< Isaya 38 >

1 Siku zile Hezekia alikuwa anaumwa karibia na kufa. Hivyo Isaya mtoto wa Amozi, nabii alikuja kwake na kumwambia, ''Yahwe amesema, 'panga mambo yako maana utakufa, hautaishi.'
In those days was Hezekiah sick and near death. Isaiah [Salvation of Yah] the prophet, the son of Amoz, came to him, and said to him, “Adonai says, ‘Enjoin your house, set it in order, for you will die, and not live.’”
2 'Halafu Hezekia akaugeukia ukuta na akamuomba Yahwe.
Then Hezekiah turned his face to the wall and prayed to Adonai,
3 Na akasema, ''samahani Yahwe, kumbuka jinsi nilivyoenenda kwa uaminifu mbele zako kwa moyo wangu wote, na jinsi nilivyofanya matendo mema katika macho yako.'' Na Hezekia akalia kwa sauti.
and said, “Remember now, Adonai, I beg you, how I have walked before you in truth and with a perfect heart, and have done that which is good in your sight.” Hezekiah wept bitterly.
4 Basi neno la Yawe likamjia Isaya, na kusema,
Then Adonai’s word came to Isaiah [Salvation of Yah], saying,
5 ''Nenda ukamwambie Hezekia, kiongozi wa watu wangu, ''Hivi ndivyo Yahwe, Mungu wa Daudi babu yenu, amesema: Nimeyasikiliza maombi yako, na nimeyaona machozi yako. Ona ninakaribia kuongeza miaka kumi na tano katika maisha yako.
“Go, and tell Hezekiah, ‘Adonai says, the God of David [Beloved] your father, “I have sh'ma ·heard obeyed· your prayer. I have seen your tears. Behold, I will add fifteen years to your life.
6 Na nitakukomboa wewe pamoja mji huu kutoka kwenye mkono wamfalme wa Asiria, na nitaulinda huu mji.
I will deliver you and this city out of the hand of the king of Assyria [Level plain], and I will defend this city.
7 Na hii itakuwa alama kwako kutoka kwangu, Yahwe, kwamba nitafanya nilichokisema:
This shall be the sign to you from Adonai, that Adonai will do this thing that he has spoken.
8 Angalia, nitasababisha kimvuli katika nyumba ya Ahazi kwenda nyuma hautua kumi.'' hivvyo basi kivuli kilirudi nyuma hatua kumi juu ya nyumba iliyopanda juu.
Behold, I will cause the shadow on the sundial, which has gone down on the sundial of Ahaz with the sun, to make teshuvah ·complete return· backward ten steps. So the sun returned ten steps on the sundial on which it had gone down.”’”
9 Haya ndiyo maandishi ya maombi ya Hezekia mfalme wa Yuda, alipokuwa anaumwa halafu akapona:
The writing of Hezekiah king of Judah [Praised], when he had been sick, and had recovered of his sickness.
10 ''Nimesema kwamba nusu ya maisha yangu nitapita katika mlango wa kuzimu; Nilitumwa pale miaka yangu yote. (Sheol h7585)
I said, “In the middle of my life I go into the gates of Sheol ·Place of the dead·. I am deprived of the residue of my years.” (Sheol h7585)
11 Nikasema sitamuona tena Yahwe, Yahwe kaika nchi ninayoishi; sitaangalia watu tena au wenyeji wa dunia hii.
I said, “I won’t see Yah, Yah in the land of the living. I will see man no more with the inhabitants of the world.
12 Maisha yangu yameondolea na kupelekwa mbali na mimi kama hema la mchungaji; Niliyakunja maisha yangu juu kama mfumaji; ameniondoa katika kifungo; kati ya mchana na usiku ameyakomesha maisha yangu.
My dwelling is removed, and is carried away from me like a shepherd’s tent. I have rolled up, like a weaver, my life. He will cut me off from the loom. From day even to night you will make an end of me.
13 Nililia mpaka asubuhi; kama simba anaivunja mifupa yangu. Kati ya usiku na mchana ameyakomesha maisha yangu.
I waited patiently until morning. He breaks all my bones like a lion. From day even to night you will make an end of me.
14 Kama mbayuwayu ndivyo nilivyolia; nililia kama njiwa; macho yangu yalichoka kuangalia juu. Bwana ninateseka; nisaidie mimi.
I chattered like a swallow or a crane. I moaned like a dove. My eyes weaken looking upward. Lord, I am oppressed. Be my security.”
15 Niseme nini? wote wameongea na mimi na amefanya hivyo; Nitatembea taratibu miaka yangu yote maana ninayashinda kwa huzuni.
What will I say? He has both spoken to me, and himself has done it. I will walk carefully all my years because of the anguish of my soul.
16 Bwana, mateso uliyoyatuma ni mazuri kwangu; ikiwezekana nirudishiwe tena maisha yangu; umeyahifadhi maisha maisha yangu na afya yangu.
Lord, men live by these things; and my spirit finds life in all of them: you restore me, and cause me to live.
17 Ni kwa faida yangu kwamba nimwpitia huzuni kama hii. Umenikomboa kutoka kwenye shimo la uharibifu; maana umetupa dhambi zangu nyuma yako.
Behold, for peace I had great anguish, but you have in chasak ·desire, to make bands· for my soul delivered it from the pit of corruption; for you have cast all my sins behind your back.
18 Maana kuzimu hapata kushukuru wewe; kifo hakikusifu wewe; wale wote waendao ndani ya shimo hawana matumaini ya uaminifu wako. (Sheol h7585)
For Sheol ·Place of the dead· can’t yadah ·extend hands in thankful praise· unto you. Death can’t celebrate you. Those who go down into the pit (of Abbadon, the unrighteous side of Sheol) can’t hope for your truth. (Sheol h7585)
19 Mtu anayeishi, mtu anayeishi, ndiye anayekushukuru wewe, kama ninavyofanya leo; baba atawjulisha watoto uaminifu wako.
The living, the living, he shall yadah ·extend hands in thankful praise· to you, as I do today. The father shall make known your truth to the children.
20 Yahwe anakarbia kunikomboa mimi, na tutasherekea kwa mziki siku zote za maisha yetu katika nyumba ya Yahwe.''
Adonai will save me. Therefore we will sing my songs with stringed instruments all the days of our life in Adonai’s house.
21 Sasa Isaya alisema, ''Waacheni wachukue donge mitini na kuliweka kweye jipu naye atapona.
Now Isaiah [Salvation of Yah] had said, “Let them take a cake of figs, and lay it for a poultice on the boil, and he shall recover.”
22 ''Hezekia pia alisema, ''Je ni ishara gan ya kwamba nitaiende juu katika nyumba ya Yahwe?''
Hezekiah also had said, “What is the sign that I will go up to Adonai’s house?”

< Isaya 38 >