< Isaya 33 >

1 Ole wenu, waharibifu ambao hamjaharibiwa! Ole wao wasaliti ambao hamjaslitiwa! Pindi mtakapoacha uaribifu, nanyi mtaharibiwa. Pindi mtakapoacha usaliti, nayi mtasalitiwa.
woe! to ruin and you(m. s.) not to ruin and to act treacherously and not to act treacherously in/on/with him like/as to finish you to ruin to ruin like/as to cease you to/for to act treacherously to act treacherously in/on/with you
2 Yahwe, tuurumie sisi; tumekusubiri wewe; umekuwa mkono wetu kila asubuhi, na wokovu wetu katika kipindi cha mateso.
LORD be gracious us to/for you to await to be arm their to/for morning also salvation our in/on/with time distress
3 Watu wamekimbia kwa kusikia sauti kubwa; uliponyanyuka, mataifa yametawanyika,
from voice: sound crowd to wander people from uplifting your to disperse nation
4 Mateka wako wamejikusanya kama mkasanyiko wa nzige; kama nzige warukavyo, watu wataruka juu yake.
and to gather spoil your gathering [the] locust like/as rushing locust to rush in/on/with him
5 Yahwe ameinuliwa. Anaishi mahali pa juu. Ataijaza Sayuni kwa haki na usawa.
to exalt LORD for to dwell height to fill Zion justice and righteousness
6 Atakuwa imara katika kipidi chenu, wingi wa wokovu, busara, na maarifa; hofu ya Yahwe iko katika hazina yake.
and to be faithfulness time your wealth salvation wisdom and knowledge fear LORD he/she/it treasure his
7 Tazama, wujumbe wanalia mtaani; wanadiplomasia wanamatumaini ya amani kwa kulia kwa uchungu.
look! hero their to cry outside [to] messenger peace bitter to weep [emph?]
8 Barabara kuu imeachwa faragha; hakuna wasafiri tena. Maagano yamevujika, mashahidi wanadharaulika, na utu wa mtu hauheshimiki.
be desolate: destroyed highway to cease to pass way to break covenant to reject city not to devise: count human
9 Nchi imeomboleza na kunyaukia mbali; Lebanoni inaibisha na kunyaukia mbali; Sharoni imekuwa kama jangwa wazi; Bashani na Kermeli zimepuputisha majani yake.
to mourn to weaken land: country/planet be ashamed Lebanon to decay to be [the] Sharon like/as Arabah and to shake Bashan and Carmel
10 ''Sasa nitanyanyuka, ''asema Yahwe; '' sasa nitanyanyuliwa juu; sasa nitainuliwa.
now to arise: rise to say LORD now to exalt now to lift: raise
11 Utashika mimba ya makapi na utazaa mabua; na punzi yako ni moto ambao utakuunguza wewe.
to conceive chaff to beget stubble spirit: breath your fire to eat you
12 Watu watachomwa na kuwa kama chokaa, kama miiba ya porini inavyokatwa na kuchomwa.
and to be people burning lime thorn to cut in/on/with fire to kindle
13 Enyi mlio mbali sana, sikiliza nilicho kifanya; na enyi mlio karibu, kirini ukuu wangu.''
to hear: hear distant which to make: do and to know near might my
14 Watenda zambi wa Sayuni wanogopa; tetemeko limewakuta wasio na Mungu. Ni nani miongoni mwetu anayeweza kukaa kwenye moto mkali? Na ni nani miongoni mwetu anayeweza kukaa kwenye moto wa milele?
to dread in/on/with Zion sinner to grasp trembling profane who? to sojourn to/for us fire to eat who? to sojourn to/for us burning forever: enduring
15 Nyie mnaotembe katika haki na kuongea kw uaminifu; yeye anayedharau mapato ya ukandamizaji, yeye anayekataa kuchuka rushwa, ambaye hausiki kwenye kupanga vurugu za kihalifu, na ambaye haangali maovu-
to go: walk righteousness and to speak: speak uprightness to reject in/on/with unjust-gain oppression to shake palm his from to grasp in/on/with bribe to shutter ear his from to hear: hear blood and to shut eyes eye his from to see: see in/on/with bad: evil
16 Ataiweka nyumba yake juu; sehemu yake ya ulinzi itakuwa ni ngome ya mwamba; chakula na maji yake hayataisha.
he/she/it height to dwell stronghold crag high refuge his food: bread his to give: give water his be faithful
17 Macho yako yatamuona mfalme katika uzuri wake; watatazama nchi kubwa.
king in/on/with beauty his to see eye your to see: see land: country/planet distance
18 Moyo wako utakumbuka hofu; yuko wapi mwandishi, yuko wapi yule aliayepima pesa? na yuko wapi yeye aesabue minara?
heart your to mutter terror where? to recount where? to weigh where? to recount [obj] [the] tower
19 Hautawaona watu wanaopinga, watu weye lugha ya ajabu ambayo hautaweza kuielewa.
[obj] people be fierce not to see: see people unfathomable lip: words from to hear: understand to mock tongue nothing understanding
20 Itazame Sayuni, mji wa sikukuu yetu; macho yako yataiona Yerusalemu kama makao tulivu, hema ambalo halitatolewa, vigingi vyake havitatolewa wala kamba zake hazitakatika.
to see Zion town meeting: festival our eye your to see: see Jerusalem pasture secure tent not to move not to set out peg his to/for perpetuity and all cord his not to tear
21 Badala yake Yahwe katika ukuu wake atakuwa pamoja na sisi, katika eneo la maji mengi na mifereji mingi. Hakuna manuari na mpiga makasia watakayepita hapo, na hakuna mashua itakayopita uko.
that if: except if: except there great LORD to/for us place river stream broad: wide hand: spacious not to go: went in/on/with him fleet oar and ship great not to pass him
22 Maana Yahwe ni hakimu wetu, Yahwe ni mwanasheria wet, Yahwe ni mfalme wetu; atatukomboa sisi.
for LORD to judge us LORD to decree us LORD king our he/she/it to save us
23 Kamba zako zimelegea; haziwezi kushika mlingoti katika eneo lake; haziwezi kuzunguka meli; pindi mateka wanavyogawanyika, hata vilema watawatoa nje kama mateka.
to leave cord your not to strengthen: hold stand mast their not to spread ensign then to divide prey spoil abundance lame to plunder plunder
24 Na wenyeji watasema, ''Ninaumwa;'' watu wanaoishi pale watasamehewa maovu yao.
and not to say neighboring be weak: ill [the] people [the] to dwell in/on/with her to lift: forgive iniquity: crime

< Isaya 33 >