< Isaya 12 >

1 Siku hiyo utasema, ''Nitakushukuru wewe, Yahwe. Japo ulikuwa na hasira na mimi, laana yako imeondoka mbali, na umenifariji mimi,
And in that day thou shalt say: 'I will give thanks unto Thee, O LORD; for though Thou was angry with me, Thine anger is turned away, and Thou comfortest me.
2 Ona Bwana ni wokovu wangu; nitamwamini na sitakuwa na hofu, kwa Yahwe, ndio, Yahwe ni nguvu yangu na wimbo wangu. Amekuwa wokovu wangu.''
Behold, God is my salvation; I will trust, and will not be afraid; for GOD the LORD is my strength and song; and He is become my salvation.'
3 Kwa furaha utachota maji kwenye kisima cha wokovu.
Therefore with joy shall ye draw water out of the wells of salvation.
4 Siku hiyo utasema, ''Mshukuru Yahwe na ita jina lake; tangaza matendo yake miongoni mwa watu, tangaza jina lake limeinuliwa.
And in that day shall ye say: 'Give thanks unto the LORD, proclaim His name, declare His doings among the peoples, make mention that His name is exalted.
5 Mwiimbie Yahwe, maana ametenda matendo yaliotukuka; acha hili lijulikane dunia nzima.
Sing unto the LORD; for He hath done gloriously; this is made known in all the earth.
6 Lia kwa nguvu na piga kelele kwa furaha, enyi wakazi wa Sayuni, maana katikati yenu ni mtakatifu wa Israeli.
Cry aloud and shout, thou inhabitant of Zion, for great is the Holy One of Israel in the midst of thee.'

< Isaya 12 >