< Isaya 2 >

1 Vitu ambavyo Isaya mtoto Amozi alivijua katika maono, kuhusu Yuda na Yerusalemu.
This is what Isaiah [Salvation of Yah] the son of Amoz saw concerning Judah [Praised] and Jerusalem [City of peace].
2 Na itakuwa katika siku za mwisho, ule mlima wa nyumba ya Yahwe itaanzishwa kama mlima mrefu zaidi, na utanyanyuliwa juu ya vilima, na mataifa yote yatakusanyika pale.
It shall happen in the latter days, that the mountain of Adonai’s house shall be established on the top of the mountains, and shall be raised above the hills; and all nations shall flow to it.
3 Watu wengi watakuja na kusema, ''Njooni, twendeni juu ya mlima wa Yahwe, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo, kwa hiyo anaweza kutufundisha baadhi ya njia zake na tunaweza kutembea katika njia zake.'' Nje ya Sayuni itaenda sheria na neno la Yahwe litatoka Yerualemu.
Many peoples shall go and say, “Come, let’s go up to the mountain of Adonai, to the house of the God of Jacob [Supplanter]; and he will teach us of his ways, and we will walk in his paths.” For out of Zion [Mountain ridge, Marking] Torah ·Teaching· shall go forth, and Adonai’s word from Jerusalem [City of peace].
4 Atahukumu kati ya mataifa na atatoa maamuzi kwa watu wote; watayapiga nyungo mapanga yao kuwa majembe, na mikiku yao kama ya kukatia ndoano; taifa halitanyanyua upanga juu ya taifa lingine, na wala hawata jiandaa kwa vita tena.
He will judge between the nations, and will decide concerning many peoples; and they shall beat their swords into plowshares, and their spears into pruning hooks. Nation shall not lift up sword against nation, neither shall they learn war any more.
5 Nyumba ya Yakobo, njooni, na tutembee katika mwanga wa Yahwe.
House of Jacob [Supplanter], come, and let us walk in the light of Adonai.
6 Kwa maana mmewatekeleza watu wenu, nyumba ya Yakobo, wamejazwa na desturi kutoka mashariki na dalili kutokea kama mfilisti, na watasalimiana kwa mikono na wana wa wageni.
For you have forsaken your people, the house of Jacob [Supplanter], because they are filled from the east, with those who practice divination like the Philistines [To roll in dust (As an insult)], and they clasp hands with the children of foreigners.
7 Nchi yao imejaa fedha na dhahabu, na hakuna mipaka katika utajiri wao; nchi yao pia imejaa farasi, wala hakuna mipika ya magari.
Their land is full of silver and gold, neither is there any end of their treasures. Their land also is full of horses, neither is there any end of their chariots.
8 Nchi yao pia imejaa sanamu; wanaabu utengenezaji wa mikono yao wenyewe, vitu aambavyo vidole vyao vimetengeneza.
Their land also is full of idols. They worship the work of their own hands, that which their own fingers have made.
9 Watu watainama chini, na kila mmoja atanguka chini; hivyo basi msiwanyanyue juu.
Man is brought low, and mankind is humbled; therefore don’t forgive them.
10 Nendeni maeneo yenye miamba na mjifiche kwenye aridhi kwa hofu ya Yahwe na kwa utukufu wa enzi yake.
Enter into the rock, and hide in the dust, to escape from the terror of Adonai, and from the glory of his majesty.
11 Mtu anaye tazama kwa kujivuna atashushw chini, na kiburi cha watu kitashushwa chini, na Yahwe mwenyewe atainuliwa siku hiyo.
The lofty looks of man will be brought low, the haughtiness of men will be bowed down, and Adonai alone will be exalted in that day.
12 Maana kutakuwa na siku ya Yahwe wa majeshi juu ya yeyote anayejigamba na kujiinua juu, na dhidi ya yeyote mwenye kiburi na atashushwa chini-
For there will be a day of Adonai Tzva'ot [Yahweh Commander of heaven’s armies] for all that is proud and haughty, and for all that is lifted up; and it shall be brought low:
13 na dhidi ya mierezi ya Lebanoni iliyo juu na kupandishwa juu, na dhidi ya mialoni ya Bashani.
For all the cedars of Lebanon, that are high and lifted up, for all the oaks of Bashan,
14 Siku hiyo ya Yahwe wa majeshi itakuwa dhidi ya milima yote mirefu, na dhidi ya vilima vyote vilivyonyanyuliwa juu,
For all the high mountains, for all the hills that are lifted up,
15 na dhidi ya minara mirefu, na dhidi ya kila ukutaunaojitokeza,
For every lofty tower, for every fortified wall,
16 na dhidi ya merikebu zote za Tarshishi, na dhidi ya vyombo vizuri vya meli.
For all the ships of Tarshish, and for all pleasant imagery.
17 Kiburi cha mwanaume kitashushwa chini, na kiburi cha wanaume kitaanguka; Yahwe mwenyewe atainuliwa siku hiyo.
The loftiness of man shall be bowed down, and the haughtiness of men shall be brought low; and Adonai alone shall be exalted in that day.
18 Sanamu zote zitaondolewa.
The idols shall utterly pass away.
19 Wanaume wataingia kwenye mapango ya miamba na mashimo ya aridhi, kwa hofu ya Yahwe, na kwa utukufu wa enzi yake, atakapo nyanyuka na kuitisha nchi.
Men shall go into the caves of the rocks, and into the holes of the earth, to escape from the terror of Adonai, and from the glory of his majesty, when he arises to shake the earth mightily.
20 Siku hiyo watu watatupa sanamu zao za fedha na dhahabu ambazo wametengeneza wenyewe kwa ajili ya kuabudia - watazitupa mbali kwa fuko na popo.
In that day, men shall cast away their idols of silver, and their idols of gold, which have been made for themselves to worship, to the moles and to the bats;
21 Watu wataingia kwenye miamba kupitia mwanya itakuwa miamba chakavu, kwa hofu ya Yahwe na utukufu wa enzi yake,
To go into the caverns of the rocks, and into the clefts of the ragged rocks, to escape from the terror of Adonai, and from the glory of his majesty, when he arises to shake the earth mightily.
22 usimwaminia mtu, ambae pumzi yake inatokea katika pua yake, ni kwa kiasi gan?
Stop trusting in man, whose breath is in his nostrils; for of what account is he?

< Isaya 2 >