< Isaya 60 >

1 Nyanyuka, uangaze; maana mwanga wako umekuja, na utukufu wa Yahwe umekuja kwako.
Arise, be bright, for come hath thy light, And the honour of Jehovah hath risen on thee.
2 Japokuwa giza litatanda katika nchi, na giza nene katika mataifa; Lakini Yahwe atakuja juu yenu, na utukufu wake utaonekana kwenu.
For, lo, the darkness doth cover the earth, And thick darkness the peoples, And on thee rise doth Jehovah, And His honour on thee is seen.
3 Mataifa yatakuja kwenye mwanga wako, na wafalme katika mwanga wako mkali uliokuja
And come have nations to thy light, And kings to the brightness of thy rising.
4 Tazama na angalia pande zote. Wamekusanyika wao wenyewe kwa pamoja na wanakuja kwako. Watoto wako watatoka mbali, na binti zao watabebwa katika mikono yenu.
Lift up round about thine eyes and see, All of them have been gathered, they have come to thee, Thy sons from afar do come, And thy daughters on the side are supported.
5 Halafu wataangalia na kuwa furaha, na moyo wako utafurahia na kufurika, maana wingi wa maji utamwagwa juu yenu, utajiri wa mataifa utakuja kwenu.
Then thou seest, and hast become bright, And thine heart hath been afraid and enlarged, For turn unto thee doth the multitude of the sea, The forces of nations do come to thee.
6 Msafara wa ngamia utawafunika ninyi, na ngamia wa Midiani na Efa; wote watakuja kutoka Sheba; wataleta dhahabu na ubani, wataimba sifa kwa Yahwe.
A company of camels covereth thee, Dromedaries of Midian and Ephah, All of them from Sheba do come, Gold and frankincense they bear, And of the praises of Jehovah they proclaim the tidings.
7 Makundi yote ya Kedari yatakusanika kwa pamoja kwako, kondoo wa Nebaioti watabeba mahitaji yako; watakubalika kutolewa sadaka katika madhebau yangu; na nitaitukuza nyumba yangu takatifu.
All the flock of Kedar are gathered to thee, The rams of Nebaioth do serve thee, They ascend for acceptance Mine altar, And the house of My beauty I beautify.
8 Ni nani hawa wanopaa wenyewe kama mawingu, na kama njiwa kwenye makazi yao?
Who [are] these — as a thick cloud they fly, And as doves unto their windows?
9 Pwani itanitafuta mimi, na meli ya Tarshishi huwaongoza, huwaleta watoto wenu kutoka mbali, pamoja na fedha zao na dhahabu zao, maana jina la Yahwe Mungu wenu, na Mtakatifu wa Israeli, maana amekuheshimu wewe.
Surely for Me isles do wait, And ships of Tarshish first, To bring thy sons from afar, Their silver and their gold with them, To the name of Jehovah thy God, And to the Holy One of Israel, Because He hath beautified thee.
10 Watoto wa wageni watajenga tena kuta zenu, n awafalme wao watawatumikia ninyi; japo katika laana yangu nimewaadhibu ninyi, lakini kwa neema yangu nitawahurumia ninyi.
And sons of a stranger have built thy walls, And their kings do serve thee, For in My wrath I have smitten thee, And in My good pleasure I have pitied thee.
11 Milango yenu itaendelea kuwa wazi; haitafungwa mchana au usiku, hivyo utajiri wa mataifa ili uweze kuletwa, pamoja na viongozi wanowaongoza.
And opened have thy gates continually, By day and by night they are not shut, To bring unto thee the force of nations, Even their kings are led.
12 Kweli, mataifa na falme ambayo hayatakutumikia wewe yatatoweka; mataifa hayo yataangamizwa kabisa.
For the nation and the kingdom that do not serve thee perish, Yea, the nations are utterly wasted.
13 Utukufu wa Lebanoni utakuja kwako, mti wa msonobari, mtidhari, pamoja na msonobari ili kupamba madhebau yangu; na Nitalitukuza eneo la miguu yangu.
The honour of Lebanon unto thee doth come, Fir, pine, and box together, To beautify the place of My sanctuary, And the place of My feet I make honourable.
14 Watakuja kwako kukusujudia wewe, watoto wa wale wanaokunyenyekea wewe; wataisujudia miguu yako; watakuita wewe mji wa Yahwe, sayani ya Mtakatifu wa Israeli.
And come unto thee, bowing down, Have sons of those afflicting thee, And bowed themselves to the soles of thy feet Have all despising thee, And they have cried to thee: 'City of Jehovah, Zion of the Holy One of Israel.'
15 Badala yake uwepo wenu umetelekezwa na kuchukiwa, kwa kuwa hakuna hata mmoja anayepita ndani yenu, nitawafanya kuwa kitu cha kiburi milele, furaha kutoka kizazi hata kizazi.
Instead of thy being forsaken and hated, And none passing through, I have made thee for an excellency age-during, A joy of generation and generation.
16 Pia utakunywa maziwa ya mataifa, utatunzwa katika kifua cha wafalme; utajua kwamba Mimi Yahwe, Mimi ni mwokozi na mkombozi wenu, aliye Mkuu wa Israeli.
And thou hast sucked the milk of nations, Yea, the breast of kings thou suckest, And thou hast known that I, Jehovah, Thy Saviour, and Thy Redeemer, [Am] the Mighty One of Jacob.
17 Badala ya shaba Nitaleta dhahabu, badaia ya chuma nitaleta fedha; badala ya mbao, shabana badala ya jiwe, chuma. Nitachagua amani kwa kiongozi wenu, na haki kiongozi wenu.
Instead of the brass I bring in gold, And instead of the iron I bring in silver, And instead of the wood brass, And instead of the stone iron, And I have made thy inspection peace, And thy exactors righteousness.
18 Vurugu hazitasikika katika aridhi yenu, uharibifu wala uvunjaji katika mipaka yenu; lakini mtaita kuta zenu wokovu, na malngo yenu mtayaita sifa.
Violence is not heard any more in thy land, Spoiling and destruction in thy borders, And thou hast called 'Salvation' thy walls, And thy gates, 'Praise.'
19 Jua halitakuwa mwanga wenu wakati wa mchana, wala mwanga wa mwenzi wakati wa usiku hautawawakia ninyi; Lakini Yahwe atakuwa mwanga wenu wa milele, na Mungu wenu na utukufu wenu.
To thee no more is the sun for a light by day, And for brightness the moon giveth not light to thee, And Jehovah hath become to thee A light age-during, and thy God thy beauty.
20 Jua lenu halitakuewepo wala mweni utaondoshwa na kutoweka; maana Yahwe atakuwa mwanga wenu daima, na siku za maombolezo zitakwisha.
Thy sun goeth no more in, And thy moon is not removed, For Jehovah becometh to thee a light age-during. And the days of thy mourning have been completed.
21 Watu wako wote watakuwa wenye haki; watachukuwa urithi wa nchi kwa mda wote, tawi la mazao yangu, kazi ya mikono yangu, ili niweze kuitukuza.
And thy people [are] all of them righteous, To the age they possess the earth, A branch of My planting, A work of My hands, to be beautified.
22 Mtoto atakuwa maelfu, na mdogo atakuwa taifa la wenye nguvu; Mimi Yahwe Nitayatimiza hayo mda utakapowadia.
The little one doth become a chief, And the small one a mighty nation, I, Jehovah, in its own time do hasten it!

< Isaya 60 >