< Isaya 48 >

1 Sikiliza hili, nyumba ya Jakobo, mlioitwa kwa jina la Israeli, na mmetoka katika mbegu ya Yuda; yeye akirie kwa jina la Yahwe na kumuhusisha Mungu wa Israeli, lakini sio kweli wala kwa namna ya haki.
Hear this, house of Jacob, who are called by the name Israel, and have come from the sperm of Judah; you who swear by the name of Yahweh and invoke the God of Israel, but not sincerely nor in a righteous manner.
2 Maana wanajiita wenyewewatu wa mji mtakatifu na kumuamini Mungu wa Israeli; Yahwe wa majeshi ndilo jina lake.
For they call themselves people of the holy city and trust in the God of Israel. Yahweh of hosts is his name.
3 ''Nimetangaza vitu kutoka siku nyingi; Wamekuja nje kutoka mdomoni mwangu, na nimewafanya wajulikane; halafu gafla nimewafanyia, na yakatimia.
“I have declared the things from long ago; they came out from my mouth, and I made them known; then suddenly I did them, and they came to pass.
4 Kwa sababu nilijua kwamba wewe ni mkaiidi, misuli ya shingo yako ni kama ya chuma, na paji la uso ni kama shaba,
Because I knew that you were obstinate, your neck muscles tight as iron, and your forehead like bronze,
5 Hivyo basi nilitangaza vitu hivi kabla havijatokeo hivyo, nilikujulisha wewe, 'Sanamu yangu imefanya haya au sanamu yangu ya kuchonga na sanamu yangu ya kuyeyusha, yamekwishisha vitu.
therefore I declared these things to you beforehand; before they happened I informed you, so you could not say, 'My idol has done them,' or 'My carved figure and my cast metal figure has ordained these things.'
6 Umesikia kuhusu mambo haya; angalia ushahidi wote; na wewe, Je hautakubali kwamba ninacho kisema ni cha kweli? Kuanzia sasa na kuendelea Nitawaonyesha vitu vipya, mambo yaliyofichika ambayo hamkuyajua.
You heard about these things; look at all this evidence; and you, will you not admit what I said is true? From now on, I am showing you new things, hidden things that you have not known.
7 Sasa, na sio yaliyopita, yamekuwa sasa, na kabla ya leo hamkusikia kuhusu wao, hivyo hautaweza kusema, 'Ndio, nilijua kuhusu wao.'
Now, and not from previously, they come into being, and before today you have not heard about them, so you will not be able to say, 'Yes, I knew about them.'
8 Haukusikia; haukuelewa; haya mambo hayakufuniliwa katika masikio kabla ya. Maana nilijua kwamba umekuwa mdanganyifu, na kwamba umekuwa muasi kutoka kuzaliwa.
You never heard; you did not know; these things were not unfolded to your ears beforehand. For I knew that you have been very deceitful, and that you have been a rebel from birth.
9 Kwa niaba ya jina langu nitahairisha asira yangu, na kwa heshima yangu nitajizuia kutokumuharibu yeye.
For the sake of my name I will defer my anger, and for my honor I will hold back from destroying you.
10 Tazama, Mimi niliwaandaa ninyi, lakini sio kama fedha; Nimekusafisha wewe katika tanuru la mateso.
Look, I refined you, but not as silver; I have purified you in the furnace of affliction.
11 Kwa niaba yangu, kwa niaba yangu nitafanya; maana ni kwa jinsi gani niruhusu jina langu lisiheshimike? Sitampa utukufu wangu mtu yeyote.
For my own sake, for my own sake I will act; for how can I allow my name to be profaned? I will not give my glory to anyone else.
12 Nisikilize mimi, Yakobo, na Israeli niliyekuita: Mimi ndiye; Mimi ni wa kwanza, na pia wa mwisho.
Listen to me, Jacob, and Israel, whom I called: I am he; I am the first, I also am the last.
13 Ndio, mkono wangu umeweka msingi wa nchi, na mkono wangu wa kuume ulizitawanya mbingu, zimesimama juu kwa pamoja.
Yes, my hand laid the foundation of the earth, and my right hand spread out the heavens; when I call to them, they stand up together.
14 Jikusanyeni wenyewe, nyinyi nyote, na sikilizeni; ni nani miongoni mwenu atangazaye mambo haya? Yahwe atakamilisha lengo lake dhidi ya Babeli. Atachukua mapenzi ya Yahwe dhidi ya wa Wakaldayo.
Assemble yourselves, all of you, and listen! Who among you has announced these things? Yahweh's ally will accomplish his purpose against Babylon. He will carry out Yahweh's will against the Chaldeans.
15 Mimi, nimezungumza, ndio, nimemchagua yeye, nimemleta yeye, na yeye atafanikiwa.
I, I have spoken, yes, I have summoned him, I have brought him, and he will succeed.
16 Sogea karibu na mimi, sikiliza hili; kutoka mwanzo sikuzungumza katika siri; lakini ilipotokea, Mimi niko hapa; na sasa Bwana Mungu amenituma mimi, na Roho wake.''
Come near to me, listen to this: From the beginning I have not spoken in secret; when it happens, I am there.” Now the Lord Yahweh has sent me, and his Spirit.
17 Yahwe asema hivi, Mkombozi wenu, Mtakatifu wa Israeli anasema, ''Mimi ni Yahwe Mungu wenu, ninayewafundisha juu ya kufanikiwa, ninayewaonyesha njia mtakayoiptia.
This is what Yahweh, your Redeemer, the Holy One of Israel says, “I am Yahweh your God, who teaches you how to succeed, who leads you by the way that you should go.
18 Ikiwa kama mtaheshimu amri zangu! Hivyo amani na maendeleo yatatiririka kama mto, na wokovu wenu ni kama mawimbi kwenye bahari.
If only you had obeyed my commandments! Then your peace and prosperity would have flowed like a river, and your salvation like the waves of the sea.
19 Watoto wako watakuwa wengi kama mchanga, na watoto kutoka kwenye tombo zenu watakuwa wengi kama nafaka kwenye mchanga; majina yao hayataondolewa wala kufutwa mbele yangu.
Your descendants would have been as numerous as the sand, and the children from your womb as numerous as the grains of sand; their name would not have been cut off nor blotted out from before me.
20 Tokeni nje ya Babeli! wakimbieni Wakaldayo! kwa sauti ya kupiga kelele tangaza kwamba! hakikisha hili linajulikana, hakikisha hili linafika mpaka miisho ya nchi! sema 'Yahwe amemkomboa Yakobo mtumishi wake.
Come out from Babylon! Flee from the Chaldeans! With the sound of a ringing cry announce it! Make this known, make it go out to the ends of the earth! Say, 'Yahweh has redeemed his servant Jacob.'
21 Hawakupatwa na kiu alipowaongoza katika jangwa, alifanya maji kutokea kwenye mwamba kwa ajili yao; aliugawa na kufungua mwamba, na maji yakatoka nje.
They did not thirst when he led them through the deserts; he made the water to flow out of the rock for them; he split open the rock, and the waters gushed out.
22 Hakuna amani kwa watenda makosa- amesema Yahwe.''
There is no peace for the wicked—says Yahweh.”

< Isaya 48 >