all these words in the cities of Judah, and in the streets of Jerusalem, saying, 'Hear the words of this covenant, and do them.
7 Kwa maana nimewaagiza wazee wenu tangu siku ile niliyowaleta kutoka nchi ya Misri hadi wakati huu wa sasa, nimewaonya mara kwa mara na kusema, “Sikilizeni sauti yangu.'”
For I earnestly protested to your fathers in the day that I brought them up out of the land of Egypt, even to this day, rising early and protesting, saying, Obey my voice.
8 Lakini hawakusikiliza au wala kutega masikio yao. Kila mtu amekuwa akitembea katika ukaidi wa moyo wake mbaya. Kwa hiyo nilileta laana zote katika agano hili nililoamuru kuja juu yao. Lakini watu bado hawakuitii.”
Yet they did not obey, nor turn their ear, but walked everyone in the stubbornness of their evil heart: therefore I brought on them all the words of this covenant, which I commanded them to do, but they did not do them.'"
9 Kisha Bwana akaniambia, “Njama imeonekana kati ya watu wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu.
Jehovah said to me, "A conspiracy is found among the men of Judah, and among the inhabitants of Jerusalem.
10 Wameugeukia uovu wa mababu zao wa mwanzo, ambao walikataa kusikiliza neno langu, ambao badala yake walifuata miungu mingine ili kuabudu. Waisraeli na nyumba ya Yuda walivunja agano langu nililoweka na baba zao.
They are turned back to the iniquities of their forefathers, who refused to hear my words; and they are gone after other gods to serve them: the house of Israel and the house of Judah have broken my covenant which I made with their fathers.
11 Kwa hiyo Bwana asema hivi, 'Tazameni, nitawaletea majanga juu yao, majanga ambayo hawataweza kuyaepuka. Ndipo wataniita, lakini sitawasikiliza.
Therefore thus says Jehovah, 'Look, I will bring disaster on them, which they shall not be able to escape; and they shall cry to me, but I will not listen to them.
12 Miji ya Yuda na wenyeji wa Yerusalemu watakwenda na kuiita miungu ambayo walitoa sadaka, lakini hakika hawatawaokoa wakati wa majanga yao.
Then shall the cities of Judah and the inhabitants of Jerusalem go and cry to the gods to which they offer incense: but they will not save them at all in the time of their trouble.
13 Kwa kuwa idadi ya miungu yako ewe Yuda imeongezeka sawa na idadi ya miji yako. Na umefanya idadi ya madhabahu ya aibu huko Yerusalemu, madhabahu ya kufukiza uvumba kwa Baali, sawa na idadi ya njia zake.
For according to the number of your cities are your gods, Judah; and according to the number of the streets of Jerusalem have you set up altars to the shameful thing, even altars to burn incense to Baal.'
14 Kwa hiyo wewe mwenyewe, Yeremia, usiwaombee watu hawa. Lazima usiomboleze au kuomba kwa niaba yao. Kwa maana siwezi kusikiliza wakati wananiita katika majanga yao.
Therefore do not pray for this people, neither lift up cry nor prayer for them; for I will not hear them in the time that they cry to me at the time of their trouble."
15 Mpendwa wangu anafanya nini nyumbani kwangu, ikiwa amekuwa na nia mbaya? Nyama za sadaka yako hazitakusaidia. Unafurahi kwa sababu ya matendo yako mabaya.
"What has my beloved to do in my house, since she has done many vile deeds? Can holy meat avert your disaster so that you can rejoice?"
16 Katika siku za nyuma Bwana alikuita mti wa mzeituni wenye majani, mzuri wenye matunda mazuri. Lakini atawasha moto juu yake ambayo itaonekana kama sauti ya dhoruba; matawi yake yatavunjika.
Jehovah called your name, "A green olive tree, beautiful with goodly fruit." With the noise of a great tumult he has kindled fire on it, and its branches are broken.
17 Kwa maana Bwana wa majeshi, aliyekua amekusudia maafa juu yako, kwa sababu ya matendo mabaya ambayo nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda wamefanya-wamenikasirisha kwa kumtolea Baali sadaka.'”
For Jehovah of hosts, who planted you, has pronounced evil against you, because of the evil of the house of Israel and of the house of Judah, which they have worked for themselves in provoking me to anger by offering incense to Baal."
18 Bwana alinijulisha mambo haya, kwa hiyo nakayajua. Wewe, Bwana, umenifanya nione matendo yao.
Jehovah gave me knowledge of it, and I knew it: then you showed me their doings.
19 Nilikuwa kama kondoo mpole unayeongozwa na mchinjaji. Sikujua kwamba walikuwa wameunda mipango dhidi yangu, “Hebu tuangamize mti na matunda yake! Hebu tumkatilie mbali na nchi ya walio hai ili jina lake lisikumbukwe tena.
But I was like a gentle lamb that is led to the slaughter; and I did not know that they had devised devices against me, saying, "Let us destroy the tree with its fruit, and let us cut him off from the land of the living, that his name may be no more remembered."
20 Lakini Bwana wa majeshi ndiye mwamuzi mwenye haki ambaye huchunguza moyo na akili. Mimi nitashuhudia kisasi chako dhidi yao, kwa kuwa nimekuletea kesi yangu kwako.
"But, Jehovah of hosts, who judges righteously, who tests the heart and the mind, I shall see your vengeance on them; for to you have I revealed my cause."
21 Kwa hiyo Bwana asema hivi juu ya watu wa Anathothi, wanaotafuta uhai wako, “wanasema, 'Usifanye unabii kwa jina la Bwana, usije utakufa kwa mkono wetu.'
Therefore thus says Jehovah concerning the men of Anathoth, who seek my life, saying, "You shall not prophesy in the name of Jehovah, that you not die by our hand;"
22 Kwa hiyo Bwana wa majeshi asema hivi, 'Tazameni, nitawaadhibu. Vijana wao wenye nguvu watakufa kwa upanga. Wana wao na binti zao watakufa kwa njaa.
therefore thus says Jehovah of hosts, "Look, I will punish them: the young men shall die by the sword; their sons and their daughters shall die by famine;
23 Hakuna hata mmoja atakayeachwa, kwa maana nitaleta maafa dhidi ya watu wa Anathothi, mwaka wa adhabu yao.'”
and there shall be no remnant to them: for I will bring disaster on the men of Anathoth, even the year of their visitation."

< Yeremia 11 >