< Isaya 61 >

1 Roho ya Bwana Yahwe i juu yangu, maana Yahwe amenipaka mafuta mimi kuhiubiri habari njema kwa wenye taabu. Amenituma mimi kuwaponywa waliopondeka mioyo, kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kufungua gereza ili waliofungwa waweze kutoka.
The spirit of the Lord GOD is upon me; because the LORD hath anointed me to bring good tidings unto the humble; He hath sent me to bind up the broken-hearted, to proclaim liberty to the captives, and the opening of the eyes to them that are bound;
2 Amenituma mimi kuutangaza mwaka wa Yahwe uliokubalika, siku ya kisasi cha Mungu wetu, na kuwafariji wale wote wanaomboleza.
To proclaim the year of the LORD'S good pleasure, and the day of vengeance of our God; to comfort all that mourn;
3 Amenituma mimi - kuwapa wale waoombolezao katika Sayuni -kuwapa wao kilemba cha majivu, mafuta ya furaha badala ya kuomboleza, vazi la kusifu katika eneo la roho ya ubutu, kuwaita mialoni ya haki, iliyooteshwa na Yahwe, ili aweze kutukuzwa.
To appoint unto them that mourn in Zion, to give unto them a garland for ashes, the oil of joy for mourning, the mantle of praise for the spirit of heaviness; that they might be called terebinths of righteousness, the planting of the LORD, wherein He might glory.
4 Wataijenga tena mahali pa kale palipohaibiwa; wataparejesha mahali palipokuwa na ukiwa. Watairejesha miji iliyoharibiwa, Mahali penye ukiwa kutoka vizazi vingi vilivyopita.
And they shall build the old wastes, they shall raise up the former desolations, and they shall renew the waste cities, the desolations of many generations.
5 Wageni watasimama na kulisha makumdi yako, na watoto wa wageni watafanya kazi kwenye mashamba yako na mizabu.
And strangers shall stand and feed your flocks, and aliens shall be your plowmen and your vinedressers.
6 Mtaitwa makuhani wa Yahwe; watawaita watumishi wa Mungu wetu. Mtakula utajiri wa mataifa, na utajivuinia katika utajiri wake.
But ye shall be named the priests of the LORD, men shall call you the ministers of our God; ye shall eat the wealth of the nations, and in their splendour shall ye revel.
7 Badala yake aibu yenu itaongezeka; na badala ya fedhea walifurahia juu ya sehemu yao. Hivyo basi sehemu yao itaongezeka mara mbili katika nchi na furaha ya milele itakuwa yao.
For your shame which was double, and for that they rejoiced: 'Confusion is their portion'; therefore in their land they shall possess double, everlasting joy shall be unto them.
8 Maana Mimi, Yahwe, ninapenda haki, na ninachukia wizi na vurugu zisizo za haki. Nitawalipa wao kataka haki na Nitafanya agano la milele na wao.
For I the LORD love justice, I hate robbery with iniquity; and I will give them their recompense in truth, and I will make an everlasting covenant with them.
9 Uzao wao utajulikana miongoni mwa mataifa, na watoto wao miongoni mwa watu. Wote watakaowaona watawakubali wao, kwamba ni watu wangu ambao Yahwe amewabariki.
And their seed shall be known among the nations, and their offspring among the peoples; all that see them shall acknowledge them, that they are the seed which the LORD hath blessed.
10 Nitafurahia sana katika Yahwe; Katika Mungu nitafurahia. Maana amenivika mimi kwa vazi la wokovu; amenivika mimi kwa vazi la haki, kama bwana harusi aliyejipamba mwenywe kwa kilemba, na kama bibi harusi aliyejipamba kwa vito.
I will greatly rejoice in the LORD, my soul shall be joyful in my God; for He hath clothed me with the garments of salvation, He hath covered me with the robe of victory, as a bridegroom putteth on a priestly diadem, and as a bride adorneth herself with her jewels.
11 Maana kama nchi inavyozalisha miti inayochipukia na kama bustani inavyofanya miti yake ikuie, hivyo Bwana atasasbabisha haki na sifa kuchipukia mbele ya mataifa yote.
For as the earth bringeth forth her growth, and as the garden causeth the things that are sown in it to spring forth; so the Lord GOD will cause victory and glory to spring forth before all the nations.

< Isaya 61 >