< Hosea 1 >

1 Hili ni neno la Bwana lililofika kwa Hosea mwana wa Beeri siku za Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na katika siku za Yeroboamu mwana wa Yoashi, mfalme wa Israeli.
[the] word of Yahweh - which it came to Hosea [the] son of Beeri in [the] days of Uzziah Jotham Ahaz Hezekiah [the] kings of Judah and in [the] days of Jeroboam [the] son of Joash [the] king of Israel.
2 Wakati Bwana alipozungumza kwanza kupitia Hosea, akamwambia, “Nenda ukajitwalie mke ambaye ni kahaba. Atakuwa na watoto ambao ni matokeo ya ukahaba wake. Kwa maana nchi inafanya uzinzi mkubwa kwa kumwacha Bwana.”
[the] beginning [when] he spoke Yahweh by Hosea. And he said Yahweh to Hosea go take for yourself a wife of prostitution and children of prostitution for continually it prostitutes itself the land from after Yahweh.
3 Basi Hosea akaenda akamwoa Gomeri binti Diblaimu, naye akachukua mimba, akazaa mtoti mwanamume.
And he went and he took Gomer [the] daughter of Diblaim and she conceived and she bore to him a son.
4 Bwana akamwambia Hosea, Mwite jina lake Yezreeli. Kwa maana kwa muda mfupi nitaiadhibu nyumba ya Yehu kwa sababu ya kumwaga damu huko Yezreeli; nami nitamaliza ufalme wa nyumba ya Israeli.
And he said Yahweh to him call name his Jezreel for yet a little and I will visit [the] blood of Jezreel on [the] house of Jehu and I will put an end to [the] kingdom of [the] house of Israel.
5 Itatokea siku ile nitakapovunja upinde wa Israeli katika bonde la Yezreeli.
And it will be on the day that and I will break [the] bow of Israel in [the] valley of Jezreel.
6 Gomeri akachukua mimba tena akamzaa binti. Ndipo Bwana akamwambia Hosea, “Mwite jina lake Lo Ruhama; kwa maana sitawahurumia tena nyumba ya Israeli, nisije nikawasamehe kwa njia yoyote.
And she conceived again and she bore a daughter and he said to him call name her Lo-Ruhamah for not I will repeat again I will have compassion on [the] house of Israel that certainly I will forgive them.
7 Hata hivyo nitawahurumia nyumba ya Yuda, nami nitawaokoa mwenyewe, Bwana, Mungu wao. Sitawaokoa kwa upinde, upanga, vita, farasi, au wapanda farasi. '
And [the] house of Judah I will have compassion on and I will save them by Yahweh God their and not I will save them by bow and by sword and by battle by horses and by horsemen.
8 Baada ya Gomeri kumwachisha Lo Ruhama, alipata mimba na kuzaa mtoto mwingine mwanamume.
And she weaned Lo-Ruhamah and she conceived and she bore a son.
9 Ndipo Bwana akasema, “Mwite jina la Lo Ami; kwa kuwa ninyi si watu wangu, wala mimi si Mungu wenu.”
And he said call name his Lo-Ammi for you not [are] people my and I not I will belong to you.
10 Hata hivyo idadi ya watu wa Israeli itakuwa kama mchanga wa bahari, ambayo haiwezi kupimwa au kuhesabiwa. Itakuwa pale ambapo waliambiwa, “Ninyi si watu wangu,” wataambiwa, “Ninyi ni watu wa Mungu aliye hai.”
And it will be [the] number of [the] people of Israel like [the] sand of the sea which not it will be measured and not it will be counted and it will be in [the] place where it was said to them not [are] people my you it will be said to them children of [the] God living.
11 Watu wa Yuda na watu wa Israeli watakusanyika pamoja. Wao wataweka kiongozi mmoja wao wenyewe, na watatoka kutoka nchi, kwa maana itakuwa siku ya Yezreeli kuu.
And they will be gathered [the] people of Judah and [the] people of Israel together and they will appoint for themselves a chief one and they will go up from the land for [will be] great [the] day of Jezreel.

< Hosea 1 >