< Isaya 12 >

1 Siku hiyo utasema, ''Nitakushukuru wewe, Yahwe. Japo ulikuwa na hasira na mimi, laana yako imeondoka mbali, na umenifariji mimi,
In that day you will say, "I will give thanks to you, the LORD; for you were angry with me, but your anger has turned away and you comfort me.
2 Ona Bwana ni wokovu wangu; nitamwamini na sitakuwa na hofu, kwa Yahwe, ndio, Yahwe ni nguvu yangu na wimbo wangu. Amekuwa wokovu wangu.''
Look, in the God of my salvation I will trust, and will not be afraid. For the LORD is my strength and my song, and he has become my salvation."
3 Kwa furaha utachota maji kwenye kisima cha wokovu.
Therefore with joy you will draw water out of the wells of salvation.
4 Siku hiyo utasema, ''Mshukuru Yahwe na ita jina lake; tangaza matendo yake miongoni mwa watu, tangaza jina lake limeinuliwa.
In that day you will say, "Give thanks to the LORD. Call on his name. Declare his doings among the peoples. Proclaim that his name is exalted.
5 Mwiimbie Yahwe, maana ametenda matendo yaliotukuka; acha hili lijulikane dunia nzima.
Sing to the LORD, for he has done excellent things. Let this be known in all the earth.
6 Lia kwa nguvu na piga kelele kwa furaha, enyi wakazi wa Sayuni, maana katikati yenu ni mtakatifu wa Israeli.
Cry aloud and shout, you inhabitant of Zion; for the Holy One of Israel is great in the midst of you."

< Isaya 12 >