< Yakobo 1 >

1 Yakobo, mtumwa wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo, kwa makabila kumi na mbili yaliyotawanyika, salaam.
Jakub, sługa Boga i Pana Jezusa Chrystusa, [przesyła] pozdrowienia dwunastu pokoleniom, które są w rozproszeniu.
2 Hesabuni kuwa ni furaha zaidi, ndugu zangu, mnapopita katika matatizo mbali mbali,
Poczytujcie to sobie za największą radość, moi bracia, gdy rozmaite próby przechodzicie;
3 mkijua kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huwapa uvumilivu.
Wiedząc, że doświadczenie waszej wiary wyrabia cierpliwość.
4 Acheni uvumilivu uikamilishe kazi yake, kwamba muweze kukomaa kikamilifu, bila kupungukiwa katika lolote.
Cierpliwość zaś niech dopełni swego dzieła, abyście byli doskonali i zupełni, niemający żadnych braków.
5 Lakini kama mtu kati yenu anahitaji hekima, aiombe kutoka kwa Mungu, ambaye hutoa kwa ukarimu na pasipo kukemea kwa wote wamwombao, na atawapa hekima.
A jeśli komuś z was brakuje mądrości, niech prosi Boga, który daje wszystkim obficie i bez wypominania, a będzie mu dana.
6 Lakini omba kwa imani, bila shaka, kwa kuwa mwenye kutia shaka ni kama mawimbi katika bahari, huchukuliwa na upepo na kutupwa huku na huko.
Ale niech prosi z wiarą, bez powątpiewania. Kto bowiem wątpi, podobny jest do fali morskiej pędzonej przez wiatr i miotanej [tu i tam].
7 Kwa hakika mtu huyu asifikirie kwamba atapokelewa ombi lake kutoka kwa Bwana;
Człowiek taki niech nie myśli, że coś otrzyma od Pana.
8 mtu huyu ana nia mbili, si imara katika njia zake zote.
Człowiek umysłu dwoistego [jest] niestały we wszystkich swoich drogach.
9 Ndugu maskini anapaswa kujivuna katika kusimama kwake juu,
Niech ubogi brat chlubi się ze swojego wywyższenia;
10 wakati huo huo ndugu tajiri katika unyenyekevu wake, kwa sababu atatoweka kama ua la kondeni katika shamba analopita.
A bogaty ze swego poniżenia, bo przeminie jak kwiat trawy.
11 Jua huchomoza na joto la kuunguza kukausha mimea, na maua huanguka na uzuri wake hufa. Vivyo hivyo watu matajiri watachakaa katikati ya kazi zao.
[Jak] bowiem wzeszło palące słońce, wysuszyło trawę, a kwiat jej opadł i zginęło piękno jego wyglądu, tak też bogaty zmarnieje na swoich drogach.
12 Amebarikiwa mtu yule anayevumilia majaribu, kwa kuwa baada ya kushinda jaribu hilo, atapokea taji ya uzima, ambayo imeahidiwa kwa wale wampendao Mungu.
Błogosławiony człowiek, który znosi próbę, bo gdy zostanie wypróbowany, otrzyma koronę życia, którą obiecał Pan tym, którzy go miłują.
13 Mtu yeyote hapaswi kusema anapojaribiwa, “Jaribu hili linatoka kwa Mungu,” kwa sababu Mungu hajaribiwi na uovu, na Mungu mwenyewe hamjaribu yeyote.
Niech nikt, gdy jest kuszony, nie mówi: Jestem kuszony przez Boga. Bóg bowiem nie może być kuszony do złego ani sam nikogo nie kusi.
14 Kila mtu hujaribiwa na tamaa zake mbaya zinazomshawishi na kumvuta mbali.
Lecz każdy jest kuszony przez własną pożądliwość, która go pociąga i nęci.
15 Ndipo baada ya tamaa ya dhambi kubeba mimba, dhambi huzaliwa, na baada ya dhambi kukomaa sawasawa, huishia katika mauti.
Następnie pożądliwość, gdy pocznie, rodzi grzech, a grzech, gdy będzie wykonany, rodzi śmierć.
16 Ndugu zangu wapendwa, msidanganyike.
Nie błądźcie, moi umiłowani bracia!
17 Kila zawadi iliyo nzuri na kila zawadi iliyokamilika hutoka juu, hushuka chini kutoka kwa Baba wa nuru. Kamwe habadiliki kama kivuli kibadilikavyo.
Wszelki dar dobry i wszelki dar doskonały pochodzi z góry i zstępuje od Ojca światłości, u którego nie ma zmiany ani cienia zmienności.
18 Mungu alichagua kutupa sisi uzima kwa Neno la kweli, ili kwamba tuweze kuwa kama uzao wa kwanza miongoni mwa viumbe vyake.
Ze swojej woli zrodził nas słowem prawdy, abyśmy byli jakby pierwocinami jego stworzeń.
19 Mnajua hili, ndugu zangu wapendwa. Kila mmoja anapaswa kuwa mwepesi wa kusikia, siyo mwepesi wa kuongea wala kukasirika,
Tak więc, moi umiłowani bracia, niech każdy człowiek będzie skory do słuchania, nieskory do mówienia [i] nieskory do gniewu.
20 kwa kuwa hasira ya mwanadamu haiwezi kutenda haki ya Mungu.
Gniew bowiem człowieka nie wykonuje sprawiedliwości Bożej.
21 Kwa hiyo wekeni mbali uchafu wa dhambi na ubaya wote ulio mahali popote, na kwa unyenyekevu lipokeeni neno lililopandwa ndani yenu, ambalo lina uwezo wa kuokoa roho zenu.
Odrzućcie więc wszelką plugawość oraz bezmiar zła i z łagodnością przyjmijcie zaszczepione [w was] słowo, które może zbawić wasze dusze.
22 Litiini neno, msilisikie tu, mkijidanganya nafsi zenu wenyewe.
Bądźcie więc wykonawcami słowa, a nie tylko słuchaczami, oszukującymi samych siebie.
23 Kwa kuwa kama yeyote alisikiaye neno bila kulitendea kazi ni sawa na mtu ajiangaliaye uso wake halisi katika kioo.
Jeśli bowiem ktoś jest słuchaczem słowa, a nie wykonawcą, podobny jest do człowieka, który przygląda się w lustrze swemu naturalnemu obliczu.
24 Hujitathimini uso wake, na huenda zake na baada ya muda mfupi husahau anavyofanana.
Bo przyjrzał się sobie, odszedł i zaraz zapomniał, jakim był.
25 Bali mtu yule anayeiangalia kwa uangalifu sheria kamili, sheria ya uhuru, na kuendelea kuitii, si kwa sababu yeye ni msikilizaji anayesahau, huyu mtu atabarikiwa anapoitenda.
Lecz kto wpatruje się w doskonałe prawo wolności i trwa [w nim], nie jest słuchaczem, który zapomina, lecz wykonawcą dzieła, ten będzie błogosławiony w swoim działaniu.
26 Ikiwa mtu yeyote atafikiri mwenyewe kuwa ni mtu wa dini, lakini hawezi kuutawala ulimi wake, huudanganya moyo wake na dini yake ni bure.
Jeśli ktoś wśród was sądzi, że jest pobożny, a nie powściąga swego języka, lecz oszukuje swe serce, tego pobożność jest próżna.
27 Dini iliyo safi na isiyoharibiwa mbele za Mungu wetu na Baba ni hii: kuwasaidia yatima na wajane katika mateso yao, na kujilinda wenyewe na ufisadi wa dunia.
Czysta i nieskalana pobożność u Boga i Ojca polega na tym, aby przychodzić z pomocą sierotom i wdowom w ich utrapieniu [i] zachować samego siebie nieskażonym przez świat.

< Yakobo 1 >