< Isaya 12 >

1 Siku hiyo utasema, ''Nitakushukuru wewe, Yahwe. Japo ulikuwa na hasira na mimi, laana yako imeondoka mbali, na umenifariji mimi,
In that day you will say, “I will give thanks to you, Adonai; for though you were angry with me, your anger has turned away and you comfort me.
2 Ona Bwana ni wokovu wangu; nitamwamini na sitakuwa na hofu, kwa Yahwe, ndio, Yahwe ni nguvu yangu na wimbo wangu. Amekuwa wokovu wangu.''
Behold, God is my yishu'ah ·salvation·. I will trust, and will not be afraid; for Yah, Adonai, is my strength and song; and he has become my salvation.”
3 Kwa furaha utachota maji kwenye kisima cha wokovu.
Therefore with joy you will draw water out of the wells of yishu'ah ·salvation·.
4 Siku hiyo utasema, ''Mshukuru Yahwe na ita jina lake; tangaza matendo yake miongoni mwa watu, tangaza jina lake limeinuliwa.
In that day you will say, “Yadah ·Extend hands in thankful praise· to Adonai! Call on his name. Declare his doings among the peoples. Proclaim that his name is exalted!
5 Mwiimbie Yahwe, maana ametenda matendo yaliotukuka; acha hili lijulikane dunia nzima.
Sing zahmar ·musical praise· to Adonai, for he has done excellent things! Let this be known in all the earth!
6 Lia kwa nguvu na piga kelele kwa furaha, enyi wakazi wa Sayuni, maana katikati yenu ni mtakatifu wa Israeli.
Cry aloud and shout, you inhabitant of Zion [Mountain ridge, Marking]; for the haKadosh Isra'el [the Holy One of God prevails] is great among you!”

< Isaya 12 >