< Isaya 32 >

1 Tazama, mfalme atatawala kwa haki, wakuu wataongoza kwa haki.
Look, a king shall reign in righteousness, and princes shall rule in justice.
2 Kila mmoja atakuwa kama makazi kutoka kwenye upepo na kimbilio kutoka kwenye dhoruba, kama mifereji kwenye sehemu kavu, kama kivuli kwenye mwamba mkubwa katika nchi iliyochoka.
A man shall be as a hiding place from the wind, and a shelter from the storm, as streams of water in a dry place, as the shade of a large rock in a weary land.
3 Halafu macho ya waie wanaoona hayataona giza, na masikio ya wale wanosikia yatasikia vizuri.
The eyes of those who see will not be dim, and the ears of those who hear will listen.
4 Wenye upele watafikiria kwa makini kwa uelewa wao, na wenye kigugumizi watazungumza dhahiri na kwa urahisi.
The heart of the rash will understand knowledge, and the tongue of the stammerers will be ready to speak plainly.
5 Mjinga hataitwa tena muheshimiwa, wala muongo hataitwa mkuu.
And they will no longer call a fool noble, nor the scoundrel be highly respected.
6 Maana mjinga anazungumza ujinga, na moyo wake unapanga maovu na matendo ya wasiomcha Mungu, na anaongea mambo mabaya kuhusu Yahwe. Na anawafanya wenye njaa kuwa tupu na wenye kiu kukosa maji
For the fool will speak folly, and his heart plans iniquity, to practice profanity, and to utter error against Jehovah, To make empty the soul of the hungry, and to cause the drink of the thirsty to fail.
7 Njia ya muongo ni maovu. Anajua kubuni mipango mibaya ya kuwalagai masikini kwa uongo, na hata kama masikini atazungumza ukweli.
The ways of the scoundrel are evil. He devises wicked devices to destroy the humble with lying words, even when the needy speaks right.
8 Lakini watu wa heshima wanapanga mipango ya kuheshimika; na kwa sabaubau ya matendo ya wenye heshima tuatasimama.
But the noble devises noble things; and he will continue in noble things.
9 Nyanyukeni juu, enyi wanawake mlio wepesi, na sikilizeni sauti yangu; enyi mabinti msiowangalifu, nisikilizeni mimi.
Rise up, you women who are at ease. Hear my voice. You careless daughters, give ear to my speech.
10 Maana kwa mda mfupi zaidi ya mwaka ujasiri wenu utavunjika, nyie wanawake msiojali, maana mavuno ya zabibu yatakwama, mavuno hayatakuwepo.
For days beyond a year you will be troubled, you careless women; for the vintage shall fail. The harvest won't come.
11 Tetemekeni, enyi wanawake, mliowadhaifu; taabikeni enyi msikuwa wangalifu; ondoeni nguo zenu nzuri mbaki wazi;
Tremble, you women who are at ease. Be troubled, you careless ones. Strip yourselves, make yourselves naked, and put sackcloth on your waist.
12 Vaeni nguo za magunia katika viuno vyenu. Ole watakaojichukulia mashamba mazuri, kwa mzabibu ulio zaa sana.
Beat your breasts for the pleasant fields, for the fruitful vine.
13 Kwenye aridhi ya watu wangu kutamea miiba na mbigiri, hata juu ya nyumba za furaha na mji ulio na shangwe.
Thorns and briars will come up on my people's land; yes, on all the houses of joy in the joyous city.
14 Maana jumba litaachwa, mji uliosongamana utakuwa faragha; kilima na mnara vitakuwa mapango daima, furaha ya punda, malisho ya mifugo;
For the palace will be forsaken. The populous city will be deserted. The hill and the watchtower will be for dens forever, a delight for wild donkeys, a pasture of flocks;
15 mpaka roho itushukie sisi kutoka juu, na jangwa litakuwa shamba linalozaa, na shamba linalozaa litachukuliwa kama msitu.
Until the Spirit is poured on us from on high, and the wilderness becomes a fruitful field, and the fruitful field is considered a forest.
16 Wenye haki wataishi jangwani; na wenye haki wataishi katika shamba linalozaa matunda.
Then justice will dwell in the wilderness; and righteousness will remain in the fruitful field.
17 Kazi ya mwenye haki itakuwa ni ya amani; na matokeo ya wenye haki, ni utulivu na kujiamini daima.
The work of righteousness will be peace; and the effect of righteousness, quietness and confidence forever.
18 Watu wangu wataishi katika makao ya amani, na katika nyumba salama na mahali tulivu pa kupumzikia.
My people will abide in a peaceful habitation, in safe dwellings, and in quiet resting places.
19 Lakini hata kama ni mvua ya mawe na msitu umeharibiwa, na mji umeteketezwa,
And it will hail when the forest comes down, and the wood is brought low in humiliation.
20 yule ambae anaye panda pembezoni mwa mifereji atabarikiwa, na yule atakaye wapeleka ng'ombe na punda kuchunga.
Blessed are you who sow beside all waters, who set free the foot of the ox and the donkey.

< Isaya 32 >